Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-34 kur. 1-4
  • Je, Kuteseka Kutaisha?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Je, Kuteseka Kutaisha?
  • Je, Kuteseka Kutaisha?
  • Habari Zinazolingana
  • Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
    Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
  • Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
    Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
    Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
Pata Habari Zaidi
Je, Kuteseka Kutaisha?
T-34 kur. 1-4

Je, Kuteseka Kutaisha?

Je, ungesema . . .

  • ndio?

  • la?

  • labda?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Mungu . . . atayafuta machozi yao yote, maana hakutakuwako tena na kifo, wala uchungu, wala kilio, wala maumivu.”​—Ufunuo 21:3, 4, Habari Njema kwa Watu Wote.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

Uhakikisho wa kwamba Mungu hasababishi matatizo yetu.​—Yakobo 1:13.

Faraja kutokana na kujua kwamba Mungu anaelewa kabisa tunavyohisi tunapoteseka.​—Zekaria 2:8.

Tumaini la kwamba kuteseka kote kutaisha.​—Zaburi 37:9-11.

Mwanamume anayesoma Biblia akipiga picha akilini mwisho wa mateso na ukosefu wa haki
Mwanamume anayesoma Biblia akipiga picha akilini mwisho wa mateso na ukosefu wa haki

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa angalau sababu mbili:

  • Mungu huchukia mateso na ukosefu wa haki. Hebu wazia jinsi Yehova Mungu alivyohisi watu wake katika nyakati za Biblia walipoteswa kikatili. Biblia inasema kwamba alifadhaika kwa sababu ya “wale waliowatesa.”​—Waamuzi 2:18, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

    Mungu hafurahishwi hata kidogo na wale wanaowaumiza wengine. Kwa mfano, Biblia inasema kwamba anachukia “mikono inayomwaga damu isiyo na hatia.” —Methali 6:16, 17.

  • Mungu anatujali tukiwa mtu mmoja mmoja. Kila mmoja wetu anajua “mateso yake mwenyewe na maumivu yake mwenyewe” lakini hata Yehova anayajua maumivu hayo!—2 Mambo ya Nyakati 6:29, 30.

    Kupitia Ufalme wake, hivi karibuni Yehova ataondoa mateso yanayomkabili kila mtu. (Mathayo 6:9, 10) Kwa sasa, anawafariji kwa wororo wale wanaomtafuta kwa moyo wote.—Matendo 17:27; 2 Wakorintho 1:3, 4.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Wanawake wawili wakijifunza Biblia
Wanawake wawili wakijifunza Biblia

Kwa nini Mungu anaruhusu watu wateseke?

Biblia inajibu swali hilo kwenye WAROMA 5:12 na 2 PETRO 3:9.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki