WIMBO NA. 52
Wakfu wa Kikristo
Makala Iliyochapishwa
1. Ulimwengu uliumbwa
Na Yehova Mungu,
Dunia na anga pia,
Vyote aliumba.
Ndiye Chanzo cha uhai,
Kaonyesha wazi.
Anastahili sifa zote,
Na ibada ya wote.
2. Na Yesu alibatizwa
Atimize haki.
Alimwambia Yehova:
‘Naja kutumika.’
Alipotoka Yordani,
Mtiwa-mafuta,
Alisali kwa Baba yake:
‘Mapenzi yatimie.’
3. Twasimama mbele zako,
Kukusifu wewe.
Tunajikana wenyewe,
Tuwe mali yako.
Ulitoa Mwana wako,
Bei kubwa sana.
Hivyo maisha yetu yote,
Tumejitoa kwako.
(Ona pia Mt. 16:24; Marko 8:34; Luka 9:23.)