MAISHA YA MKRISTO
Upendo wa Kweli Ni Nini?
Yehova alikusudia ndoa iwe muungano wa kudumu kati ya mwanamume na mwanamke. (Mwa 2:22-24) Talaka iliruhusiwa tu mwenzi wa ndoa alipofanya uzinzi. (Mal 2:16; Mt 19:9) Kwa kuwa Yehova anataka ndoa ziwe na furaha, ametoa kanuni zinazoweza kuwasaidia Wakristo kuchagua mwenzi wa ndoa kwa hekima na kudumisha ndoa yenye furaha.—Mhu 5:4-6.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UPENDO WA KWELI NI NINI?, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Kwa nini ushauri ambao Frank na Bonnie walimpa binti yao, Liz, ulikuwa wenye hekima na upendo?
Kwa nini si jambo la hekima kufikiri kwamba unaweza kumbadili mtu unayemchumbia?
Paul na Priscilla Mwashamba walimpa Liz ushauri gani wenye hekima?
Kwa nini matatizo yalitokea katika ndoa ya Zak na Megan?
John na Liz walikuwa na miradi gani ya kiroho iliyopatana?
Kwa nini unapaswa kumfahamu “yule mtu wa siri wa moyoni” wa mtu kabla ya kuweka nadhiri za ndoa na mtu huyo? (1Pe 3:4)
Upendo wa kweli ni nini? (1Ko 13:4-8)