Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • lff somo la 9
  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Mkaribie Mungu Kupitia Sala
  • Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • CHIMBA ZAIDI
  • MUHTASARI
  • CHUNGUZA ZAIDI
  • Zawadi ya Sala
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Kumkaribia Mungu Katika Sala
    Mungu Anataka Tufanye Nini?
  • Mkaribie Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Nini Hasa?
  • Namna ya Kupata Msaada kwa Sala
    Unaweza Kuishi Milele Katika Paradiso Duniani
Pata Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Masomo ya Kujifunza Biblia
lff somo la 9
Somo la 9. Mwanamke akisali.

SOMO LA 09

Mkaribie Mungu Kupitia Sala

Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa
Makala Iliyochapishwa

Je, wakati mwingine wewe unahisi kwamba unahitaji mwongozo maishani? Je, kuna maswali muhimu ambayo ungependa kupata majibu? Je, unahitaji kufarijiwa au kutiwa moyo? Je, ungependa kuhisi ukiwa karibu zaidi na Yehova? Sala inaweza kukusaidia katika hali hizo zote. Lakini tunapaswa kusali kwa njia gani? Je, Mungu husikiliza sala zote? Unaweza kufanya nini ili uwe na uhakika kwamba atasikiliza sala zako? Acha tuone.

1. Tunapaswa kusali kwa nani, na tunaweza kusali kuhusu nini?

Yesu alifundisha kwamba tunapaswa kusali tu kwa Baba yetu wa mbinguni. Yesu mwenyewe alisali kwa Yehova. Alisema: “Basi, salini hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni . . . ’” (Mathayo 6:9) Tunaposali kwa Yehova, tunaimarisha urafiki wetu pamoja naye.

Tunaweza kusali kuhusu jambo lolote. Bila shaka, ili Mungu ajibu sala zetu, zinapaswa kupatana na mapenzi yake. “Tukiomba chochote kulingana na mapenzi [ya Mungu], yeye hutusikia.” (1 Yohana 5:14) Yesu alitoa mfano wa mambo tunayoweza kutaja katika sala zetu. (Soma Mathayo 6:9-13.) Tunaweza kusali kuhusu mahangaiko yetu bila kusahau kumshukuru Mungu kwa mambo ambayo ametufanyia na pia kumwomba awasaidie wengine.

2. Tunapaswa kusali jinsi gani?

Biblia inatutia moyo ‘tumwage mioyo yetu mbele za Mungu.’ (Zaburi 62:8) Basi tunapaswa kusali kwa unyoofu na kutoka moyoni. Tunaweza kusali kwa sauti au kimyakimya tukiwa tumekaa kwa njia yoyote inayoonyesha kwamba tunamheshimu Yehova. Tunaweza kusali wakati wowote na mahali popote.

3. Mungu hujibu sala zetu jinsi gani?

Yeye hujibu kwa njia mbalimbali. Yehova ametupatia Neno lake, Biblia, ambalo linajibu maswali yetu. Kusoma Neno la Mungu kunaweza “[kumfanya] asiye na uzoefu awe na hekima.” (Zaburi 19:7; soma Yakobo 1:5.) Yehova anaweza kutusaidia kupata amani ya akili tunapokabili matatizo. Na anaweza kuwatumia watumishi wake kutusaidia tunapokuwa na uhitaji.

CHIMBA ZAIDI

Chunguza jinsi unavyoweza kusali kutoka moyoni kwa njia inayompendeza Mungu, na uone jinsi sala inavyoweza kukusaidia.

4. Mungu ameweka viwango tunavyopaswa kufuata kuhusu sala

Ni mambo gani yanayoamua ikiwa Mungu atasikiliza au hatasikiliza sala zetu? Onyesha VIDEO.

VIDEO: Je, Mungu Husikiliza Sala Zote?​—Kisehemu (2:42)

Yehova anataka tusali kwake. Soma Zaburi 65:2, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Je, unafikiri “Msikiaji wa sala” anataka wewe usali kwake? Kwa nini?

Tunapaswa kujitahidi kuishi kulingana na viwango vya Mungu ili asikilize sala zetu. Soma Mika 3:4 na 1 Petro 3:12, kisha mzungumzie swali hili:

  • Tunaweza kufanya nini ili tuwe na hakika kwamba Yehova atasikiliza sala zetu?

Wakati wa vita, pande zote husali ili kupata ushindi. Je, tunaweza kutazamia Mungu ajibu sala hizo?

5. Tunapaswa kusali kutoka moyoni

Watu fulani wamefundishwa kusali kwa kukariri maneno yaleyale. Lakini je, hivyo ndivyo Mungu anataka tusali kwake? Soma Mathayo 6:7, kisha mzungumzie swali hili:

  • Unawezaje kuepuka kusema “mambo yaleyale tena na tena” katika sala zako?

Kila siku, unaweza kufikiria kuhusu baraka fulani hususa katika maisha yako kisha umshukuru Yehova kwa baraka hiyo. Ukifanya hivyo kila siku kwa juma moja, utasali kuhusu mambo saba tofauti bila kurudia jambo lilelile.

Mvulana akizungumza na wazazi wake.

Baba mzuri angependa mtoto wake azungumze naye kutoka moyoni. Vivyo hivyo, Yehova anataka tusali kwake kutoka moyoni

6. Sala ni zawadi kutoka kwa Mungu

Sala inaweza kutusaidiaje hasa tunapokabili matatizo maishani? Onyesha VIDEO.

VIDEO: Sala Hutusaidia Kukabiliana na Matatizo (1:32)

Biblia inatuahidi kwamba sala inaweza kutusaidia kupata amani ya akili. Soma Wafilipi 4:6, 7, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Ingawa wakati fulani matatizo yetu hayaondoki tunaposali, sala inaweza kutusaidiaje?

  • Wewe ungependa kusali kuhusu mambo gani?

Je, wajua?

Neno “amina” linamaanisha “na iwe hivyo” au “bila shaka.” Tangu nyakati za Biblia, watu husema “amina” mwishoni mwa sala.​—1 Mambo ya Nyakati 16:36.

7. Tenga wakati wa kusali

Wakati mwingine huenda tukawa na shughuli nyingi sana hivi kwamba tukasahau kusali. Ni nini kinachoonyesha kwamba Yesu aliona sala kuwa jambo muhimu sana? Soma Mathayo 14:23 na Marko 1:35, kisha mzungumzie maswali haya:

  • Yesu alifanya nini ili kupata muda wa kusali?

  • Unaweza kufanya nini ili upate muda wa kusali?

Picha: Mwanamke akisali pindi mbalimbali. 1. Asubuhi. 2. Pamoja na watoto wake. 3. Kazini. 4. Kabla ya kula chakula.

WATU FULANI HUSEMA: “Sala ni njia ya kukusaidia tu ujihisi vizuri, hakuna anayesikiliza.”

  • Wewe una maoni gani?

MUHTASARI

Tunaposali kutoka moyoni tunahisi tukiwa karibu zaidi na Mungu, tunapata amani ya akili, na nguvu tunazohitaji ili kumpendeza Yehova.

Ungejibuje?

  • Tunapaswa kusali kwa nani?

  • Tunapaswa kusali jinsi gani?

  • Tunanufaikaje tunaposali?

Lengo

CHUNGUZA ZAIDI

Pata majibu ya maswali ambayo watu wengi hujiuliza kuhusu sala.

“Mambo Saba Unayohitaji Kujua Kuhusu Sala” (Mnara wa Mlinzi, Oktoba 1, 2010)

Jifunze kwa nini ni muhimu kusali na jinsi unavyoweza kuboresha sala zako.

“Kwa Nini Ninapaswa Kusali?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Chunguza uone Biblia inafundisha tunapaswa kusali kwa nani.

“Je, Ni Sawa Kusali kwa Watakatifu?” (Makala iliyo kwenye mtandao)

Katika video hii ya muziki, ona ikiwa tunaweza kusali mahali popote au wakati wowote.

Sali Wakati Wowote (1:22)

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki