Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • T-33 kur. 1-4
  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
  • Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
  • Habari Zinazolingana
  • Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
    Una Maoni Gani Kuhusu Wakati Ujao?
  • Ufalme wa Mungu Ni Nini?
    Ufalme wa Mungu Ni Nini?
  • Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
    Je, Kweli Wafu Wataishi Tena?
  • Je, Kuteseka Kutaisha?
    Je, Kuteseka Kutaisha?
Pata Habari Zaidi
Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?
T-33 kur. 1-4

Ni Nani Hasa Anayeuongoza Ulimwengu?

Je, unafikiri ni . . .

  • Mungu?

  • wanadamu?

  • mtu mwingine?

BIBLIA HUSEMA HIVI

“Ulimwengu wote unatawaliwa na yule Mwovu.”—1 Yohana 5:19.

“Mwana wa Mungu alikuja . . . kuiharibu kazi ya Ibilisi.”—1 Yohana 3:8, Biblia Habari Njema.

FAIDA ZA KUAMINI JAMBO HILO

Maelezo yenye kueleweka kuhusu hali za ulimwengu.​—Ufunuo 12:12.

Sababu ya kuamini kwamba ulimwengu wetu utakuwa mzuri zaidi.​—1 Yohana 2:17.

Shetani akiongoza siasa, majeshi, dini, na watu wa ulimwengu huu
Shetani akiongoza siasa, majeshi, dini, na watu wa ulimwengu huu

JE, KWELI TUNAWEZA KUAMINI KILE AMBACHO BIBLIA HUSEMA?

Ndiyo, kwa angalau sababu tatu:

  • Utawala wa Shetani utakomeshwa. Yehova ameazimia kuukomesha utawala wa Shetani. Anaahidi ‘kumwangamiza . . . Ibilisi’ na kuondoa kabisa madhara yote ambayo Shetani amesababisha.—Waebrania 2:14, Tafsiri ya Ulimwengu Mpya.

  • Mungu amemchagua Yesu Kristo atawale ulimwengu. Yesu ni tofauti kabisa na mtawala wa sasa wa ulimwengu huu ambaye ni mkatili, na mwenye ubinafsi. Kuhusu utawala wa Yesu, Mungu anaahidi: “Atamhurumia mtu wa hali ya chini na maskini . . . Atawaokoa kutoka katika ukandamizaji na ukatili.”—Zaburi 72:13, 14.

  • Mungu hawezi kusema uwongo. Biblia inasema hivi waziwazi: “Mungu hawezi kamwe kusema uwongo.” (Waebrania 6:18) Yehova anapoahidi kufanya jambo fulani, ni kana kwamba jambo hilo tayari limetimizwa! (Isaya 55:10, 11) “Mtawala wa ulimwengu huu atatupwa nje.”—Yohana 12:31.

JAMBO LA KUFIKIRIA

Familia yenye furaha ikifurahia wakati pamoja
Familia yenye furaha ikifurahia wakati pamoja

Ulimwengu utakuwaje baada ya mtawala wake kuondolewa?

Biblia inajibu swali hilo kwenye ZABURI 37:10, 11 na UFUNUO 21:3, 4.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki