Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g05 9/8 kur. 11-12
  • Upatano Utakapoenea Ulimwenguni Pote

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Upatano Utakapoenea Ulimwenguni Pote
  • Amkeni!—2005
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Amani na Upatano wa Kweli
  • Paradiso Iko Karibu!
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Toleo la Watu wote)—2021
  • Jinsi Wewe Unaweza Kuona Amani ya Kimungu kwa Ukamili Zaidi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1987
  • Njia ya Kurudia Paradiso
    Amkeni!—1997
  • Kwa Nini Tunamhitaji Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2005
g05 9/8 kur. 11-12

Upatano Utakapoenea Ulimwenguni Pote

MAISHA yangependeza kwelikweli ikiwa kungekuwa na upatano, bila mvurugo na mizozo. Lakini kama tu Biblia ilivyotabiri kuhusu nyakati zetu, watu ‘hawataki makubaliano yoyote.’—2 Timotheo 3:1-5.

Hata hivyo, katika hali hizi ngumu, mamilioni ya watu wenye mioyo minyoofu wanajifunza kuishi pamoja kwa amani na upatano wa kweli. Jinsi gani? Kwa kukubali mwaliko mchangamfu unaopatikana katika Biblia kwenye Isaya 48:17, 18. Andiko hilo linasema: “Mimi, Yehova, ni Mungu wako, Yeye anayekufundisha ili ujifaidi mwenyewe, Yeye anayekufanya uende katika njia unayopaswa kutembea ndani yake. Laiti ungesikiliza amri zangu! Ndipo amani yako ingekuwa kama mto, na uadilifu wako kama mawimbi ya bahari.”

Tunapokubali mwaliko huo mchangamfu, kwa njia fulani Yehova hutufaidi. Anatuonyesha jinsi tunavyoweza “kutembea” kwa amani na upatano wa kweli. Ni upumbavu kutenda kinyume cha hilo, yaani, kufuata nadharia na falsafa za wanadamu wasio wakamilifu. Historia ya wanadamu imethibitisha tena na tena ukweli huu wa msingi unaotajwa katika Yeremia 10:23: “Njia ya mtu wa udongo haimo katika uwezo wake. Mwanadamu anayetembea hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” Kwa ufupi, hatuna uwezo wa kujiongoza na kujiwekea sheria za maadili zinazofaa na zinazokubalika ulimwenguni pote. Mungu ndiye mwenye haki ya kufanya hivyo.—Isaya 33:22.

Amani na Upatano wa Kweli

Hivi karibuni Mungu atafanya dunia yetu iwe na upatano. Anaahidi wakati ambapo “dunia hakika itajawa na kumjua Yehova kama vile maji yanavyoifunika bahari.” (Isaya 11:9) Naam, mwishowe kutakuwa na amani inayodumu.

Kwa kweli, viumbe duniani watashirikiana kwa njia mpya, kwa kuwa Mungu atawafundisha wanadamu washikamanifu jinsi ya kutunza makao yao ya kidunia kwa ustadi. Hata ‘atafanya agano’ kwa njia ya mfano na wanyama wote wakali, na kuwafanya wajitiishe kwa wanadamu kwa amani.—Hosea 2:18; Mwanzo 1:26-28; Isaya 11:6-8.

Hiyo si ndoto tu. Katika Mahubiri ya Mlimani, Yesu alitaja jambo hilo mara mbili. Kwanza alisema: “Wenye furaha ni wale walio na tabia-pole, kwa kuwa watairithi dunia.” Kisha, alipokuwa akiwafundisha wanafunzi wake jinsi ya kusali, alisema: “Baba yetu . . . , mapenzi yako na yatendeke duniani kama ilivyo mbinguni.” (Mathayo 5:5; 6:9, 10) Alipokaribia kufa, Yesu alieleza kifupi hilo litamaanisha nini kwa wanadamu kwa kutumia neno moja zuri, “paradiso.” (Luka 23:43) Naam, damu ya Yesu iliyomwagwa hufanya tumaini la kuishi milele katika dunia paradiso liwe hakika!—Yohana 3:16.

[Picha katika ukurasa wa 12]

Katika Paradiso ya Mungu inayokuja, viumbe duniani watashirikiana kwa njia mpya

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki