Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
MACHI 13-19
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YEREMIA 5-7
Yeremia—Nabii wa Hukumu za Mungu Asiyependwa na Wengi
7 “Na hakika wao watapigana dhidi ya wewe,” Yehova akaonya, “lakini wao hawatashinda dhidi ya wewe.” (Yeremia 1:19, NW) Sasa ni kwa sababu gani Wayahudi na watawala wao wangetaka kupigana dhidi ya nabii huyu? Ni kwa sababu ujumbe wake ulishambulia ukinaifu wao na namna yao ya ibada ya kidesturi tu. Yeremia hakulegeza ushambulizi wake: “Tazama! Neno lenyewe la Yehova limekuwa suto kwao, neno ambalo wao hawawezi kupendezwa nalo. Kwa maana kutoka aliye mdogo zaidi kati yao hata kufika kwa aliye mkubwa zaidi kati yao, kila mmoja anajifanyia mwenyewe pato lisilo la haki; na kutoka kwa nabii hata kufika kwa kuhani [watu wale wale ambao wanapaswa kuwa watunza mema ya kiadili na kiroho], kila mmoja anatenda kwa ubandia.”—Yeremia 6:10, 13, NW.
8 Ni kweli, wao walikuwa wakiongoza taifa katika kutoa dhabihu. Wao walikuwa wakifanya-fanya ibada ya kweli kwa njia za kidesturi, lakini mioyo yao haikuwa humo. Kufuata mila za ibada kulikuwa jambo la maana kwao kuliko kufuata mwenendo unaofaa. Wakati ule ule, viongozi wa dini Wayahudi walikuwa wakifanya taifa lile lisinzie katika usingizi wa kudhani lilikuwa na usalama, wakisema, “Kuna amani! Kuna amani!” na hali hakukuwa na amani. (Yeremia 6:14; 8:11, NW) Ndiyo, wao walikuwa wakiwapumbaza watu waitikadi kwamba walikuwa na amani pamoja na Mungu. Wao walihisi kwamba hakukuwa na jambo la kufanyia wasiwasi, kwa maana wao walikuwa watu waokolewa wa Yehova, wenye kumiliki ule mji mtakatifu na hekalu lao. Lakini je! hivyo ndivyo Yehova alivyoiona hali hiyo?
Yeremia—Nabii wa Hukumu za Mungu Asiyependwa na Wengi
9 Yehova aliamuru Yeremia asimame mahali fulani ambapo angeonwa kabisa na watu kwenye lango la hekalu na atoe ujumbe Wake kwa waabudu walioingia humo. Yeye alipaswa kuwaambia hivi: “Msitie itibari yenu katika maneno yenye kukosesha, mkisema, ‘Hekalu la Yehova, hekalu la Yehova, hekalu la Yehova ndivyo walivyo!’ . . . Kwa uhakika hilo halitakuwa lenye manufaa hata kidogo.” Wayahudi walikuwa wakitembea kwa kuona, si kwa imani, huku wakijisifu katika hekalu lao. Tayari wao walikuwa wamesahau maneno ya Yehova ya kutahadharisha hivi: “Mbingu ni kiti cha ufalme changu, na dunia ni kibago cha miguu yangu. Iko wapi, basi, nyumba ambayo ninyi watu mnaweza kunijengea mimi?” Kwa uhakika Yehova, Bwana Mwenye Enzi Kuu wa huu ulimwengu wote mzima ulio mkubwa sana, hakuwekewa mipaka ya kuzuiliwa akae ndani ya hekalu lao, hata kama lilikuwa lenye utukufu kama nini!—Yeremia 7:1-8; Isaya 66:1, NW.
10 Yeremia aliendelea kufanya peupe kemeo lake lenye kuwauma sana: “Je! kunaweza kuwako kuiba, kuua na kufanya uzinzi na kuapa kwa ubandia na kufanya moshi wa kidhabihu kwa Baali na kutembea kwa kufuata miungu mingine ambayo ninyi hamkuwa mmejua, . . . na ni lazima ninyi mseme, ‘Kwa uhakika sisi tutakombolewa,’ na hali mnafanya makuruhi yote haya?” Wayahudi, wakiwa ndio ‘watu wachaguliwa’ wa Mungu, walifikiri yeye angevumilia mwenendo wa aina yo yote, maadamu wao walikuwa wakileta dhabihu zao kwenye hekalu. Hata hivyo, ikiwa fahamu zao zilihisi kwamba yeye alikuwa baba mwenye kuongozwa na misisimuko-sisimuko, mwenye kudekeza-dekeza mtoto wake mmoja tu aliyeharibika kwa kubembelezwa-bembelezwa, wangeshtushwa sana waache kuzubaa.—Yeremia 7:9, 10; Kutoka 19:5, 6, NW.
Kutafuta Hazina za Kiroho
Yeremia—Nabii wa Hukumu za Mungu Asiyependwa na Wengi
Yuda Yalipa Bei
15 Wapata mwaka wa 632 K.W.K., Ashuru ilikuwa imeanguka mikononi mwa Wakaldayo na Wamedi, na Misri ilishindwa ikawa serikali ndogo tu kusini mwa Yuda. Tisho halisi kwa Yuda lingekuja kupitia ile njia ya uvamizi upande wa kaskazini. Hivyo, Yeremia alilazimika kuwapa Wayahudi wenzake habari fulani mbaya! “Tazama! Jamii ya watu inakuja kutoka bara ya kaskazini. . . Hiyo ni yenye ukatili, na wao hawatakuwa na sikitikio. . . . Hiyo imejipanga katika mpangilio wa pigano kama mwanamume wa vita dhidi ya wewe, O binti ya Sayuni.” Serikali kubwa ya ulimwengu iliyokuwa imepanda cheo wakati huo ilikuwa Babuloni. Hiyo ingekuwa ndiyo chombo cha Mungu cha kuadhibia Yuda isiyo na uaminifu.—Yeremia 6:22, 23; 25:8, 9, NW.
MACHI 20-26
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YEREMIA 8-11
it-1 555
Matango
Nguzo, mihimili au vifaa vingine viliwekwa pia kwenye mashamba ili kuwaogopesha wanyama. Nabii Yeremia alitumia vitu hivyo visivyo na uhai na ambavyo haviwezi kusema yaani, “sanamu ya kufukuza ndege ya shamba la matango” kulinganisha sanamu zilizotengenezwa na mataifa yaliyoabudu sanamu.—Yer 10:5.
MACHI 27–APRILI 2
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | YEREMIA 12-16
it-1 1121 ¶2
Viuno
Yehova alizungumza kuhusu nyumba ya Israeli na Yuda kwamba walikuwa kama mshipi kwenye kiuno chake, aliwaweka karibu sana naye, ili wawe sifa na kitu kizuri kwake. (Yer 13:11) Unabii kuhusu utawala wa Yesu Kristo ulionyesha kwamba atakapotawala uadilifu utakuwa kama mshipi wa viuno vyake na uaminifu kama mshipi wa viuno vyake. Hilo linamaanisha kwamba nguvu zote za utendaji za Yesu ni za uadilifu na za uaminifu wakati wote. Kama mshipi unaoimarisha, uadilifu utamwimarisha atakapotenda akiwa Hakimu aliyechaguliwa na Yehova.—Isa 11:1, 5.