Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • fl sura 8 kur. 97-113
  • Daraka Lenu Kama Wazazi

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Daraka Lenu Kama Wazazi
  • Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • DARAKA LA MAANA LA MAMA
  • KUJIFUNZA UPENDO KWA KUPENDWA
  • DARAKA LA MAANA SANA LA BABA
  • BABA NA MAMA NI WENZI
  • JE! NI VYEPESI KUWAHESHIMU NINYI WAZAZI?
  • MAZINGIRA (HALI) YA NYUMBANI
  • Zoeza Mtoto Wako Tangu Utoto Mchanga Sana
    Siri ya Furaha ya Familia
  • Kulea Watoto tangu Uchanga
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Kuwa na Watoto— Daraka na Thawabu
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
  • Ubora wa Kutia Adabu katika Upendo
    Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
Pata Habari Zaidi
Kufanya Maisha ya Jamaa Yako Yawe Yenye Furaha
fl sura 8 kur. 97-113

Sura ya 8

Daraka Lenu Kama Wazazi

1-3. (a) Kuzaliwa kwa kitoto kichanga kunaweza kuletea wazazi matokeo gani? (b) Sababu gani ni jambo la maana baba na mama wafahamu madaraka yao kama wazazi?

KATIKA MAISHA matukio mengi yanatupasa sisi kwa kiasi kidogo sana. Mengine yana matokeo makubwa na yenye kuendelea. Kwa wazi kuzaliwa kwa mtoto kuna matokeo makubwa na yenye kuendelea. Tokea hapo maisha ya mume na mke hayatakuwa kama yalivyokuwa hapo mwanzo. Ijapokuwa ni mdogo sana, mgeni huyo nyumbani atajifanya mwenyewe asikiwe kwa sauti na kuwapo kusikoweza kusahauliwa.

2 Bila shaka maisha ya wazazi yatakuwa yenye maana zaidi na yenye furaha zaidi. Lakini yanaleta daraka, na, kwa matokeo bora zaidi, daraka hilo lahitaji kutimizwa na wazazi wote wawili. Kuzaa mtoto kuliwataka ninyi wawili, na ninyi wawili mna daraka la maana sana katika ukuzi wa mtoto tangu kuzaliwa kwake na kuendelea. Hapo mbeleni, uhitaji wa kuwa na ushirikiano wa unyofu wa moyo, wa kuwa na umoja— na wa unyenyekevu haukuwa mkubwa zaidi kama ulivyo sasa.

3 Kulifahamu daraka la kila mzazi na namna madaraka hayo yanavyoweza kupatana kutasaidia sana mtimize mahitaji ya mtoto wenu, kulete matokeo yenye furaha. Usawa wahitajiwa. Hata ijapokuwa akili zinajitahidi kuwa za kiasi, maono ya moyoni yanaziondoa katika usawa. Huenda tukaelekea kutenda ma mbo kupita kiasi tangu mambo yaliyo machache mno mpaka kwenye mambo yaliyo mengi mno, kisha kuyarudia yaliyo machache mno. Baba anatakiwa atumie ukichwa wake, lakini, akiutumia kupita kiasi, anakuwa mwonezi. Yamfaa mama ashiriki kulea na kuwatia watoto adabu, lakini kufanya kazi hizo peke yake bila baba kunaharibu mpango wa jamaa. Chema ni chema, lakini chema kinakuwa kibaya ikiwa kinafanywa kupita kiasi.—Wafilipi 4:5.

DARAKA LA MAANA LA MAMA

4. Ni mambo gani machache ambayo kitoto kichanga kinahitaji kutoka kwa mama yake?

4 Kitoto kinachozaliwa hivi karibuni kinategemea kabisa mama yake kipate mahitaji ya wakati huo. Mama akikipa mahitaji hayo, kitoto kinajiona salama. (Zaburi 22:9, 10) Kinapaswa kilishwe vizuri na kuwekwa safi na kupashwa moto; lakini kutoa mahitaji ya kimwili hakutoshi. Mahitaji ya moyoni ni ya maana sana. Mtoto asipoonyeshwa upendo, anakuwa bila usalama. Upesi mama anaweza kujifunza kujua namna uhitaji huo ulivyo mkubwa sana wakati kitoto chake kichanga kinapotaka kuangaliwa. Lakini kilio chake kikiendelea kuonwa kama mchezo tu, huenda kitoto kikawa kigonjwa. Kikikosa kuonyeshwa upendo kwa muda mrefu kinaweza kuwa bila furaha maisha yake yote.

5-7. Kulingana na uchunguzi wa karibuni, upendo na uangalifu wa mama unakifanya kitoto kichanga kiwe namna gani?

5 Majaribio katika mahali mbalimbali yamehakikisha ukweli huu: Vitoto vichanga vinakuwa vigonjwa na hata kufa vikikosa kuonyeshwa upendo unaoonyeshwa kwa kusema na kugusa, kupigapiga kwa upole na kukumbatiwa. (Linganisha Isaya 66:12; 1 Wathesalonike 2:7) Ijapokuwa huenda wengine wanafanywa hivyo, bila shaka mama ambaye katika tumbo lake la uzazi kitoto hicho kilitoka na kutunzwa kwa miezi ya kwanza ya maisha, yamfaa sana afanye hivyo. Kuna hali ya asili ya kutendeana inayotukia kati ya mama na mtoto. Tamaa yake ya asili ya kumshika karibu sana naye mtoto mchanga aliyezaliwa sasa hivi, inalingana na ile ya kitoto kichanga ya kutafuta matiti (maziwa).

6 Uchunguzi umeonyesha kwamba ubongo wa kitoto kichanga unatenda kazi kwa bidii sana na maendeleo ya akili yanaongezwa wakati fahamu zake za kugusa, kusikia, kuona na kunusa zinapoamshwa. Wakati kitoto kichanga kinaponyonya, kinafahamu umotomoto na harufu ya ngozi ya mama yake. Kinaendelea kutazama uso wa mama anapokilisha. Si sauti yake tu anayosikia wakati anaposema au kuimba, bali vilevile mdundo (mpigo) wa moyo wa mama yake, sauti ambayo kilisikia wakati kilipokuwa bado katika tumbo la uzazi. Katika kitabu cha nchi ya Norway, mchunguzi wa magumu yanayopata akili za watoto, Anne-Marit Duve, anaeleza hivi:

“Kwa kuwa utendaji wa wanafunzi unaonyesha waziwazi kadiri ubongo unavyotenda, tunayo sababu ya kusadiki kwamba kadiri kubwa ya kuamshwa kwa ngozi, kadiri kubwa ya kugusana—hata kule kugusana kunakohusiana na kunyonyesha—inaweza kuamsha akili zipate kutenda, nayo yaweza kuongoza kwenye uwezo wa akili ulio mkubwa zaidi katika utu mzima.”

7 Basi, kitoto kichanga kinapoona kila mara mguso wa mama, wakati anapokiinua, kukikumbatia au kukiogesha na kukikausha maji, ile hali ya kuamshwa ambayo kinapokea ina sehemu ya maana sana katika ukuzi wake na kitakavyokuwa katika maisha yake ya baadaye. Ijapokuwa kuamka usiku na kutumia wakati kumbembeleza (kumtuliza) mtoto mchanga anayelia huenda kusifurahishe sana, kujua faida zinazotokea baadaye kunaweza kufidia (kulipia) sana hasara ya usingizi.

KUJIFUNZA UPENDO KWA KUPENDWA

8-10. (a) Kitoto kichanga kinajifunza nini kutokana na upendo wa mama yake? (b) Sababu gani hilo ni jambo la maana sana?

8 Kupendwa kwa mtoto mchanga ni kwa maana sana ili akuze maono ya moyoni. Anajifunza kupenda kwa kupendwa, kwa kuona mifano ya upendo. Likizungumza juu ya kumpenda Mungu, 1 Yohana 4:19 lasema: “Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda kwanza.” Mafundisho ya kwanza ya kuonyesha upendo yamtegemea sana mama. Mama anainama amfikie mtoto katika kitanda chake, anaweka mkono wake kifuani mwake na kumtikisa polepole wakati anapoweka uso wake karibu na mtoto na kusema, ‘Nakuona! Nakuona!’ Kwa kweli, mtoto mchanga hayajui maneno hayo (ambayo hayana maana sana kwa vyo vyote). Lakini kitoto kinafurukuta-furukuta na kutoa mlio wa furaha, maana kinajua mkono huo wa mchezo na aina hiyo ya sauti vinakiambia waziwazi hivi, ‘Nakupenda! Nakupenda!’ Kinatulizwa moyo na kujisikia salama.

