Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • yb07 kur. 3-5
  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza
  • 2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
  • Habari Zinazolingana
  • “Lazima Umpende Yehova Mungu Wako”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Mtukuze Yehova—Mungu wa Pekee wa Kweli
    Mwabudu Mungu wa Pekee wa Kweli
  • Usiruhusu Upendo Wako Upoe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2017
  • Mpende Mungu Anayekupenda
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2006
Pata Habari Zaidi
2007 Kitabu cha Mwaka cha Mashahidi wa Yehova
yb07 kur. 3-5

Barua Kutoka kwa Baraza Linaloongoza

KAMA Yesu, sisi Mashahidi wa Yehova tunasali kwa moyo wote: ‘Jina lako litakaswe.’ Tunaonyesha kwa mwenendo wetu kwamba tunataka sana kuishi kupatana na sala hiyo. Hata hivyo, haitoshi tu kujua jina la Mungu. Tunapaswa kutumia nafasi zote tunazopata kulitukuza. Kuitwa Mashahidi wa Yehova ni pendeleo lisilo na kifani.—Mt. 6:9; Isa. 43:10.

Kama Zaburi 110:3 linavyoonyesha, watu wa Yehova wanashiriki kwa hiari katika kazi ambayo Yehova ameamuru ifanywe. Kwa nini watu wa umri na malezi mbalimbali wanatumia nguvu zao katika kazi ya kuhubiri? Hasa, ni kwa sababu wanampenda Mungu na wanataka kumtumikia kwa moyo wote. Andiko la Kumbukumbu la Torati 6:5, 6 linatuamuru tumpende Yehova kwa ‘moyo wetu wote, nafsi yetu yote, na kwa nguvu zetu zote.’ Upendo huo wa kutoka moyoni unatusukuma tutumie wakati, nguvu, na mali zetu kuunga mkono kazi ya Ufalme wa Mungu. Njia moja ya kufanya hivyo ni kushiriki katika kazi ya kuhubiri kwa kadiri tunavyoweza.

Yehova ameagiza habari njema juu ya Ufalme wake ihubiriwe kotekote duniani kwa sababu anawapenda wanadamu. Hataki yeyote aangamizwe bali anataka wote watubu, waache mwenendo wao mpotovu, na kumgeukia Muumba wao ili waweze kupata kuishi milele. (2 Pet. 3:9) Yehova anasema hivi: “Ninapendezwa, si na kifo cha mwovu, bali kwamba mtu mwovu ageuke na kuiacha njia yake na kwa kweli aendelee kuishi.” (Eze. 33:11) Kazi yetu ya kuhubiri inathibitisha kwamba Yehova anawapenda wanadamu wenzetu. Bila shaka hilo linachangia shangwe na uradhi tunaopata tunaposhiriki katika utumishi huo wa maana.

Maoni yetu kuhusu Neno lake lililoongozwa kwa roho, yaani Maandiko Matakatifu, yanaonyesha pia kwamba tunampenda sana Yehova. Kama hatungekuwa na Biblia hatungemjua Mungu wala hatungeweza kumkaribia kama andiko la Yakobo 4:8 linavyotutia moyo tufanye. Hatungejua kusudi la maisha au mambo yatakayotokea wakati ujao. Hatungejua kwamba Adamu, babu wa kwanza wa wanadamu wote, ndiye chanzo cha matatizo yetu yote. (Rom. 5:12) Wala hatungejua kwamba Mungu anatupenda sana na alimtuma Mwana wake mzaliwa-pekee awe fidia kwa ajili yetu. Kwa njia nyingine nyingi, Yehova anatupa kiasi fulani cha ujuzi, hekima, na uelewaji wake. Tunathamini sana zawadi ambayo ametupa, yaani, Neno lake lililoongozwa kwa roho! Uthamini wetu kwa zawadi hiyo bora unatuchochea ‘tununue wakati’ kusoma, kujifunza, na kutafakari maneno ya Yehova. (Efe. 5:15, 16; Zab. 1:1-3) Hatupaswi kamwe kuona vibaya kutenga wakati kusoma Neno la Mungu kila siku, bali tunapaswa kuvutiwa kulisoma kwa sababu tunampenda Mungu. Hilo linatuwezesha kumjua na kumpenda zaidi.

Tumejifunza katika Biblia kwamba wazao wote wa Adamu, kutia ndani sisi, walijikuta katika hali mbaya sana bila tumaini kwa sababu Adamu alimkosea Yehova. Lakini, Mungu anaweza kuwasaidia wanadamu, na amefanya hivyo kwa kuchukua hatua ya kuhakikisha kwamba kusudi lake kuhusu dunia litatimia.—Mwa. 3:15.

Bila shaka, kila mmoja wetu anataka sana kutakasa jina lisilo na kifani la Mungu wetu. Tunapoendelea kujua vizuri zaidi sifa nzuri za Yehova Mungu, tunasukumwa kushirikiana naye na tengenezo lake kutangaza jina lake kuu na kusudi lake. Tuna hakika kwamba tutaendelea kupata kibali na baraka zake sasa, na uzima wa milele katika ulimwengu mpya.

Sisi tunaotumika katika Baraza Linaloongoza tunataka kuwahakikishia ninyi ndugu na dada kwamba tunawapenda. Tunataka pia kuwashukuru sana kwa jitihada zenu za kutumia wakati unaobaki kabla ya “dhiki kuu” kuwahubiria watu wengi iwezekanavyo habari njema. (Ufu. 7:14) Mnapofanya kazi hiyo, mnawapa watu nafasi ya kupata ujuzi ambao ninyi wenyewe tayari mmepata, yaani, ujuzi kumhusu Mungu na Kristo unaoongoza kwenye uzima wa milele.—Yoh. 17:3.

Ndugu zenu,

Baraza Linaloongoza la Mashahidi wa Yehova

[Picha katika ukurasa wa 4]

Carey W. Barber

[Picha katika ukurasa wa 4]

John E. Barr

[Picha katika ukurasa wa 4]

Samuel Herd

[Picha katika ukurasa wa 4]

Geoffrey Jackson

[Picha katika ukurasa wa 4]

Stephen Lett

[Picha katika ukurasa wa 5]

Theodore Jaracz

[Picha katika ukurasa wa 5]

Gerrit Lösch

[Picha katika ukurasa wa 5]

Anthony Morris III

[Picha katika ukurasa wa 5]

Guy Pierce

[Picha katika ukurasa wa 5]

David Splane

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki