Wimbo Na. 82
Igeni Upole wa Kristo
Makala Iliyochapishwa
1. Bwana Yesu hakuwa na kiburi;
Hakujitakia makuu kamwe.
Alikuwa na jukumu muhimu;
Lakini kajishusha sikuzote.
2. Nyote mulio na mahangaiko,
Ichukueni nira yake Kristo.
Mutapata burudisho la nafsi;
Bwana wetu ana tabia-pole.
3. ‘Nyote ni ndugu,’ kasema Bwanetu.
Musiwe mukitafuta makuu.
Wapole wana thamani kwa Mungu;
Watairithi dunia milele.
(Ona pia Mt. 5:5; 23:8; Met. 3:34; Rom. 12:16.)