SOMO LA 20
Umalizio Wenye Matokeo
Mhubiri 12:13, 14
MUHTASARI: Katika maneno yako ya kumalizia, wachochee wasikilizaji wakubali na kutumia mambo waliyojifunza.
JINSI YA KUFANYA HIVYO:
Husianisha umalizio na habari yote kwa ujumla. Taja tena au utumie maneno mengine kurudia mambo makuu na mada kuu ya habari yako.
Wachochee wasikilizaji. Waonyeshe wasikilizaji wanachohitaji kufanya, na uwape sababu za msingi za kufanya hivyo. Zungumza kwa njia inayoonyesha unasadiki jambo unalosema na kwamba ni muhimu.
Umalizio uwe rahisi na mfupi. Usianze kutaja mambo makuu mapya. Ukitumia maneno machache iwezekanavyo, wachochee kwa mara ya mwisho wachukue hatua.