Wimbo 13
Wakfu wa Kikristo
1. Ni Yehova aliumba
Ulimwengu wote,
Dunia na anga pia,
Kazi zake zote.
Uhai ameutoa
Viumbe vijue
Ndiye wa kusifiwa sana,
Vimwabudu yeye tu.
2. Waisraeli wa kale,
Walisema hivi:
Tutazitii sheria
Zote za Yehova,
Alikuwa mume wao;
Akawanunua.
Taifa la wakifu kwake
Daima liwe hivyo.
3. Na Yesu alibatizwa
Atimize haki,
Akajitoa kwa Mungu
Afanye mapenzi.
Alipotoka Yordani
Mupakwa wa Mungu,
Amutumikie Yehova
Akiwa muwakifu.
4. Twakujia E Yehova,
Tusifu jinako.
Tujikane na kuweka
Maisha wakifu.
Ulitoa Mwana wako
Bei kubwa sana.
Tufe, tuishi sisi wako
Tumejitoa kwako.