Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb17 Machi uku. 8
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
  • Habari Zinazolingana
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Jinsi ya Kutumia Broshua Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
    Huduma ya Ufalme—2013
  • Mambo Makuu ya Sehemu ya 2
    Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
    Huduma ya Ufalme—2013
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2017
mwb17 Machi uku. 8
Dada akizungumzia pamoja na mwanafunzi wa Biblia somo moja katika broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

MAISHA YA MKRISTO

Jinsi ya Kutumia Broshua​—Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Yaliyomo katika broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? ilitayarishwa ili kujifunza na wanafunzi wa Biblia mwanzoni au mwishoni mwa kila kipindi cha funzo la Biblia.a Somo la 1 hadi la 4 linawasaidia wanafunzi kuelewa sisi ni watu wa aina gani, somo la 5 hadi la 14 linawasaidia kujifunza kuhusu utendaji wetu, na somo la 15 hadi la 28 linawaonyesha jinsi tengenezo letu linavyofanya kazi. Ni vizuri kuzungumzia masomo hayo kama yanavyofuatana, lakini ikiwa somo fulani linahusiana na mahitaji ya mwanafunzi ya wakati huo mnaweza kulizungumzia kwanza. Kila somo lina urefu wa ukurasa mmoja tu na linaweza kuzungumziwa kwa dakika tano hadi kumi.

  • Somo la 8 katika broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?

    Anza kwa kukazia swali lililo kwenye kichwa cha somo

  • Someni somo lote pamoja. Mnaweza kusoma mafungu yote kwanza, au msome sehemu moja na kuizungumzia kabla ya kusoma sehemu inayofuata

  • Zungumzieni sehemu mliyosoma. Tumia maswali yanayopatikana katika sehemu ya chini ya ukurasa na picha. Someni na mzungumzie maandiko yaliyotajwa kulingana na uhitaji. Kazia kwamba vichwa vidogo vya habari vilivyoandikwa kwa herufi nzito vinajibu swali kwenye kichwa cha somo hilo

  • Ikiwa somo lina sanduku lenye kichwa “Pata Kujua Mengi Zaidi” soma na mwanafunzi na umtie moyo afuate mapendekezo yaliyotolewa

a Toleo la mtandaoni ndilo toleo la karibuni zaidi la broshua hiyo.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki