Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g 12/15 uku. 16
  • Uwezo wa Mwili wa Mwanadamu wa Kujiponya

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Uwezo wa Mwili wa Mwanadamu wa Kujiponya
  • Amkeni!—2015
  • Habari Zinazolingana
  • Daktari wa Upasuaji Anaeleza Kwa Nini Anamwamini Mungu
    Amkeni!—2014
  • Maradhi ya Moyo—Tisho kwa Uhai
    Amkeni!—1996
  • Upendo wa Kikristo Kati ya Misiba Katika Mexico
    Amkeni!—1996
  • Ni Umajimaji Gani Ulio na Thamani Kubwa Zaidi?
    Amkeni!—2006
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2015
g 12/15 uku. 16
Mchoro wa chembe za damu

JE, NI KAZI YA UBUNI?

Uwezo wa Mwili wa Mwanadamu wa Kujiponya

Bendeji mkononi

MIONGONI mwa mifumo inayomwezesha mwanadamu kuendeleza uhai ni uwezo wa mwili wa kuponya majeraha na kuzalisha upya tishu zilizoharibika. Jambo hilo huanza punde tu mwili unapopata jeraha.

Fikiria hili: Uwezo huo wa kujitibu hutegemea matukio yanayofuatana ya utendaji tata wa chembe:

  • Vigandisha damu hujishikiza kwenye tishu katika eneo la jeraha, kisha kufanya damu igande na kufunika mishipa ya damu iliyokuwa imejeruhiwa.

  • Eneo lililoathiriwa huvimba ili kuzuia maambukizo kupitia kidonda na kuondoa uchafu wowote uliosababishwa na jeraha.

  • Baada ya siku kadhaa, mwili huanza kuzalisha chembe mpya, hivyo kidonda kinafunga na mishipa kujirekebisha.

  • Hatimaye, tishu zinazotengeneza kovu huparekebisha na kupaimarisha mahali penye jeraha.

Uwezo wa damu kuganda umewachochea watafiti kutengeneza aina ya plastiki inayojirekebisha. Plastiki hizo zimefanyizwa na mirija midogo iliyo na kemikali mbili ambazo huvuja plastiki inapopasuka. Kemikali hizo zinapochanganyika, hutokeza umajimaji fulani ambao husambaa katika eneo lote lililoharibika na kufunika nyufa na mashimo. Umajimaji huo unapogandamana, eneo hilo huwa gumu na hivyo kurejesha hali ya awali ya plastiki hiyo. Mtafiti fulani anakiri kwamba mfumo huo wa kujirekebisha wa vitu visivyo hai unaoendelea kutengenezwa umebuniwa kwa kuiga uwezo wa kujirekebisha wa viumbe hai.

Una maoni gani? Je, uwezo wa mwili wa kujiponya ulijitokeza wenyewe? Au ulibuniwa?

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki