MAISHA YA MKRISTO
Unaweza Kuhubiri na Kufundisha!
Mwanzoni Musa alikuwa na shaka kuhusu uwezo wake wa kutimiza mgawo ambao Yehova alikuwa amempa. (Kut 4:10, 13) Je, umewahi kuhisi hivyo? Je, unajifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova? Je, wewe hujiuliza ikiwa siku moja utaweza kuhubiri nyumba kwa nyumba? Au labda wewe ni kijana ambaye anasitasita kuhubiri shuleni. Au labda unaogopa kuhubiri kupitia simu au kushiriki katika utumishi fulani wa hadharani. Mwombe Yehova akupe roho yake takatifu. (1Pe 4:11) Uwe na uhakika kwamba anaweza kukusaidia utimize mgawo wowote anaokupa.—Kut 4:11, 12.
TAZAMENI VIDEO YENYE KICHWA UWE JASIRI UKIWA . . . MHUBIRI, KISHA MJIBU MASWALI YAFUATAYO:
Dada Aoyama alikabili changamoto gani?
Alipata wapi nguvu na ujasiri?—Yer 20:7-9
Alifaidikaje kwa kufanya mengi zaidi katika utumishi wa Yehova?
Yehova anaweza kukusaidia kushinda changamoto gani katika huduma?