Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • g17 Na. 4 kur. 10-11
  • Watoto Wanapoondoka Nyumbani

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Watoto Wanapoondoka Nyumbani
  • Amkeni!—2017
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHANGAMOTO
  • CHANZO CHA HALI HIYO
  • MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jinsi ya Kuepuka “Talaka ya Uzeeni”
    Msaada kwa Ajili ya Familia
  • Wazazi—Wafundisheni Watoto Wenu Kumpenda Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • “Ndoa na Iheshimiwe”
    “Jitunzeni Katika Upendo wa Mungu”
Pata Habari Zaidi
Amkeni!—2017
g17 Na. 4 kur. 10-11
Mwanamume akitazama televisheni wakati mke wake anafuma vitambaa

MSAADA KWA AJILI YA FAMILIA | NDOA

Watoto Wanapoondoka Nyumbani

CHANGAMOTO

Wenzi wa ndoa hukabili changamoto kubwa zaidi watoto wanapokuwa watu wazima na kuondoka nyumbani. Nyumba inapokuwa haina watoto, wenzi wa ndoa huhisi kana kwamba hawafahamiani. Mshauri wa masuala ya familia M. Gary Neuman aliandika hivi: “Watu wengi ninaowashauri ni wale ambao hawajui jinsi ya kurudisha uhusiano wa karibu kati yao na wenzi wao wa ndoa. Watoto wanapoondoka, [wazazi] wanakuwa na mambo machache ya kusimuliana au kuzungumzia.”a

Je, kwa njia fulani mambo hayo yanafunua hali ilivyo katika ndoa yako? Ikiwa ndivyo, unaweza kuboresha mahusiano yenu. Kwanza kabisa, fikiria sababu ambazo huenda zimechangia hali ya kutokuwa na ukaribu kati yako na mwezi wako wa ndoa.

CHANZO CHA HALI HIYO

Kwa miaka mingi watoto walichukua nafasi ya kwanza. Wakiwa na nia nzuri kabisa, wazazi wengi hutanguliza mahitaji ya watoto kuliko mahitaji ya ndoa yao. Matokeo ni kwamba, wanazoea kutimiza majukumu yao ya kuwa baba na mama na hivyo kudhoofisha uhusiano wao wakiwa mume na mke, jambo ambalo huonekana wazi mara tu watoto wanapoondoka nyumbani. Mwanamke fulani aliyeolewa mwenye umri wa miaka 59 anasema hivi: “Watoto walipokuwepo, angalau tulifanya mambo pamoja.” Lakini anakiri kwamba, baada ya wototo kuondoka “kila mtu alianza kufuatilia mambo yake.” Wakati fulani hata alimwambia mume wake hivi: “Unaingilia mambo yangu.”

Baadhi ya wenzi wa ndoa hawajajiandaa kukabili hali hiyo mpya maishani. Kitabu Empty Nesting kinasema hivi: “Kwa wenzi wengi wa ndoa, hali hubadilika na kuwa kana kwamba wameingia katika ndoa mpya.” Kwa sababu wanahisi wana mambo machache sana ya kufanya pamoja, waume wengi na wake huamua kila mtu ajitenge na kufuatilia mambo yake, na hivyo badala ya kuwa wenzi wa ndoa wanakuwa tu kama watu wanaoishi nyumba moja.

Habari njema ni kwamba, unaweza kukwepa madhara hayo, na hata kufurahia maisha yenu mapya. Biblia inaweza kukusaidia. Acheni tuone jinsi inavyoweza kufanya hivyo.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Azimia kukubali mabadiliko. Biblia inasema hivi kuhusu watoto ambao tayari ni watu wazima: “Mwanamume atamwacha baba yake na mama yake.” (Mwanzo 2:24) Mkiwa wazazi, lengo lenu lilikuwa kuwafundisha watoto na kuwasaidia wasitawishe ustadi ambao watahitaji kuutumia watakapokuwa watu wazima. Kwa msingi huo, kuondoka kwa watoto nyumbani ni jambo mnalopaswa kujivunia.—Kanuni ya Biblia: Marko 10:7.

Bila shaka, bado utaendelea kuwa mzazi kwa watoto wako. Hata hivyo, badala ya kuwa msimamizi wewe sasa ni mshauri. Uhusiano huo mpya unakuwezesha kudumisha ukaribu na watoto wako, na wakati huohuo kutanguliza mahitaji ya mwenzi wako wa ndoa.b—Kanuni ya Biblia: Mathayo 19:6.

Eleza hisia zako. Mweleze mwenzi wako jinsi mabadiliko hayo ya maisha yanavyokuathiri, na uwe tayari kusikiliza hisia zake pia. Jitahidi kuelewa na uwe mwenye subira. Huenda ikachukua muda kuimarisha uhusiano wenu kama mume na mke, lakini jitahada hizo zina matokeo mazuri.—Kanuni ya Biblia: 1 Wakorintho 13:4.

Tafuteni mambo mapya mnayoweza kufanya pamoja. Zungumzieni kuhusu malengo ambayo mngependa kutimiza pamoja au mambo ambayo mngependa kufurahia mkiwa wenzi wa ndoa. Kwa sababu ya kulea watoto, mmepata hekima nyingi ya jinsi ya kushughulika na maisha. Kwa nini msiitumie kuwasaidia wengine?—Kanuni ya Biblia: Ayubu 12:12.

Azimieni upya kuimarisha uhusiano wenu. Fikiria kuhusu sifa za mwenzi wako zilizokuvutia. Vilevile, fikirieni kuhusu historia yenu na changamoto mlizofanikiwa kushinda mkiwa pamoja. Hatimaye, mtaweza kufurahia maisha yenu mapya. Kwa kweli, kwa jitihada za pamoja sasa mna fursa ya kuboresha hali ya ndoa yenu na kurudisha upendo wenu wa mwanzoni.

a Kutoka katika kitabu Emotional Infidelity.

b Ikiwa bado unalea watoto kumbuka kwamba wewe na mwenzi wako wa ndoa ni “mwili mmoja.” (Marko 10:8) Watoto huhisi wakiwa salama iwapo uhusiano kati ya wazazi wao ni imara.

MAANDIKO MUHIMU

  • “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake.”—Marko 10:7.

  • “Kile ambacho Mungu ameunganisha mtu yeyote asikitenganishe.” —Mathayo 19:6.

  • “Upendo ni wenye ustahimilivu na wenye fadhili.”—1 Wakorintho 13:4.

  • “Je, hekima haimo katikati ya wazee?”—Ayubu 12:12.

Salvatore na Aurora

SALVATORE NA AURORA

“Tuligundua kwamba tuna muda mwingi zaidi na tunahitaji kuutumia vizuri. Kwa hiyo tukaamua kutumia muda wetu na watu wengine, kama vile wenzi walio na watoto au wapya katika ndoa. Tunapenda kuwasaidia wengine na kuwaeleza mambo ambayo tumejionea katika maisha yetu.”

Carlo na Caterina

CARLO NA CATERINA

“Ilichukua muda kukubali wazo la kwamba maisha yetu yamebadilika. Kwa miaka mingi tulizungumzia hasa kuhusu watoto. Sasa, tunapofanya mambo kwa pamoja, hatua kwa hatua tumeanza kuzoea kujieleza na kuzungumzia mambo tunayofurahia.”

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki