SOMO LA 11
Shauku
Waroma 12:11
MUHTASARI: Wachangamshe na kuwachochea wasikilizaji kwa kuzungumza kwa shauku.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Habari unayozungumzia inapaswa kugusa moyo wako. Unapojitayarisha kutoa mgawo wako, fikiria kwa kina kuhusu umuhimu wa ujumbe wako. Elewa vizuri jambo unalotayarisha ili uweze kuwasilisha habari hiyo kutoka moyoni.
Wafikirie wasikilizaji wako. Tafakari jinsi ujumbe utakaosoma au kufundisha utakavyowanufaisha wengine. Fikiria jinsi utakavyowasilisha habari hiyo kwa njia ambayo itawafanya wasikilizaji wako waithamini zaidi.
Toa hotuba yako kwa uchangamfu. Zungumza kwa hisia. Tumia ishara za mikono, kichwa, na uso kuonyesha hisia zako.