MAISHA YA MKRISTO
Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka kwa Wakristo Wenye Uzoefu?
Katika makutaniko yetu kuna ndugu na dada ambao wamemtumikia Yehova kwa makumi ya miaka. Tunaweza kujifunza kutokana na jinsi walivyomtegemea Yehova. Tunaweza kuwauliza kuhusu historia ya tengenezo la Yehova na changamoto walizopata na jinsi Yehova alivyowasaidia. Huenda hata wakati wa jioni ya Ibada ya Familia tunaweza kumwomba mmoja kati yao atueleze mambo aliyoona.
Ikiwa umemtumikia Yehova kwa miaka mingi, waeleze kwa uhuru Wakristo ambao hawana uzoefu kama wako kuhusu imani yako. Yakobo na Yosefu waliwaeleza watoto wao kuhusu mambo waliyojionea. (Mwa 48:21, 22; 50:24, 25) Baadaye, Yehova aliwaagiza vichwa vya familia wawafundishe watoto wao kuhusu matendo yake yenye kustaajabisha. (Kum 4:9, 10; Zb 78:4-7) Katika siku zetu, wazazi na wengine kutanikoni wanaweza kuwasimulia vijana mambo yenye kustaajabisha ambayo wameona Yehova akitimiza kupitia tengenezo lake.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUDUMISHA UMOJA WAKATI WA MARUFUKU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Ofisi ya tawi ya Austria iliwasaidiaje ndugu katika nchi fulani zilizokuwa zimepigwa marufuku?
Akina ndugu katika nchi hizo walifauluje kudumisha imani yao ikiwa yenye nguvu?
Kwa nini wahubiri wengi nchini Rumania walijitenga na tengenezo la Yehova, na walirudije?
Mambo hayo yaliyoonwa yameimarishaje imani yako?
Jifunze mambo mengi ya kiroho kutoka kwa akina ndugu na dada ambayo yatakusaidia kuimarisha imani yako!