WIMBO NA. 133
Mwabudu Yehova Ujanani
Makala Iliyochapishwa
1. Yehova Mungu anatupenda,
Sisi ni wana na binti zake.
Tunapomtumikia Yeye,
Hutubariki na kututunza.
2. Tuwaheshimu wazazi wetu,
Tuwaeleze hisia zetu.
Tutapata kibali cha Mungu,
Tutakuwa rafiki za Mungu.
3. Basi Yehova tumkumbuke,
Sikuzote tuipende kweli.
Tukifanya yote tuwezayo,
Tutamfurahisha Yehova.
(Ona pia Zab. 71:17; Omb. 3:27; Efe. 6:1-3.)