WIMBO NA. 130
Uwe Mwenye Kusamehe
Makala Iliyochapishwa
1. Kwa upendo Mungu,
Kapanga Mwana afe.
Dhambi ziweze kufutwa,
Kifo kiondolewe.
Tukitubu kweli kweli,
Tunaweza kumwomba,
Kwa msingi wa fidia,
Aliyotoa Kristo.
2. Twapata rehema,
Tukimwiga Yehova.
Tukisamehe wengine,
Kwa upendo, huruma.
Tukiepuka kinyongo,
Tukivumiliana;
Tukiwaheshimu ndugu,
Tukiwa na upendo.
3. Sote tunapaswa,
Kuonyesha rehema.
Itaondoa kinyongo,
Na uchungu wa chuki.
Tukitenda kama Mungu,
Apendaye zaidi,
Tutasamehe kikweli;
Na kumwiga Yehova.
(Ona pia Mt. 6:12; Efe. 4:32; Kol. 3:13.)