HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 38-39
Yehova Hakumwacha Yosefu Kamwe
Yosefu alipokuwa akikabili majaribu mengi, Yehova “alikuwa akifanikisha kila jambo alilokuwa akifanya” na “kumfanya apate kibali machoni pa ofisa mkuu wa gereza.” (Mwa 39:2, 3, 21-23) Tunaweza kujifunza masomo gani kutokana na simulizi hilo?
Majaribu tunayokabili hayamaanishi kwamba tumepoteza kibali cha Yehova.—Zb 34:19
Tunapaswa kuwa macho kuona baraka za Yehova na kumshukuru.—Flp 4:6, 7
Tunapaswa kumtegemea Yehova atutegemeze.—Zb 55:22