Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • rr kur. 26-27
  • Ezekieli—Maisha na Nyakati Zake

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Ezekieli—Maisha na Nyakati Zake
  • Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • MANABII WA NYAKATI ZAKE
  • Yerusalemu Laharibiwa
    Masomo Unayoweza Kujifunza Katika Biblia
  • Kutumikia Katika “Siku za Mwisho”
    Mungu Asema Nasi Kupitia Yeremia
  • Yehova—Anapenda Haki
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1977
  • Kufumbua Fumbo la Ule Mti Mkubwa
    Sikiliza Unabii wa Danieli!
Pata Habari Zaidi
Hatimaye Ibada Safi ya Yehova Yarudishwa!
rr kur. 26-27

SANDUKU LA KUFUNDISHIA LA 2B

Ezekieli​—Maisha na Nyakati Zake

Makala Iliyochapishwa

Jina Ezekieli linamaanisha “Mungu Huimarisha.” Ingawa unabii anaotoa una maonyo mengi, ujumbe wake kwa ujumla unapatana na maana ya jina lake na unaimarisha imani ya watu wanaotaka kumtolea Mungu ibada safi.

Ezekieli.

MANABII WA NYAKATI ZAKE

  • Yeremia.

    YEREMIA,

    alitoka katika familia ya kikuhani, alitumikia hasa Yerusalemu (647 hadi 580 K.W.K)

  • Hulda.

    HULDA

    alitumikia wakati kitabu cha Sheria kilipopatikana hekaluni karibu mwaka wa 642 K.W.K.

  • Danieli.

    DANIELI,

    alitoka katika kabila la kifalme la Yuda, alipelekwa Babiloni mwaka wa 617 K.W.K.

  • Habakuki.

    HABAKUKI

    huenda alitumikia Yuda mwanzoni mwa utawala wa Yehoyakimu

  • Obadia.

    OBADIA

    alitoa unabii dhidi ya Edomu, huenda wakati wa kuharibiwa kwa Yerusalemu

WALITABIRI LINI? (TAREHE ZOTE NI K.W.K.)

Mfuatano wa matukio unaoonyesha manabii wengine wakati wa Ezekieli (tarehe zote ni K.W.K). Yeremia: kuanzia 647 hadi 580 hivi; Hulda: 642 hivi; Danieli: kuanzia 617 hadi 537 hivi, Habakuki: 625 hivi; Ezekieli: kuanzia 613 hadi 591 hivi; Obadia: 607 hivi.

MATUKIO MUHIMU KATIKA MAISHA YA EZEKIELI (TAREHE ZOTE NI K.W.K.)

  1. Karibu 643: Azaliwa

  2. 617: Achukuliwa mateka kwenda Babiloni

  3. 613: Aanza kutabiri; aona maono ya Yehova

  4. 612: Aona maono ya uasi hekaluni

  5. 611: Aanza kushutumu Yerusalemu

  6. 609: Mke wake afa na Yerusalemu laanza kuzingirwa kwa mara ya mwisho

  7. 607: Apokea uhakikisho kwamba Yerusalemu limeharibiwa

  8. 593: Aona maono ya hekalu

  9. 591: Atabiri kwamba Nebukadneza atavamia Misri; akamilisha maandishi yake

WAFALME WA YUDA NA BABILONI

  1. 659-629: Yosia atetea ibada safi lakini anakufa vitani akipigana na Farao Neko

  2. 628: Yehoahazi atawala vibaya kwa miezi mitatu naye atekwa na Farao Neko

  3. 628-618: Yehoyakimu ni mfalme mbaya na Farao Neko anamfanya kuwa kibaraka

  4. 625: Nebukadneza ashinda jeshi la Wamisri

  5. 620: Nebukadneza avamia Yuda kwa mara ya kwanza na kumfanya Yehoyakimu kuwa kibaraka wake huko Yerusalemu

  6. 618: Yehoyakimu amwasi Nebukadneza lakini huenda anakufa Wababiloni wanapovamia Nchi ya Ahadi kwa mara ya pili.

  7. 617: Yehoyakini, anayeitwa pia Yekonia, ni mfalme mbaya anayetawala kwa miezi mitatu, kisha anajisalimisha kwa Nebukadneza

  8. 617-607: Mfalme mwovu na mwoga Sedekia, afanywa kuwa kibaraka na Nebukadneza

  9. 609: Sedekia anamwasi Nebukadneza, ambaye anavamia tena Yuda kwa mara ya tatu

  10. 607: Nebukadneza aharibu Yerusalemu, amkamata Sedekia, ampofusha, na kumpeleka Babiloni

Angalia sura ya 2, fungu la 28, 29

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki