Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 12/15 uku. 14
  • Kuimulika Ulaya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Kuimulika Ulaya
  • Amkeni!—2015
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • Faida za Sauti ya Mama
  • Je, Wanachochewa Kujiona Kuwa Bora Kuliko Wengine?
  • Wana Mtazamo Mzuri Licha ya Kutimiza Miaka 100
  • Kuishi Miaka Mingi—Je, Siri Inapatikana Okinawa?
    Amkeni!—2008
  • Daraka Lenu Kama Wazazi
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Kulea Watoto Wenye Kujali Katika Ulimwengu Wenye Ubinafsi
    Amkeni!—2013
  • Kuwa na Watoto— Daraka na Thawabu
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 12/15 uku. 14
Mama anazungumza na mtoto wake

KUUTAZAMA ULIMWENGU

Kuimulika Ulaya

Zamani Ulaya lilikuwa eneo la kidini, lakini sasa watu wengi hawapendezwi na dini. Hata hivyo, hebu ona jinsi habari za karibuni kuhusu Ulaya zinavyohusiana na Biblia.

Faida za Sauti ya Mama

Watafiti jijini Milan nchini Italia waligundua kwamba watoto wanaozaliwa kabla ya wakati, yaani njiti, hunufaika kiafya wanaposikia sauti za mama zao kupitia kifaa wanachovalishwa mkononi wakiwa hospitalini. Mbinu hii inafanana na ile ambayo mtoto hutumia kuhisi sauti ya mama yake akiwa tumboni. Utafiti huo ukamalizia hivi: “Watoto wanaozaliwa kabla ya wakati wanafaidika sana wanaposikia sauti ya mama tangu wanapozaliwa.”

BIBLIA INAFUNDISHA NINI: “Nimeituliza na kuinyamazisha nafsi yangu kama mtoto aliyeachishwa kunyonya juu ya mama yake.”—Zaburi 131:2.

Je, Wanachochewa Kujiona Kuwa Bora Kuliko Wengine?

Utafiti uliofanywa ukihusisha watoto 565 nchini Uholanzi, ulionyesha kwamba watoto ambao walionwa na wazazi wao kuwa “bora kuliko wengine” na wanapaswa “kutendewa kwa njia ya pekee,” waligunduliwa kuwa na ubinafsi zaidi, walijiona kuwa bora kuliko wenzao, na wenye haki ya kupewa chochote wanachotaka. Mwandishi alisema: “Watoto huamini wazazi wao wanapowaeleza kwamba wao ni bora kuliko wengine, na jambo hilo linaweza kuwa na madhara kwao na kwa jamii.”

BIBLIA INAFUNDISHA NINI: “Namwambia kila mtu hapo kati yenu asijifikirie mwenyewe zaidi kuliko ilivyo lazima kufikiri; bali kufikiri ili awe na akili timamu.”—Waroma 12:3.

Wana Mtazamo Mzuri Licha ya Kutimiza Miaka 100

Mtafiti fulani wa Chuo Kikuu cha Heidelberg nchini Ujerumani aliripoti kwamba watu walio na umri wa miaka 100 na zaidi bado wanatamani sana kuendelea kuishi licha ya matatizo ya afya na udhaifu mwingine. Kati ya kila wazee wanne waliohojiwa, watatu walisema wanatamani kuendelea kuishi na wanajitahidi kufurahia maisha kadiri wawezavyo. Walitimiza malengo yao, walikuwa na tumaini na mtazamo unaofaa, walikuwa na kusudi maishani, na walidumisha viwango vya maadili na vya kidini.

JAMBO LA KUFIKIRIA: Kulingana na andiko la Mhubiri 3:11, tamaa yetu ya kuendelea kuishi inaonyesha nini?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki