Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • mwb20 Juni uku. 5
  • Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka kwa Wakristo Wenye Uzoefu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka kwa Wakristo Wenye Uzoefu?
  • Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
  • Habari Zinazolingana
  • Wasaidie Watoto Waelewe Tengenezo la Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2010
  • Mna Sababu ya Kushangilia
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Kaa Salama Ukiwa Sehemu ya Tengenezo la Mungu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1998
  • Kujifunza Kutoka kwa Wahubiri Wenye Uzoefu Zaidi
    Huduma Yetu ya Ufalme—2015
Pata Habari Zaidi
Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2020
mwb20 Juni uku. 5
Dada kijana akimshika mkono dada mwenye umri mkubwa.

MAISHA YA MKRISTO

Tunaweza Kujifunza Nini Kutoka kwa Wakristo Wenye Uzoefu?

Katika makutaniko yetu kuna ndugu na dada ambao wamemtumikia Yehova kwa makumi ya miaka. Tunaweza kujifunza kutokana na jinsi walivyomtegemea Yehova. Tunaweza kuwauliza kuhusu historia ya tengenezo la Yehova na changamoto walizopata na jinsi Yehova alivyowasaidia. Huenda hata wakati wa jioni ya Ibada ya Familia tunaweza kumwomba mmoja kati yao atueleze mambo aliyoona.

Ikiwa umemtumikia Yehova kwa miaka mingi, waeleze kwa uhuru Wakristo ambao hawana uzoefu kama wako kuhusu imani yako. Yakobo na Yosefu waliwaeleza watoto wao kuhusu mambo waliyojionea. (Mwa 48:21, 22; 50:24, 25) Baadaye, Yehova aliwaagiza vichwa vya familia wawafundishe watoto wao kuhusu matendo yake yenye kustaajabisha. (Kum 4:9, 10; Zb 78:4-7) Katika siku zetu, wazazi na wengine kutanikoni wanaweza kuwasimulia vijana mambo yenye kustaajabisha ambayo wameona Yehova akitimiza kupitia tengenezo lake.

TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA KUDUMISHA UMOJA WAKATI WA MARUFUKU, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:

  • Ofisi ya tawi ya Austria iliwasaidiaje ndugu katika nchi fulani zilizokuwa zimepigwa marufuku?

  • Akina ndugu katika nchi hizo walifauluje kudumisha imani yao ikiwa yenye nguvu?

  • Kwa nini wahubiri wengi nchini Rumania walijitenga na tengenezo la Yehova, na walirudije?

  • Mambo hayo yaliyoonwa yameimarishaje imani yako?

Picha: Sehemu mbalimbali za video ‘Kudumisha Umoja Wakati wa Marufuku.’ 1. Ramani ikionyesha nchi za Ulaya Mashariki zilizokuwa zimepigwa marufuku. 2. Mashine ya kunakili vitabu. 3. Ndugu nchini Rumania wakikumbatiana.

Jifunze mambo mengi ya kiroho kutoka kwa akina ndugu na dada ambayo yatakusaidia kuimarisha imani yako!

Vipi ikiwa wahubiri wengi katika kutaniko lenu walibatizwa katika miaka ya karibuni? Mnaweza kupata mambo yaliyoonwa ya Mashahidi wa muda mrefu kwenye jw.org sehemu ya Maktaba chini ya “Video” au kwenye Fahirisi (Watch Tower Publications Index) chini ya “Masimulizi ya Maisha ya Mashahidi wa Yehova.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki