SOMO LA 9
Kutumia Picha na Video Vizuri
Mwanzo 15:5
MUHTASARI: Tumia picha na video ili kufanya mambo unayofundisha yawe wazi na yaeleweke kwa urahisi.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Chagua vielelezo vitakavyoboresha ufundishaji wako. Unapotoa hotuba unaweza kutumia picha, michoro, ramani, mpangilio wa matukio, au vielelezo vingine vya aina hiyo ili kuonyesha mambo makuu wala si mambo madogo-madogo. Katika huduma unaweza pia kutumia video ili kutimiza kusudi hilo. Wasaidie wasikilizaji wako wakumbuke si tu vielelezo ulivyotumia bali jambo kuu lililofanya utumie vielelezo hivyo.
Hakikisha wasikilizaji wako wanaweza kuona vielelezo vyako. Kwa mfano, ikiwa utaonyesha picha jukwaani hakikisha ni kubwa vya kutosha ili wasikilizaji waweze kuiona.