Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
FEBRUARI 25–MACHI 3
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAROMA 9-11
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-1 1260 ¶2
Mwenye Wivu, Wivu
Bidii isiyoelekezwa kwa njia inayofaa. Mtu anaweza kuwa na bidii, au awe na wivu, wa kutimiza jambo fulani lakini wakati huohuo awe amekosea na awe anamkasirisha Mungu. Ilikuwa hivyo kwa Wayahudi wengi katika karne ya kwanza. Walifikiri kazi walizofanya chini ya Sheria ya Musa zingewafanya kuwa waadilifu. Lakini Paulo alionyesha kwamba bidii yao ilielekezwa kwa njia isiyofaa kwa sababu hawakuwa na ujuzi sahihi. Hivyo, hawakupata uadilifu wa kweli unaokuja kutoka kwa Mungu. Walipaswa kutambua kosa lao na kumgeukia Mungu kupitia Kristo ili wapate uadilifu na uhuru kutokana na hukumu ya Sheria ya Musa. (Ro 10:1-10) Sauli wa Tarso alikuwa mmoja kati yao. Alikuwa na bidii nyingi kupita kiasi katika dini ya Kiyahudi kufikia hatua ya “kulitesa sana kutaniko la Mungu na kuliangamiza.” Alikuwa akiishika Sheria kikamili akiamini alikuwa “mtu ambaye hakuwa na hatia.” (Gal 1:13, 14; Flp 3:6) Hata hivyo, wivu wake kwa ajili ya dini ya Kiyahudi ulikuwa umeelekezwa vibaya. Alikuwa na moyo mnyoofu, na hiyo ndiyo sababu Yehova alimwonyesha fadhili zisizostahiliwa kupitia Kristo na kumgeuza afuatie ibada ya kweli.—1Ti 1:12, 13.