Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w15 6/1 kur. 3-5
  • Jinsi Sayansi Inavyoathiri Maisha Yako

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Jinsi Sayansi Inavyoathiri Maisha Yako
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • YALE AMBAYO SAYANSI IMESHINDWA KUTIMIZA
  • Chanzo cha Ulimwengu na Uhai Ni Nini?
    Amkeni!—2002
  • Waweza Kuitumaini Sayansi Kadiri Gani?
    Amkeni!—1998
  • Kupatanisha Sayansi na Dini
    Amkeni!—2002
  • Mashahidi wa Yehova Wana Maoni Gani Kuhusu Sayansi?
    Maswali Yanayoulizwa Mara Nyingi Kuhusu Mashahidi wa Yehova
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
w15 6/1 kur. 3-5
Maendeleo ya sayansi yanatia ndani magari, GPS, setilaiti, ndege, na kuchunguza ubongo

HABARI KUU JE, SAYANSI | IMECHUKUA NAFASI YA BIBLIA?

Jinsi Sayansi Inavyoathiri Maisha Yako

Kulingana na kamusi ya Kiswahili sanifu, sayansi ni “elimu inayotokana na uchunguzi, majaribio, vipimo na kuthibitishwa kwa muda uliopo.” Ni vigumu kufanya mambo yote hayo na mara nyingi kazi hiyo huchosha. Wanasayansi hujitahidi kufanya majaribio kwa majuma, miezi, au hata miaka kadhaa. Nyakati fulani kazi zao hazifanikiwi, lakini katika visa vingi wanasayansi wamenufaisha wanadamu. Fikiria mifano kadhaa.

Kampuni fulani ya Ulaya ilitumia plastiki ngumu na vifaa bora vya kuchujia maji kutokeza kifaa ambacho kinawasaidia watu kuepuka magonjwa yanayotokana na kunywa maji yasiyo safi. Vifaa kama hivyo hutumika wakati wa misiba ya asili, kama wakati wa tetemeko la ardhi lililoikumba nchi ya Haiti mwaka wa 2010.

Huko angani, setilaiti kadhaa hufanyiza kile kinachoitwa Global Positioning System (GPS). Kifaa hicho kilichobuniwa kwa ajili ya matumizi ya kijeshi, kinawasaidia pia madereva, marubani, waongozaji wa meli, wawindaji na watembeaji wa masafa marefu kujua njia. Kwa sababu ya uvumbuzi huo wa wanasayansi, GPS imerahisisha kujua mahali unapotaka kwenda.

Je, unatumia simu, kompyuta au Intaneti? Je, afya yako imeboreshwa au umepona baada ya kutumia dawa? Je, wewe husafiri kwa ndege? Ikiwa ndivyo, basi unafaidika kutokana na yale ambayo sayansi imewafanyia wanadamu. Sayansi imeathiri maisha yako katika njia nyingi nzuri.

YALE AMBAYO SAYANSI IMESHINDWA KUTIMIZA

Katika jitihada za kuongeza ujuzi wao, wanasayansi wa kisasa wamechunguza kwa kina kuhusu asili ya ulimwengu. Wanafizikia wa nyuklia wamechunguza utendaji wa atomu, wakati huohuo wamejaribu kuelewa mwanzo wa ulimwengu kwa kuchunguza jinsi ulivyokuwa mabilioni ya miaka iliyopita. Kadiri wanavyochunguza kwa mapana na marefu, hata katika ulimwengu usioonekana na usiofikika, baadhi ya wanasayansi wanahisi kwamba ikiwa Mungu anayetajwa katika Biblia yupo, basi wangeweza kumwona.

Baadhi ya wanasayansi na wanafalsafa mashuhuri wana maoni zaidi. Wanaendeleza kile ambacho mwandishi wa sayansi Amir D. Aczel alikiita kuwa “mjadala wa wanasayansi unaopinga kuwapo kwa Mungu.” Kwa mfano, mwanafizikia mashuhuri sana alidai kwamba “kukosekana kwa ushahidi wa kuwapo kwa Mungu anayetimiza fungu muhimu katika uumbaji wa ulimwengu ni uthibitisho usiopingika kwamba hakuna mungu.” Wengine husema kwamba utendaji wa Mungu unaotajwa katika Biblia ni “uchawi” na “nguvu fulani za ajabu.”a

Hata hivyo, swali tunalopaswa kujiuliza ni kwamba: Je, wanasayansi wamejifunza vya kutosha kuhusu uumbaji hivi kwamba waweze kufikia mkataa? Jibu rahisi ni, hapana. Sayansi imefanya maendeleo makubwa, lakini wanasayansi wengi wanajua kwamba kuna vitu vingi sana visivyojulikana na vile ambavyo ni tata. Kuhusu kuelewa uumbaji, mwanafizikia na mshindi wa tuzo ya Nobeli Steven Weinberg alisema hivi: “Hatutawahi kamwe kuelewa kabisa uumbaji.” Mtaalamu wa nyota mashuhuri zaidi nchini Uingereza, Profesa Martin Rees, aliandika hivi: “Kuna vitu ambavyo huenda wanadamu hawatavielewa kamwe.” Ukweli ni kwamba wanasayansi bado hawajajua vizuri uumbaji kuanzia seli ndogo zaidi hadi ulimwengu mzima. Ona mifano ifuatayo:

  • DNA

    Wanabiolojia hawajui kikamili hatua zinazotokea ndani ya seli zilizo hai. Baadhi ya maswali ambayo bado sayansi haiwezi kujibu kikamili ni kama vile jinsi seli zinavyopata nguvu, zinavyotokeza protini na zinavyojigawa.

  • Mvulana akitupa mpira

    Nguvu ya uvutano hutuathiri kila sekunde. Hata hivyo, wanafizikia hawajajua kikamili jinsi jambo hilo linavyotendeka. Hawaelewi vizuri kwa nini uvutano huo hutuvuta chini ardhini tunaporuka au jinsi uvutano huo unavyodumisha mwezi kwenye njia yake ili kuzunguka dunia.

  • Ulimwengu

    Wanakosmolojia wanakadiria kwamba asilimia 95 hivi ya vitu vinavyofanyiza ulimwengu havionekani na haviwezi kugunduliwa na vifaa vya kisayansi. Wamegawanya vitu hivyo katika makundi mawili, mata nyeusi na nguvu nyeusi. Asili ya vitu hivyo bado haijulikani.

Kuna vitu vingine ambavyo havijulikani vinavyowatatiza wanasayansi. Kwa nini jambo hilo ni muhimu? Mwandishi mashuhuri wa sayansi alisema hivi: “Mambo tusiyoyajua ni mengi sana ukilinganisha na yale tunayoyajua. Sayansi inaweza kukufanya ustaajabu na kukufanya utamani kujifunza zaidi, badala ya kukufanya ujione kuwa hujui mambo mengi.”

Kwa hiyo, kama unajiuliza ikiwa sayansi inaanza kuchukua nafasi ya Biblia na kwamba inapinga kuwapo kwa Mungu, fikiria jambo hili: Ikiwa wanasayansi mashuhuri pamoja na vifaa vyao vyenye nguvu wameweza kuwa na ujuzi mdogo tu kuhusu uumbaji, je, litakuwa jambo linalopatana na akili kuacha kuamini au kutafuta ukweli wa mambo ambayo sayansi imeshindwa kuchunguza? Kuhusu jambo hilo, katika makala ndefu inayoeleza historia na maendeleo ya elimu ya nyota, kitabu Encyclopedia Britannica kinafikia mkataa huu: “Baada ya miaka 4,000 hivi ya utaalamu wa nyota, ulimwengu bado ni tata kama tu vile ambavyo huenda Wababiloni waliuona.”

Mashahidi wa Yehova wanaheshimu haki ya kila mtu ya kufanya uamuzi kuhusu jambo hilo. Tunajitahidi kufuata mwongozo wa Biblia: “Usawaziko wenu na ujulikane kwa watu wote.” (Wafilipi 4:5) Ni kwa msingi huo tunakualika uchunguze jinsi ambavyo sayansi na Biblia zinapatana na kukamilishana.

a Baadhi ya watu huipinga Biblia kwa sababu ya mafundisho ya zamani na ya sasa ya dini kama vile kuamini kwamba dunia ni kitovu cha ulimwengu wote au kwamba Mungu aliumba dunia katika siku sita zenye urefu wa saa 24.—Tazama sanduku lenye kichwa “Biblia na Mambo Yaliyothibishwa Kisayansi.”

Biblia na Mambo Yaliyothibitishwa Kisayansi

Biblia haidai kuwa ni kitabu cha kisayansi. Hata hivyo, waandishi wake walieleza mambo yanayopaswa kuwavutia wanasayansi leo kutokana na usahihi wake. Ona mifano ifuatayo.

  • Ulimwengu

    Umri wa dunia na ulimwengu

    Wanasayansi wanakadiria kwamba dunia ina umri wa miaka bilioni 4 hivi na kwamba ulimwengu una umri wa miaka bilioni 13 hadi 14 hivi. Biblia haitaji tarehe ya kuumbwa kwa ulimwengu. Pia, haisemi kwamba dunia ina umri wa miaka elfu kadhaa tu. Mstari wa kwanza katika Biblia unasema hivi: “Hapo mwanzo Mungu aliumba mbingu na dunia.” (Mwanzo 1:1) Maneno hayo yanawawezesha wanasayansi kukadiria umri wa ulimwengu kwa kutumia kanuni za kisayansi zinazotegemeka.

  • Milima, uoto, na maji

    Kutayarishwa kwa dunia ili kuwa makao ya mwanadamu

    Mwanzo sura ya 1 hutumia usemi “siku” inapotaja hatua zilizohusika kuandaa dunia kwa ajili ya viumbe hai wa aina mbalimbali. Jambo la pekee linalotajwa katika mistari hiyo ni kuumbwa kwa wanadamu. Biblia haitaji urefu wa “siku” sita za uumbaji. Badala yake, inafungua njia kwa wanasayansi kufanya uchunguzi na kujua urefu wa kipindi hicho. Tunajua kwamba “siku” za uumbaji zilikuwa na urefu wa zaidi ya saa 24.

  • Dunia

    Jinsi dunia inavyoelea

    Biblia inaeleza kwamba dunia imetundikwa “pasipo na kitu.” (Ayubu 26:7) Biblia haisemi kwamba dunia yetu iko juu ya migongo ya tembo wakubwa walio juu ya kobe mkubwa, kama masimulizi fulani ya kale yalivyodai. Badala yake, Biblia inawaruhusu wanasayansi kufanya uchunguzi wao. Baada ya muda, Nicolaus Copernicus na Johannes Kepler walieleza jinsi sayari zinavyolizunguka jua kwa kuongozwa na nguvu isiyoonekana. Baadaye, Isaac Newton alieleza jinsi ambavyo nguvu za uvutano zinavyoongoza vitu vingine vyote angani.

  • Bakteria wenye umbo la kijiti

    Maagizo ya jinsi ya kudhibiti magonjwa na kudumisha usafi

    Kitabu cha Mambo ya Walawi kina maagizo waliyopewa Waisraeli kuhusu jinsi ya kuepuka maambukizi ya magonjwa ya mlipuko, kutia ndani utaratibu wa kuwatenga wagonjwa. Kuhusu usafi, sheria iliyo katika Kumbukumbu la Torati 23:12, 13 iliwaagiza Waisraeli kufukia kinyesi chao nje ya kambi. Walihitaji ‘kufunika mavi yao’ ardhini. Ni miaka 200 hivi imepita tangu wanasayansi na madaktari walipoona umuhimu wa kuweka viwango hivyo.

Habari za Biblia ulizosoma ziliandikwa karne nyingi zilizopita. Kwa nini waandishi wa Biblia walijua mambo kwa usahihi ingawa watu wenye elimu wa wakati wao hawakujua? Mtungaji wa Biblia anajibu hivi: “Kama vile mbingu zilivyo juu kuliko dunia, ndivyo njia zangu zilivyo juu kuliko njia zenu, na mawazo yangu kuliko mawazo yenu.”—Isaya 55:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki