HAZINA ZA NENO LA MUNGU | MWANZO 48-50
Wenye Umri Mkubwa Wanaweza Kutufundisha Mengi
Wenye umri mkubwa huimarisha imani yetu katika Yehova na ahadi zake wanapotusimulia kuhusu ‘kazi za Yehova zinazostaajabisha’ ambazo wamejionea katika siku hizi za mwisho. (Zb 71:17, 18) Ikiwa kutaniko lenu limebarikiwa kuwa na ndugu na dada wenye umri mkubwa, waulize
Yehova aliwasaidiaje walipokabili changamoto huku wakimtumikia?
wameona ongezeko gani katika idadi ya wahubiri wa Ufalme?
wamepata shangwe kadiri gani walipopata uelewaji mpya wa kweli za Biblia?
wamejionea mabadiliko gani katika tengenezo la Yehova?