Jinsi ya Kutumia Broshua Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo?
Broshua Mpya Iliyokusudiwa Kuwaelekeza Wanafunzi wa Biblia Kwenye Tengenezo
1. Broshua Mapenzi ya Yehova inatimiza mambo gani matatu?
1 Je, umeanza kutumia broshua mpya Ni Nani Wanaofanya Mapenzi ya Yehova Leo? Imekusudiwa (1) kuwasaidia wanafunzi wa Biblia wawafahamu vizuri zaidi Mashahidi wa Yehova, (2) kuwasaidia wajifunze mambo tunayofanya, na (3) kuwaonyesha jinsi tengenezo letu linavyofanya kazi. Broshua Mapenzi ya Yehova ina masomo yaliyo katika kurasa moja moja na yanayoweza kuzungumziwa kwa urahisi kwa dakika tano au kumi baada ya kila funzo.
2. Elezea kuhusu muundo na mambo yaliyomo katika broshua hiyo.
2 Jinsi Ilivyo: Broshua hiyo imegawanywa katika sehemu tatu, kila sehemu inazungumzia mambo tofauti kuhusiana na tengenezo la Yehova kama ilivyotajwa hapo juu. Karibia vichwa vya masomo yote 28 vimeandikwa kama swali, na vichwa vidogo vinavyofuata ambavyo vimeandikwa kwa herufi nzito hujibu swali hilo. Broshua hiyo ina picha zilizochukuliwa kutoka katika nchi zaidi ya 50 zinazoonyesha jinsi kazi yetu ilivyoenea ulimwenguni pote. Katika baadhi ya masomo kuna masanduku yenye kichwa “Pata Kujua Mengi Zaidi,” ambayo yana mapendekezo unayoweza kumtia moyo mwanafunzi wako atumie.
3. Tunaweza kutumiaje broshua Mapenzi ya Yehova?
3 Jinsi Unavyoweza Kuitumia: Anza kwa kumwonyesha swali ambalo ni kichwa cha somo. Kisha, mnaposoma pamoja somo hilo, kazia vichwa vidogo vyenye maandishi mazito. Mwishowe, zungumzia maswali ya pitio yanayopatikana katika sehemu ya chini ya ukurasa. Unaweza kusoma somo lote au kusoma sehemu kadhaa na kuzizungumzia. Unaweza kuamua ni maandiko gani utakayosoma. Usisahau kuzungumzia picha na masanduku yenye kichwa “Pata Kujua Mengi Zaidi.” Kwa kawaida, masomo yanapaswa kuzungumziwa kwa mpangilio. Hata hivyo, uwe huru kuchunguza somo lililo mbele linalozungumzia jambo linalomhusu mwanafunzi wakati huo. Kwa mfano, ikiwa kutakuwa na kusanyiko karibuni, unaweza kuacha somo mnalozungumzia na mjifunze somo la 11.
4. Kwa nini unafurahia kupata broshua hiyo mpya?
4 Tunapojifunza Biblia na mtu fulani, tunamsaidia amjue vizuri Baba yetu wa mbinguni. Hata hivyo, tunahitaji pia kumfundisha kuhusu tengenezo la Yehova. (Met. 6:20) Tunafurahi sana kupata broshua hiyo mpya inayotusaidia kufanya hivyo kwa urahisi!