Marejeo ya Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha
SEPTEMBA 2-8
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 7-8
“Kuhani Milele kwa Mfano wa Melkizedeki”
it-2 366
Melkizedeki
Mfalme wa Salemu la kale na “kuhani wa [Yehova] Mungu Aliye Juu Zaidi.” (Mwa 14:18, 22) Yeye ndiye kuhani wa kwanza anayetajwa na Maandiko; alipata cheo hicho muda fulani kabla ya mwaka wa 1933 K.W.K. Akiwa mfalme wa Salemu, jina linalomaanisha “Amani,” Melkizedeki anatambulishwa na mtume Paulo kuwa “Mfalme wa Amani” na, kwa msingi wa jina lake, kuwa “Mfalme wa Uadilifu.” (Ebr 7:1, 2) Salemu la kale linaeleweka kuwa msingi wa jiji ambalo baadaye lilikuja kuwa Yerusalemu, na jina lake lilitiwa ndani ya jina Yerusalemu, ambalo nyakati fulani pia linarejelewa kuwa “Salemu.”—Zb 76:2.
Baada ya Abramu (Abrahamu) kumshinda Kedorlaoma na wafalme waliokuwa pamoja naye, mzee huyo wa ukoo alienda kwenye Bonde la Shave au “Bonde la Mfalme.” Hapo Melkizedeki “akaleta mkate na divai” na kumbariki Abrahamu, akisema: “Abramu na abarikiwe na Mungu Aliye Juu Zaidi, Muumba wa mbingu na dunia; na asifiwe Mungu Aliye Juu Zaidi, ambaye amewatia mikononi mwako wale wanaokukandamiza!” Basi Abrahamu akampa mfalme huyo ambaye pia alikuwa kuhani “sehemu ya kumi ya vitu vyote,” yaani, kati ya “zile nyara bora” ambazo alipata aliposhinda muungano huo wa wafalme.—Mwa 14:17-20; Ebr 7:4.
it-1 uk. 1113
Kuhani Mkuu
Ukuhani Mkuu wa Yesu Kristo. Kitabu cha Biblia cha Waebrania kinaonyesha kwamba tangu wakati ambapo Yesu Kristo alifufuliwa na kuingia mbinguni, yeye ni “kuhani mkuu milele kama Melkizedeki.” (Ebr 6:20; 7:17, 21) Ili kuonyesha ukuu wa ukuhani wa Kristo na ubora wake juu ya ukuhani wa Haruni, mwandikaji anaonyesha kwamba Melkizedeki aliwekwa rasmi na Mungu Aliye Juu Zaidi kuwa mfalme na kuhani, si kupitia urithi. Kristo Yesu, ambaye hakuwa wa kabila la Lawi, bali alizaliwa katika kabila la Yuda na alikuwa mzao wa Daudi, hakurithi cheo chake kutoka kwa Haruni, bali aliwekwa rasmi na Mungu moja kwa moja, kama Melkizedeki. (Ebr 5:10) Mbali na ahadi iliyorekodiwa kwenye Zaburi 110:4: “Yehova ameapa naye hatabadili nia yake: ‘Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki!” Kristo pia ana mamlaka ya Kifalme kwa msingi wa kuwa mzao wa Daudi. Kuwekwa kwake rasmi kwa njia hiyo kunamfanya awe Mfalme na Kuhani mbinguni. Kuhusu kuwa mfalme, anakuwa mrithi wa ufalme ulioahidiwa katika agano la Daudi. (2Sa 7:11-16) Kwa hiyo, anakuwa na cheo cha kifalme na cha kikuhani wakati uleule, kama Melkizedeki.
Kwa njia nyingine, ubora wa ukuhani mkuu wa Kristo unaonekana wazi katika maana ya kwamba Lawi, ambaye alikuwa wa kwanza katika ukoo wa makuhani wa Kiyahudi, ni kana kwamba alimpa Melkizedeki sehemu ya kumi, kwa kuwa Lawi alikuwa bado katika viuno vya Abrahamu wakati ambapo mzee huyo wa ukoo alimpa sehemu ya kumi mfalme na kuhani wa Salemu. Isitoshe, ni katika maana hiyo kwamba pia Lawi alibarikiwa na Melkizedeki, na sheria ni kwamba mdogo hubarikiwa na mkubwa. (Ebr 7:4-10) Pia mtume Paulo anatokeza wazo la kwamba Melkizedeki “hana baba wala mama, hana ukoo, na hana mwanzo wa siku wala mwisho wa uzima” akiwa mwakilishi wa ukuhani wa milele wa Yesu Kristo, ambaye amefufuliwa na kupewa “uzima usioweza kuharibika.”—Ebr 7:3, 15-17.
it-2 367 ¶4
Melkizedeki
Ni katika njia gani inaweza kusemwa kwamba kwa kweli Melkizedeki hakuwa na “mwanzo wa siku wala mwisho wa uzima”?
Paulo anataja jambo la pekee kumhusu Melkizedeki, anaposema: “Hana baba wala mama, hana ukoo, na hana mwanzo wa siku wala mwisho wa uzima, bali akiwa amefanywa kama Mwana wa Mungu, anadumu akiwa kuhani daima.” (Ebr 7:3) Kama wanadamu wengine, Melkizedeki alizaliwa na akafa. Hata hivyo, majina ya baba na mama yake hayatajwi, ukoo wake na uzao wake hautajwi, na Maandiko hayatoi habari zozote kuhusu mwanzo wa siku zake au mwisho wa maisha yake. Hivyo, Melkizedeki ni mfano unaofaa wa Yesu Kristo, ambaye ukuhani wake hauna mwisho. Kama tu ambavyo hakukuwa na kuhani aliyemtangulia Melkizedeki wala hakukuwa na aliyechukua mahali pake, ndivyo pia Kristo hakutanguliwa na kuhani mkuu kama yeye, na Biblia inaonyesha hakutakuwa na yeyote atakayechukua mahali pake. Isitoshe, ingawa Yesu alizaliwa katika kabila la Yuda na katika ukoo wa kifalme wa Daudi, ukoo wake wa kimwili haukuhusiana kwa vyovyote na ukuhani wake, na hakupewa migawo ya kuwa kuhani na mfalme kwa sababu ya ukoo wa kibinadamu. Alipata migawo hiyo kutokana na kiapo ambacho Yehova alimtolea.
it-2 366
Melkizedeki
Mfano wa Ukuhani wa Kristo. Unabii mmoja wenye kutokeza kumhusu Masihi ni kiapo hiki cha Yehova kwa “Bwana” wa Daudi: “Wewe ni kuhani milele kwa mfano wa Melkizedeki!” (Zb 110:1, 4) Zaburi hiyo iliyoongozwa na roho iliwapa Waebrania sababu ya kumwona Masihi kuwa yule ambaye angepewa mgawo wa kuwa kuhani na mfalme. Mtume Paulo, katika barua aliyowaandikia Waebrania, aliondoa shaka kuhusu utambulisho wa yule aliyeahidiwa, alipozungumza kumhusu “Yesu, ambaye amekuwa kuhani mkuu milele kama Melkizedeki.”—Ebr 6:20; 5:10; tazama AGANO.
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-1 523 ¶5
Agano
Agano la Sheria lilifanywaje “lichakae”?
Hata hivyo, agano la Sheria ‘lilichakaa’ kwa njia fulani Mungu alipotangaza kupitia nabii Yeremia kwamba kungekuwa na agano jipya. (Yer 31:31-34; Ebr 8:13) Katika mwaka wa 33 W.K. agano la Sheria lilifutwa kwa msingi wa kifo cha Kristo kwenye mti wa mateso (Kol 2:14), na agano jipya likachukua mahali pake.—Ebr 7:12; 9:15; Mdo 2:1-4.
SEPTEMBA 9-15
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 9-10
“Kivuli cha Mambo Mema Yatakayokuja”
it-1 862 ¶1
Msamaha
Kulingana na sheria ambayo Mungu alilipatia taifa la Israeli, ili mtu asamehewe dhambi aliyotenda dhidi ya Mungu au dhidi ya mwanadamu mwenzake, kwanza alihitaji kurekebisha mambo kama Sheria ilivyoagiza kisha, katika visa vingi, alihitaji pia kutoa dhabihu ya damu ya mnyama kwa Yehova. (Law 5:5–6:7) Kwa sababu hiyo, Paulo alitaja kanuni hii: “Ndiyo, kulingana na Sheria karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na hakuna msamaha unaopatikana bila kumwaga damu.” (Ebr 9:22) Hata hivyo, kihalisi damu ya dhabihu za wanyama haingeweza kuondoa dhambi na kumpa mtu dhamiri safi kikamilifu. (Ebr 10:1-4; 9:9, 13, 14) Tofauti na hilo, agano jipya lililotabiriwa lilifanya mtu aweze kupata msamaha wa kweli, kwa msingi wa dhabihu ya fidia ya Yesu Kristo. (Yer 31:33, 34; Mt 26:28; 1Ko 11:25; Efe 1:7) Hata alipokuwa duniani, Yesu alionyesha kwamba alikuwa na mamlaka ya kusamehe dhambi alipomponya mwenye ukoma.—Mt 9:2-7.
it-2 602-603
Ukamilifu
Ukamilifu wa Sheria ya Musa. Sheria ambayo Waisraeli walipewa kupitia Musa ilitia ndani kuwepo kwa uandalizi wa makuhani na kutolewa kwa dhabihu mbalimbali za wanyama. Ingawa Sheria ilitoka kwa Mungu, na hivyo ilikuwa kamilifu, Sheria hiyo pamoja na uandalizi wake wa makuhani, na dhabihu zilizotolewa hazingeweza kuwaletea ukamilifu wale waliokuwa chini yake, kama mtume aliyeongozwa na roho anavyoonyesha. (Ebr 7:11, 19; 10:1) Badala ya kuleta uhuru kutokana na dhambi na kifo, ilifanya dhambi ionekane wazi zaidi. (Ro 3:20; 7:7-13) Hata hivyo, maandalizi hayo yote kutoka kwa Mungu yalitimiza kusudi lake; Sheria ilitenda kama “mtunzaji” ikiwaongoza watu kwa Kristo, na hivyo kuwa “kivuli [kikamilifu] cha mambo mema yatakayokuja.” (Gal 3:19-25; Ebr 10:1) Hivyo, Paulo alipozungumzia “kile ambacho Sheria ilishindwa kufanya kwa sababu ilikuwa dhaifu kupitia mwili” (Ro 8:3), inaonekana alikuwa akirejelea kwamba kuhani mkuu wa Wayahudi (ambaye aliwekwa rasmi na Sheria kusimamia mipango ya dhabihu na yeye ndiye aliyeingia kwenye Patakatifu Zaidi katika Siku ya Kufunika Dhambi akiwa na damu ya dhabihu) asingeweza “kuwaokoa kikamili” wale aliowatumikia, kama Waebrania 7:11, 18-28 inavyoeleza. Ingawa matoleo ya dhabihu kupitia ukuhani wa Haruni yaliwasaidia watu kudumisha msimamo mzuri mbele za Mungu, haikuwaondolea kikamili au kikamilifu ukweli wa kwamba walikuwa na dhambi. Mtume huyo alirejelea hilo aliposema kwamba kufunikwa kwa dhambi kupitia dhabihu hakungeweza “kuwafanya wale wanaokaribia wawe wakamilifu,” yaani, kuhusiana na dhamiri yao. (Ebr 10:1-4; linganisha Ebr 9:9.) Kuhani mkuu hangeweza kuandaa bei ya fidia iliyohitajiwa ili kupata ukombozi wa kweli kutokana na dhambi. Ukuhani wa Kristo wa kudumu na dhabihu yake inayofaa ndiyo tu itakayotimiza hilo.—Ebr 9:14; 10:12-22.
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-1 249-250
Ubatizo
Luka anataja kwamba Yesu alikuwa akisali wakati wa ubatizo wake. (Lu 3:21) Pia, mwandikaji wa barua kwa Waebrania anasema kwamba Yesu Kristo alipokuja “katika ulimwengu” (si wakati alipozaliwa na hangeweza kusoma au kusema maneno hayo, lakini alipojitoa kwa ajili ya ubatizo na kuanza huduma yake) alisema hivi akinukuu Zaburi 40:6-8 (LXX): “Hukutaka dhabihu na toleo, bali ulinitayarishia mwili. . . . Tazama! nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa kunihusu) kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.” (Ebr 10:5-9) Yesu alizaliwa akiwa mshiriki wa taifa la Wayahudi, taifa ambalo lilikuwa katika agano pamoja na Mungu, yaani, agano la Sheria. (Kut 19:5-8; Gal 4:4) Kwa sababu hiyo, Yesu tayari alikuwa katika uhusiano wa kiagano pamoja na Yehova Mungu alipoenda kwa Yohana ili abatizwe. Kwa kuchukua hatua hiyo, Yesu alikuwa akifanya mengi zaidi kuliko aliyohitaji kufanya chini ya Sheria. Alikuwa akijitoa kwa Baba yake Yehova ili kufanya “mapenzi” ya Baba yake kuhusiana na kutoa mwili wake “uliotayarishwa” na kuhusiana na kuondolewa kwa dhabihu zilizotolewa kulingana na Sheria. Mtume Paulo anasema hivi: “Kwa ‘mapenzi’ hayo sisi tumetakaswa kupitia toleo la mwili wa Yesu Kristo mara moja kwa wakati wote.” (Ebr 10:10) Mapenzi ya Baba kwa ajili ya Yesu pia yalihusisha utendaji wa Ufalme, na Yesu alijitoa pia kwa ajili ya huduma hiyo. (Lu 4:43; 17:20, 21) Yehova alikubali toleo hilo la Mwana wake, na kumtia mafuta kwa roho takatifu akisema: “Wewe ni Mwanangu, mpendwa; nimekukubali.”—Mk 1:9-11; Lu 3:21-23; Mt 3:13-17.
SEPTEMBA 16-22
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-1 804 ¶5
Imani
Mifano ya Zamani ya Imani. Kila mmoja katika ‘wingu kubwa la mashahidi’ wanaotajwa na Paulo (Ebr 12:1) alikuwa na msingi thabiti wa imani yake. Kwa mfano, Abeli alijua kuhusu ahadi ya Mungu ya “uzao” ambao ungeponda kichwa cha “nyoka.” Na aliona uthibitisho ulio wazi wa hukumu ambayo Yehova alitoa huko Edeni ikitimia juu ya wazazi wake. Wakiwa nje ya Edeni, Adamu na familia yake walikula mkate kwa jasho la nyuso zao kwa sababu ardhi ililaaniwa na kutoa miiba na michongoma. Inawezekana kwamba Abeli aliona jinsi Hawa alivyomtamani mume wake na jinsi Adamu alivyomtawala mke wake. Bila shaka, mama yake alitaja uchungu aliopata wakati wa kuzaa. Pia, mwingilio wa bustani ya Edeni ulilindwa na makerubi na upanga uliowaka moto. (Mwa 3:14-19, 24) Mambo hayo yote yalifanyiza “uthibitisho ulio wazi,” na kumpa Abeli uhakikisho kwamba ukombozi ungekuja kupitia ‘uzao ulioahidiwa.’ Hivyo, akiongozwa na imani “alimtolea Mungu dhabihu,” dhabihu ambayo ilithibitika kuwa yenye thamani kubwa zaidi kuliko ile ya Kaini.—Ebr 11:1, 4.
SEPTEMBA 23-29
HAZINA ZA NENO LA MUNGU | WAEBRANIA 12-13
Nidhamu—Uthibitisho wa Upendo wa Yehova
it-1 uku. 629
Nidhamu
Mateso ambayo Yehova anaweza kuruhusu yawapate watumishi wake yanaweza kuonwa kuwa nidhamu, au mazoezi, yanayotokeza matunda yanayofaa ya uadilifu, ambayo yatafurahiwa baada ya jaribu kwisha chini ya hali zenye amani. (Ebr 12:4-11) Hata Mwana wa Mungu alizoezwa kuwa kuhani mkuu mwenye huruma na mwenye uwezo wa kutusikitikia kupitia mateso ambayo Baba yake alimruhusu kukabili.—Ebr 4:15.
Kutafuta Hazina za Kiroho
Toeni Dhabihu Ambazo Zampendeza Yehova
10 Basi Waebrania walihitaji kuepuka ‘kuchukuliwa na mafundisho ya namna nyingine nyingine, na ya kigeni’ ya watetezi wa mawazo ya dini ya Kiyahudi. (Wagalatia 5:1-6) Ili ubaki ukiwa thabiti katika ukweli, ‘moyo waweza kufanywa imara kwa neema ya Mungu’ wala si kupitia mafundisho hayo. Yaonekana watu fulani walitoa ubishi kuhusu vyakula na dhabihu, kwa kuwa Paulo alisema kwamba moyo haukufanywa imara ‘kwa vyakula, ambavyo wao waliokwenda navyo hawakupata faida.’ Manufaa za kiroho zatokana na ujitoaji kimungu na kuthamini ukombozi, si kutokana na kuhangaikia isivyofaa kula vyakula fulani na kushika siku fulani hususa. (Warumi 14:5-9) Tena, dhabihu za Kristo ilifanya dhabihu za Walawi ziwe zisizofaa.—Waebrania 9:9-14; 10:5-10.
SEPTEMBA 30–OKTOBA 6
Kutafuta Hazina za Kiroho
it-2 253-254
Nuru
Yehova ni “Baba wa mianga ya mbinguni.” (Yak 1:17) Yeye si tu Yule “ambaye hutoa jua ili liangaze wakati wa mchana, sheria za mwezi na nyota ili ziangaze usiku” (Yer 31:35) bali pia yeye ndiye Chanzo cha nuru ya kiroho. (2Ko 4:6) Sheria yake, maamuzi yake ya kihukumu, na neno lake ni nuru kwa wale wanaojiruhusu kuongozwa nayo. (Zb 43:3; 119:105; Met 6:23; Isa 51:4) Mtunga-zaburi alitangaza hivi: “Kwa nuru yako tunaweza kuona nuru.” (Zb 36:9; linganisha Zb 27:1; 43:3.) Kama nuru ya jua inavyozidi kuongezeka kuanzia mapambazuko mpaka “mchana kamili,” ndivyo barabara ya waadilifu inavyoangaziwa na nuru kutoka kwa Mungu, inavyozidi kung’aa zaidi na zaidi. (Met 4:18) Mtu anapofuata njia ambayo Yehova ametoa anatembea katika nuru yake. (Isa 2:3-5) Kwa upande mwingine, mtu anayeangalia vitu kwa njia iliyopotoka au ya uovu, anakuwa katika giza kubwa la kiroho. Kama Yesu alivyosema: “Ikiwa jicho lako lina wivu, mwili wako wote utakuwa na giza. Ikiwa nuru iliyo ndani yako kwa kweli ni giza, basi giza hilo ni kubwa sana!”—Mt 6:23; linganisha Kum 15:9; 28:54-57; Met 28:22; 2Pe 2:14.
it-2 222 ¶4
Sheria
“Sheria ya Kifalme.” Inafaa kwamba “sheria ya kifalme” ingekuwa na umuhimu na umaarufu mkubwa zaidi kuliko sheria nyingine zinazowaongoza wanadamu kama tu ambavyo mfalme ana umuhimu na umaarufu mkubwa kuliko raia wake. (Yak 2:8) Msingi wa agano la Sheria ulikuwa upendo; na sheria ya pili kati ya sheria ambazo Sheria yote na Manabii hutegemea inasema “lazima umpende jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe” (sheria ya kifalme). (Mt 22:37-40) Hata hivyo, Wakristo ambao hawako chini ya agano la Sheria, wako chini ya sheria ya Mfalme Yehova na Mwana wake, Mfalme Yesu Kristo, kuhusiana na agano jipya.