9 Vitoto vichanga na watoto wakubwa kidogo kuliko hivyo wanaoonyeshwa upendo wanauthamini, na, kwa kuiga upendo huo, wanajizoeza kuuonyesha, wakiweka mikono midogo yao katika shingo ya mama na kumbusu kwa shauku sana. Kama matokeo, wanapendezwa na itikio la upendo lenye kuchangamsha moyo wanalopokea kutoka kwa mama yao. Wanaanza kujifunza soma la maana la kwamba kuna furaha katika kutoa upendo kama zilivyo katika kuupokea, kwamba kwa kupanda upendo nao wanavuna upendo. (Matendo 20:35; Luka 6:38) Ushuhuda unaonyesha kwamba ikiwa mtoto anaanza mapema kukosa kumpenda mama yake, baadaye huenda akaona ugumu wa kupenda na kutumikia wengine.

10 Kwa kuwa watoto wanaanza kujifunza mara baada ya kuzaliwa, miaka ile michache ya kwanza ndiyo ya maana sana. Wakati wa miaka hiyo upendo wa mama ni wa maana sana. Akiweza kuonyesha na kufundisha upendo—si kujifurahisha mwenyewe—anaweza kufanya jambo lenye faida ya kudumu; akishindwa anaweza kufanya jambo lenye hasara ya kudumu. Kuwa mama mwema ni mojawapo ya kazi ngumu na zenye kuthawabisha ambazo mwanamke anaweza kuwa nazo. Ijapokuwa shida na magumu yake, ni kazi gani ya maisha ambayo ulimwengu unatoa inayoweza kuwa ya maana na yenye kuleta furaha kama kazi hiyo ya mama?

DARAKA LA MAANA SANA LA BABA

11. (a) Baba anawezaje kutia daraka lake katika akili za mtoto? (b) Sababu gani hilo ni la lazima?

11 Ni kawaida kwamba wakati wa utoto mchanga mama ndiye mwenye daraka kuu zaidi katika maisha ya mtoto. Lakini tangu kuzaliwa kwa kitoto kichanga na kuendelea, imempasa baba vilevile ashiriki daraka la kusaidia kitoto kichanga. Hata mtoto anapokuwa bado ni kitoto kichanga, baba anaweza, naye imempasa ashiriki, na kukiangalia kitoto kichanga nyakati nyingine, akicheza nacho, kukituliza wakati kinapolia. Katika njia hiyo baba anakaa imara katika akili za mtoto. Mwishowe daraka la baba limepaswa liendelee kuwa kubwa kuliko la mama. Akikawia kuanza upesi, huenda ukawa mwanzo wa tatizo linalotokea sana sana wakati mtoto anapokuwa mwenye umri wa kati ya miaka kumi na mitatu na kumi na tisa, wakati inapokuwa vigumu kumtia mtoto adabu. Sana sana mtoto wa kiume mwenye umri wa kati ya miaka kumi na mitatu na kumi na tisa anahitaji msaada wa baba yake. Lakini ikiwa uhusiano mzuri haukutangulia kuwekwa, lile pengo lililofanyizwa miaka mingi haliwezi kuzibwa kwa muda wa juma chache.

12, 13. (a) Baba ana daraka gani katika jamaa? (b) Maoni ya watoto juu ya mamlaka yanaweza kugeuzwaje na jinsi baba anavyotimiza madaraka yake kwa kufaa?

12 Kwamba mtoto ni wa kiume au wa kike, zile sifa za kiume za baba zinaweza kumsaidia asitawishe utu kamili, uliosawazika. Neno la Mungu linaonyesha kwamba baba ndiye kichwa cha jamaa. Yeye ana daraka la kuwapatia mahitaji ya kimwili. (1 Wakorintho 11: 3 ; 1 Timotheo 5:8) Hata hivyo, “mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha [Yehova] .” Kwa habari ya watoto wake, baba anaamriwa vilevile ‘awalee katika adabu na maonyo ya [Yehova]’ (Kumbukumbu la Torati 8:3; Waefeso 6:4) Ijapokuwa kuwapenda watoto wake kama ilivyo kawaida kumepaswa kumwongoze, zaidi ya yote, ni kufahamu daraka lake kwa Muumba wake ndiko kumepaswa kumwongoze ajitahidi kulitimiza agizo lake alilopewa na Mungu.

13 Pamoja na uchangamshi, upole na huruma ambazo mama anaonyesha, baba anaweza kutoa uongozi wenye kuimarisha, ulio na nguvu na wenye usimamizi wa hekima. Maoni ambayo baadaye watoto wake wataonyesha juu ya mamlaka ya kibinadamu na ya kimungu, kwamba ni kuiheshimu ama kutokuiheshimu, yatategemea namna anavyotimiza mgawo aliopewa na Mungu. Hilo pia litapasa namna watakavyoweza kufanya kazi vizuri bila kuchukia wala kuasi, wakisimamiwa na mtu mwingine.

14. Mfano mwema wa baba unaweza kuwa na matokeo gani kwa mwana au binti?

14 Akiwa ana mtoto wa kiume, mfano wa baba na namna anavyosimamia mambo unaweza kusaidia sana kujua kama mtoto huyo wa kiume anaendelea kuwa mtu mnyonge na mwenye kusita-sita, au anazidi kuwa mtu hodari, aliye imara, anayeonyesha uhodari wa kusadikishwa na anayo nia ya kutimiza daraka. Unaweza kuonyesha mwishowe mwana huyo atakuwa mume au baba wa aina gani—mwenye kushikilia jambo moja tu, asiye na kiasi, mkali, au aina ya mtu aliyesawazika, mwenye ufahamu na mwenye fadhili. Ikiwa katika jamaa hiyo kuna binti, uongozi na uhusiano wa baba unaweza kugeuza maoni yake yote juu ya wanaume, unaweza kusaidia ama kuzuia ndoa yake isifanikiwe wakati ujao. Matokeo ya uongozi huo wa baba yanaanza tangu uchanga.

15, 16. (a) Ni daraka gani la kufundisha ambalo Biblia inamwekea baba? (b) Hilo laweza kutimizwaje?

15 Kadiri daraka la baba la kufundisha linavyopaswa kutimizwa inaonyeshwa katika maagizo ambayo Mungu aliwapa watu wake katika Kumbukumbu la Torati 6:6, 7: “Maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako; nawe uwafundishe watoto wako kwa bidii, na kuyanena uketipo katika nyumba yako, na utembeapo njiani, na ulalapo, na uondokapo.”

16 Si maneno yenyewe tu yanayopatikana katika Neno la Mungu, bali vilevile ule ujumbe (habari) unaotolewa nayo unapaswa ukazwe kila siku katika akili za mtoto. Kuna nafasi hizo sikuzote. Maua bustanini, wadudu hewani, ndege au kindi (wanyama wadogo) katika miti, makombe ya baharini pwani, matunda ya misunobari milimani, nyota zinazometameta angani usiku—maajabu yote hayo yanamshuhudia Muumba, nawe imekupasa uwaeleze watoto wako maana ya maneno yao. Mtunga zaburi anasema: “Mbingu zauhubiri utukufu wa Mungu, na anga laitangaza kazi ya mikono yake. Mchana husemezana na mehana, usiku hutolea usiku maarifa.” (Zaburi 19:1, 2) Kwa kuwa tayari kutumia mambo hayo, na sana sana kutumia mambo ya maisha ya kila siku ili atoe mifano na kukazia kanuni za haki na katika kuonyesha hekima na faida ya shauri la Mungu, baba anaweza kutia katika akili na moyo wa mtoto wake msingi ulio wa maana sana kwa wakati ujao: si kusadikishwa tu kwamba kuna Mungu, bali vilevile kwamba yeye “huwapa thawabu wale wamtafutao” kwa bidii.—Waebrania 11:6.

17, 18. (a) Baba amepaswa awatieje watoto wake adabu? (b) Njia yenye matokeo sana kuliko kufanya sheria nyingi ni nini?

17 Vilevile kutia adabu ni sehemu ya daraka la baba. “Ni mwana gani asiyetiwa adabu na baba?” ndilo ulizo linaloulizwa katika Waebrania 12:7, NW. Lakini ni wajibu wake kufanya hivyo kwa kiasi, bila kuonya makosa kupita kiasi kwa kadiri ya kumkasirisha au hata kumtesa mtoto. Neno la Mungu linawaambia akina baba hivi, “Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, wasije wakakata tamaa.” (Wakolosai 3:21) Vizuizi ni vya lazima, lakini mara nyingine tunaweza kuzidisha na kuongeza sheria nyingi mpaka ziwe mzigo na kuvunja moyo.

18 Mafarisayo wa nyakati za kale walipenda sana sheria; walifanya sheria nyingi sana na kufanyiza wanafiki wengi. Ni makosa ya kibinadamu kudhani kwamba magumu yanaweza kumalizwa kwa kutunga sheria nyingi zaidi; lakini yanayoonwa maishani yanaonyesha wazi kwamba njia iliyo ya kweli kuliko sheria nyingi ni kuufikia moyo. Kwa hiyo usitumie sheria nyingi, badala yake, jaribu kukazia kanuni, ukielekeza upande ambao Mungu mwenyewe anaelekeza: “Nitawapa sheria zangu katika [akili] zao, na katika mioyo yao nitaziandika.”—Waebrania 8:10.

BABA NA MAMA NI WENZI

19. Ili kuweko kupashana habari vizuri katika nyumba, ni jambo gani linaloweza kufanywa?

19 Kwa kawaida baba ndiye anayetoa riziki, na anaporudi nyumbani kutoka kazini huenda akawa amechoka, na bado labda anazo kazi nyingine za kufanya. Lakini imempasa atafute wakati wa kuwa pamoja na mke wake na watoto wake. Inampasa aongee na jamaa yake, aweke wakati wa mazungumzo ya jamaa na wa kufanya kazi za jamaa, wakati wa kucheza pamoja na jamaa au kwenda kwenye matembezi pamoja na jamaa yake. Umoja na ushirika wa jamaa unaimarishwa katika njia hiyo. Labda kabla watoto hawajazaliwa yeye na mke wake walikuwa wakitumia wakati mwingi wakiwa katika matembezi. Lakini sasa ikiwa wangezidi kufanya hivyo, wakienda huku na huku na labda wa kikaa huko mpaka wanaporudi wakiwa wamechelewa sana, huko hakungepatana na daraka la uzazi. Lingekuwa jambo baya sana kwa watoto wao. Upesi, wazazi hao wangepata hasara kwa sababu ya kutokuwa na utaratibu na kutimiza daraka lao. Kama watu wazima, watoto wanakuwa na hali bora wakati maisha yao yanapokuwa na hali imara na utaratibu wa msingi; hiyo inaleta afya ya akili, ya mwili na ya moyoni. Kazi za kila siku za maisha ya jamaa zitajaa tele mambo mazuri na yasiyo mazuri pasipo wazazi kuyaongeza.—Linganisha Mathayo 6:34; Wakolosai 4:5.

20. Unapokuwa wakati wa kutia watoto adabu, wazazi wanaweza kufanya nini hivi kwamba wataungana katika jitihada zao?

20 Imewapasa baba na mama washirikiane pamoja katika kutendea watoto, kuwafundisha, kuwawekea vizuizi, kuwatia adabu, kuwapenda. ‘Nyumba inayojigawanya yenyewe haiwezi kusimama.’ (Marko 3: 25, NW) Inawapasa wazazi wazungumze pamoja adabu itakayotolewa; ndipo wanapoweza kuepuka kufanya watoto waone tofauti ye yote kati ya wazazi wao juu ya adabu inayotolewa. Kufanya vingine kungeweza kuwaruhusu watoto wajaribu kugawanya wazazi kisha wawatawale. Ni kweli huenda ikawa kwamba pindi fulani, mzazi mmoja anatenda bila kufikiri au kwa hasira na kutoa adabu ya kupita kiasi, au, wakati ushuhuda wote unapofikiriwa, inaonekana kwamba adabu hiyo haikuwa ya lazima sana. Labda itawezekana wazazi wazungumze hilo kwa faragha bila watoto kuwapo) kisha yule mzazi aliyetenda bila hekima anaweza kuchagua kwa kupenda kwake mwenyewe kutengeneza mambo hayo pamoja na mtoto. Au, ikiwa haiwezekani kuzungumza hivyo kwa faragha, yule mzazi anayedhani kwamba kumwunga mkono mwenzi wake kungemaanisha kuunga mkono udhalimu (tendo lisilo la haki), anaweza kusema jambo kama hili, ‘Nafahamu sababu gani umekasirika, mimi vilevile ningekasirika. Lakini labda kuna jambo fulani ambalo hukulijua, nalo ni . . .’ kisha aeleze lo lote ambalo anaona kwamba liliachwa bila kuangaliwa. Hiyo inaweza kuleta matokeo yenye kutuliza pasipo kuonyesha mgawanyiko wala kutopatana mbele ya mtoto anayetiwa adabu. Kama mithali iliyoongozwa na Mungu inavyosema: “Kiburi huleta mashindano tu; bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.”—Mithali 13:10; tazama vilevile Mhubiri 7:8.

21. Je! mzazi mmoja aachiwe kazi ya kutia watoto adabu? Sababu gani au sababu gani sivyo?

21 Maandiko ya Kiebrania yanaonyesha kutia adabu kuwa daraka la watu wawili: “Mwanangu, yasikilize mafundisho ya baba yako, wala usiiache sheria ya mama yako.” Maandiko ya Kikristo ya Kigiriki yanasema vivyo hivyo: “Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, maana hii ndiyo haki.” Mara nyingine baba anakuona kutia watoto adabu kuwa kazi ya mke wake. Au, huenda mke akawa na maoni tofauti, asifanye lo lote ila kumtisha tu mtoto asiye na adabu kwa kusema ‘Wewe ngoja baba yako arudi nyumbani, utaona !’ Lakini ili iweko furaha ya jamaa na kila mzazi apendwe na kuheshimiwa na watoto, daraka hilo lapaswa lishirikiwe na wote wawili.—Mithali 1:8; Waefeso 6:1.

22. Ni jambo gani linalopaswa kuepukwa wakati wa kujibu maombi ya mtoto, na kwa sababu gani?

22 Watoto wanahitaji waone wazazi wao wakiungana katika jambo hili na kila mmoja akiwa na nia ya kutimiza daraka lake. Ikiwa nyakati zote mtoto anayeomba kitu anamsikia baba yake akisema, ‘Nenda kamwulize mama yako,’ au sikuzote mama akimsukumizia baba uamuzi, basi mzazi anayepata kuona kwamba ombi hilo linamtaka kujibu “Hapana” anaonwa kuwa mbaya kabisa. Bila shaka, huenda zikawako hali wakati baba anapoweza kusema, ‘Ndiyo, unaweza kwenda ukacheze nje kidogo—lakini mwulize mama yako kwanza ili ujue wakati chakula cha jioni kitakapokuwa tayari.’ Au labda nyakati nyingine mama anaweza kuona kwamba, ijapokuwa hawezi kupinga ombi fulani, imempasa mume wake aamue jambo hilo. Lakini wote wawili watakuwa macho kuona kwamba hawamtii moyo wala kumruhusu mtoto katika njia yo yote awachonganishe wazazi kusudi atimize lengo lake. Vilevile mke mwenye hekima ataangalia asije akatumia fungu lake la mamlaka anayoshiriki na mume wake katika njia ya kushindana, akijaribu kwa kubembeleza, apendwe sana na mtoto kuliko mume wake.

23. Katika jamaa, je! ni lazima baba peke yake ndiye atoe maamuzi?

23 Kwa kweli, huenda katika maamuzi ya jamaa kila mshiriki akawa na mambo ambayo katika hayo uamuzi wake wastahili uchunguzi wa pekee. Baba analo daraka la kuamua mambo yanayopasa hali njema yote ya jamaa, mara nyingi anaamua hayo akiisha kuyazungumza pamoja na wengine na kufikiria matakwa yao na mambo ambayo wanapendelea zaidi. Mama anaweza kufanya maamuzi ya mambo ya jikoni na mambo mengine mengi ya nyumbani. (Mithali 31:11, 27) Wanapokuwa wakubwa, labda watoto wanaweza kuruhusiwa kufanya maamuzi juu ya mahali wanakotaka kucheza, namna fulani ya mavazi, au mambo fulani mengine ambayo ni ya kibinafii. Lakini lazima wazazi wasimamie hayo na kuhakikisha kwamba kanuni njema zimefuatwa, usalama wa watoto hauko hatarini na kwamba haki za wengine haziingiliwi. Jambo hilo laweza kuwapa watoto mwanzo wa polepole katika kufanya maamuzi.

JE! NI VYEPESI KUWAHESHIMU NINYI WAZAZI?

24. Uhakika wa kwamba inawapasa watoto waheshimu baba yao na mama yao, unawekea wazazi daraka gani?

24 Watoto wanaambiwa hivi, “Waheshimu baba yako na mama yako.” (Waefeso 6:2; Kutoka 20:12) Kufanya kwao hivyo ni kuheshimu amri ya Mungu vilevile. Je, ninyi mnawafanyia iwe vyepesi? Wewe mke, unaa mbiwa kumheshimu na kumstahi mume wako. Je! huoni ni vigumu kwako kufanya hivyo ikiwa hajitahidi kufuata yale anayotakiwa na Neno la Mungu kufanya? Mume, inakupasa umthamini na kumheshimu mke wako kama mwenzi wa kusaidia umpendaye. Je! si vigumu kufanya hivyo, ikiwa hakusaidii? Basi wafanyieni watoto wenu iwe vyepesi kutii amri ya Mungu inayosema wawaheshimu ninyi, wazazi wao. Pateni heshima yao kwa kuwapatia makao yenye amani, kanuni njema, mifano myema ya mwenendo wenu wenyewe, mafundisho na malezi mama, na adabu ya upendo inapokuwa ya lazima.

25. Ni magumu gani yanayoweza kutokea wakati wazazi hawaungani pamoja juu ya namna watoto wanavyopaswa wapewe malezi?

25 “Afadhali kuwa wawili kuliko mmoja,” ndivyo alivyosema Mfalme Sulemani, “maana wapata ijara njema kwa kazi yao.” (Mhubiri 4:9) Watu wawili wanapotembea pamoja na mmoja anaanguka, mwenzake yupo asaidie kumwinua. Vivyo hivyo, katika jamaa mume na mke wanaweza kusaidiana na kutiana moyo ili kila mmoja atimize daraka lake. Madaraka kayo yanapatana sana katika mambo mengi sana ya uzazi, na hilo ni jambo jema kwa umoja wa jamaa. Wamepaswa watoto wawalete wazazi wao karibu zaidi, wakiwaunganisha katika kazi moja ya kuona malezi. Lakini mara nyingine huenda yakatokea maulizo yenye kugawanya wazazi juu ya namna mtoto anavyopaswa kupewa malezi na kutiwa adabu. Mara nyingine mke anakaza fikira nyingi mno juu ya mtoto hata mume wake anajiona kama ametupiliwa mbali, hata anaona uchungu. Hilo laweza kumfanya awe na maoni mabaya juu ya mtoto. Huenda akamwonyesha maoni ya ubaridi, au badala yake, huenda akampenda mtoto sana lakini asimwangalie sana mke wake. Kunatokea hasara kubwa wakati mume au mke anapokosa usawa.

26. Ni jambo gani linaloweza kufanywa ili mtoto mkubwa asione wivu wakati inapokuwa lazima mama atumie wakati wake mwingi akikiangalia kitoto kichanga?

26 Bado huenda likatokea tatizo jingine wakati mtoto mwingine anapozaliwa na bado kuna mtoto mkubwa kidogo. Inampasa mama atumie wakati wake mwingi sana akiwa pamoja na kitoto kichanga ambacho kimezaliwa sasa. Ili mtoto yule wa kwanza asijione kuwa ametupiliwa mbali na kuona wivu, huenda baba akamwangalia zaidi huyo mkubwa.

27. Wakati mmoja wa wenzi waliooana si mwamini, watoto wanaweza kusaidiwaje kiroho?

27 Bila shaka ni afadhali kuwa wawili kuliko mmoja, lakini afadhali mmoja kuliko bila. Huenda ikawa kwamba kwa sababu ya hali fulani, mama ndiye anayepaswa kulea watoto pasipo msaada wa baba. Au, huenda baba ndiye akapatwa na tatizo ilo hilo. Mara nyingi jamaa zinagawanyika kwa sababu ya dini, hata ikawa kwamba mzazi mmoja, akiwa mtumishi wa Yehova Mungu, ndiye anayeamini sana shauri la Biblia, na mzazi mwingine haamini. Ikiwa Mkristo aliyejiweka wakf ndiye mume, yeye, akiwa kichwa cha jamaa, anayo mamlaka zaidi ya kuonyesha njia inayopaswa kufuatwa katika kulea na kutia watoto adabu. Hata hivyo, huenda akahitajhva kuonyesha uvumilivu mkuu, kujiweza na ustahimilivu; imempasa awe imara kunapokuwa na jambo zito sana, lakini akiwa mwenye kiasi na fadhili hata akikasirishwa, tena awe mwepesi wa kugeuka wakati wo wote hali zinaporuhusu kufanya hivyo. Ikiwa anayeamini ni mke, na hivyo yuko chini ya mume, namna anavyotenda mambo itategemea sana maoni ya mume wake. Je! mume huyo hapendezwi tu na Biblia, au anapinga imani ambazo mke wake anafuata na jitihada zake za kufundisha watoto imani hizo? Ikiwa anampinga, inampasa mke afuate mwendo ambao mtume alieleza: Huenda mume ‘akavutwa pasipo lile Neno’ kwa kuona mke anatimiza kazi zake vizuri na kuwa na maoni yenye heshima. Vilevile atatumia nafasi alizo nazo awafundishe watoto wake kanuni za Biblia.—1 Petro 3:1-4.

MAZINGIRA (HALI) YA NYUMBANI

28, 29. Ni mazingira (hali) gani ya nyumbani yanayotamanika, na kwa sababu gani?

28 Daraka la wazazi wote wawili ni kusitawisha hali ya upendo katika nyumba. Hali hiyo ikionwa na watoto, mashaka au makosa yao hayatajaa mioyo yao kwa sababu ya kuogopa kuwaambia wazazi wao. Wanajua kwamba wanaweza kuwaambia wazazi habari yao wapate kufahamika, na ya kwamba magumu yao yatamalizwa kwa upendo. (Linganisha 1 Yohana 4: 17-19; Waebrania 4:15, 16) Nyumba haitakuwa kibanda tu cha kuishi, bali vilevile mahali penye salama. Upendo wa wazazi utasaidia watoto wazidi kuchangamka na kusitawi.

29 Huwezi kutia sifongo (yavuyavu) katika siki (vinaigre) uitazamie kujaa maji. Inaweza kunywa tu maji yanayoizunguka. Sifongo itakunywa maji ikichovywa ndani yake tu. Vilevile, watoto wanachukua hali zinazowazunguka. Wanazifahamu nia na kuyatazama mambo yanayotendeka karibu nao, nao wanayachukua hayo kama vile sifongo zinavyokunywa maji. Watoto wanafahamu maoni yenu, kwamba hayo ni wasiwasi ama ni hali zenye starehe na utulivu. Hata vitoto vichanga vinachukua sifa za hali iliyo nyumbani, hivyo hali ya imani, ya upendo, ya kiroho na ya kumtegemea Yehova Mungu ni bora sana.

30. Ni maulizo gani ambayo wazazi wanaweza kujiuliza ili wajue kama wanatolea watoto wao uongozi mzuri?

30 Jiulize mwenyewe: Unawatazamia watoto wako watimize kanuni gani? Je! ninyi wazazi wote wawili mnazitimiza? Jamaa yenu inatetea nini? Ninyi ni mifano ya namna gani kwa watoto? Je! mnanung’unikiana, mnatafutiana makosa, mnalaumu wengine, mnaendelea na mawazo yasiyofaa? Je! hivyo ndivyo mnavyotaka watoto wenu wawe? Au, mnawekea jamaa yenu kanuni bora, mkizifuata, na kuwatazamia watoto wenu vilevile wazifuate? Je! wanafahamu kwamba kuwa sehemu ya jamaa hiyo ni lazima matakwa fulani yatimizwe, mwenendo fulani unakubalika, na matendo na maoni fulani hayakubaliki? Watoto wanataka waone usalama wa kuwa sehemu ya jamaa, basi acheni waone idhini (ruhusa) na kibali yenu wakati wanapotimiza kanuni za jamaa. Watu wana njia ya kufuata mambo wanayotazamiwa wafuate. Ukimwona mtoto wako kuwa mbaya, labda atakuwa hivyo. Ukitazamia mema kutoka kwake, utamtia moyo afanye mema.

31. Ni nini kinachopaswa sikuzote kitie nguvu uongozi wa wazazi?

31 Watu wanalaumiwa kwa matendo yao kuliko kwa maneno yao. Vilevile, huenda watoto wasiangalie sana maneno kama wanavyofanya kwa matendo, na mara nyingi wako macho kuchunguza unafiki (udanganyifu) wo wote. Maneno mengi mno yanaweza kutatiza (kuchafua akili) watoto. Hakikisheni kwamba maneno yenu yanatiwa nguvu kwa kutimiza mnayosema.—1 Yohana 3:18.

32. Ni shauri la nani linalopaswa lifuatwe nyakati zote?

32 Kwamba wewe ni baba au mama, daraka lako ni gumu. Lakini daraka gumu laweza kutimizwa kwa matokeo yenye furaha ikiwa unalifuata shauri la Mpaji wa uzima. Litimize kwa uaminifu daraka lako ulilopewa, kana kwamba unamtumikia Yeye. (Wakolosai 3: 17) Epuka kufanya mambo kupita kiasi, tunza usawa wako na ‘kukiacha kiasi chako kijulikane kwa wote,’ kutia na watoto wako.—Wafilipi 4:5, NW.

[Picha katika ukurasa wa 100]

Mtazamo wa mama na mguso na hali ya sauti yake, humbambia mtoto hivi, “Nakupenda wewe.”

[Picha katika ukurasa wa 104]

Je, unapanga uwe na tafrija pamoja na watoto wako?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki