SOMO LA 11
Shauku
Waroma 12:11
MUHTASARI: Wachangamshe na kuwachochea wasikilizaji kwa kuzungumza kwa shauku.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
- Habari unayozungumzia inapaswa kugusa moyo wako. Unapojitayarisha kutoa mgawo wako, fikiria kwa kina kuhusu umuhimu wa ujumbe wako. Elewa vizuri jambo unalotayarisha ili uweze kuwasilisha habari hiyo kutoka moyoni. 
- Wafikirie wasikilizaji wako. Tafakari jinsi ujumbe utakaosoma au kufundisha utakavyowanufaisha wengine. Fikiria jinsi utakavyowasilisha habari hiyo kwa njia ambayo itawafanya wasikilizaji wako waithamini zaidi. 
- Toa hotuba yako kwa uchangamfu. Zungumza kwa hisia. Tumia ishara za mikono, kichwa, na uso kuonyesha hisia zako.