Mahangaiko
Je, una mahangaiko kwa sababu ya matatizo kama vile, umaskini, njaa, au kukosa mahali pa kuishi?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
Omb 3:19—Baada ya uharibifu wa Yerusalemu, nabii Yeremia na Waisraeli wenzake wengi hawakuwa na mahali pa kuishi
2Ko 8:1, 2; 11:27—Umaskini wa kupindukia unawaathiri Wakristo huko Makedonia, na mara nyingi mtume Paulo anakosa chakula, mavazi, na mahali pa kuishi
Maandiko yenye kufariji:
Tazama pia Kum 24:19
Je, una mahangaiko kwa sababu unaogopa kukosa marafiki, kuwa mpweke, au kutopendwa?
Masimulizi ya Biblia yanayohusika:
1Fa 18:22; 19:9, 10—Nabii Eliya anahisi kwamba yeye peke yake ndiye mtumishi mwaminifu wa Yehova aliyebaki
Yer 15:16-21—Nabii Yeremia anahisi upweke kwa sababu watu wanaomzunguka wanakazia fikira zaidi starehe na kupuuza ujumbe wa Yehova
Maandiko yenye kufariji:
Masimulizi ya Biblia yenye kufariji:
1Fa 19:1-19—Yehova anampatia nabii Eliya msaada hususa, anasikiliza mahangaiko yake kwa subira, na anamtia moyo kwa kumwonyesha waziwazi nguvu Zake
Yoh 16:32, 33—Yesu anajua kwamba rafiki zake watamwacha, lakini pia anajua kwamba kwa kweli hayuko peke yake