Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w09 7/1 uku. 9
  • “Mimi Yehova Mungu Wenu Ni Mtakatifu”

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Mimi Yehova Mungu Wenu Ni Mtakatifu”
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Habari Zinazolingana
  • “Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, Ni Bwana”
    Mkaribie Yehova
  • “Lazima Muwe Watakatifu”
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2021
  • Lazima Mwe Watakatifu Kwa Sababu Yehova Ni Mtakatifu
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Inamaanisha Nini Kuwa Mtakatifu?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
w09 7/1 uku. 9

Mkaribie Mungu

“Mimi Yehova Mungu Wenu Ni Mtakatifu”

Mambo ya Walawi Sura ya 19

“MTAKATIFU, mtakatifu, mtakatifu ni Yehova Mungu.” (Ufunuo 4:8) Kwa maneno hayo, Biblia inaonyesha kwamba Yehova ni mtakatifu, yaani, ana utakatifu na usafi wa hali ya juu zaidi. Mungu hawezi kamwe kutenda dhambi; hawezi kuchafuliwa au kupotoshwa na dhambi kwa njia yoyote ile. Je, hilo linamaanisha kwamba hakuna tumaini kwa wanadamu wasio wakamilifu kuwa na uhusiano mzuri pamoja na Mungu ambaye ni mtakatifu zaidi? Hapana! Acheni tuchunguze maneno yatakayotupa tumaini yaliyo kwenye Mambo ya Walawi sura ya 19.

Yehova alimwambia Musa hivi: “Sema na kusanyiko lote la wana wa Israeli.” Maneno yanayofuata yalimhusu kila mtu katika taifa hilo. Musa angewaambia nini? Mungu aliendelea kusema hivi: “Utawaambia, ‘Muwe watakatifu, kwa sababu mimi Yehova Mungu wenu ni mtakatifu.’” (Mstari wa 2) Kila Mwisraeli alipaswa kuonyesha utakatifu. Maneno “muwe watakatifu” yanaonyesha kwamba hilo halikuwa pendekezo, ilikuwa amri. Je, Mungu alikuwa akiwatazamia wafanye jambo lisilowezekana?

Ona kwamba Yehova alitaja utakatifu wake mwenyewe, si kama kiwango kilichopaswa kufikiwa, bali kama sababu iliyofanya amri hiyo itolewe. Kwa maneno mengine, Yehova hakuwaambia waabudu wake wasio wakamilifu katika Israeli wawe watakatifu kama alivyo. Hilo halingewezekana. Yehova, “Aliye Mtakatifu Zaidi,” ni mkuu zaidi kuliko wengine wote katika utakatifu. (Methali 30:3) Hata hivyo, kwa kuwa Yehova ni mtakatifu, anawatazamia waabudu wake wawe watakatifu, yaani, kwa kadiri inavyowezekana kwa wanadamu wasio wakamilifu. Wanaweza kujionyesha wenyewe kuwa watakatifu katika njia gani?

Baada ya kutoa amri ya kuwa watakatifu, Yehova kupitia Musa alitoa matakwa yaliyohusu kila sehemu ya maisha. Kila Mwisraeli alitazamiwa kutii viwango vya mwenendo kama vifuatavyo: kuwaheshimu inavyofaa wazazi na waliozeeka (mistari 3, 32); kuwaheshimu viziwi, vipofu, na watu wengine wanaoteseka (mistari 9, 10, 14); kuwa wanyoofu na kutokuwa na upendeleo wanaposhughulika na wengine (mistari 11-13, 15, 35, 36); na mtu kumpenda mwabudu mwenzake kama anavyojipenda mwenyewe. (Mstari 18) Kwa kutii viwango hivyo na vingine vilivyotajwa, Mwisraeli angejionyesha ‘kuwa mtakatifu kwa Mungu’ wake.—Hesabu 15:40.

Amri kuhusu utakatifu inatusaidia kuelewa kwa undani mawazo na njia za Yehova Mungu. Kwanza kabisa, tunajifunza kwamba ili tuwe na uhusiano wa karibu pamoja naye, tunahitaji kujitahidi kabisa kuishi kulingana na viwango vyake vya mwenendo mtakatifu. (1 Petro 1:15, 16) Kwa kutii viwango hivyo, tunaweza kufurahia njia bora zaidi ya maisha.—Isaya 48:17.

Pia, amri ya kuwa watakatifu inaonyesha kwamba Yehova anawaamini waabudu wake. Yehova hatutazamii kamwe tufanye mambo yanayopita uwezo wetu. (Zaburi 103:13, 14) Anajua kwamba sisi wanadamu ambao tumeumbwa kwa mfano wake, tuna uwezo wa kusitawisha utakatifu kwa kiasi fulani. (Mwanzo 1:26) Je, unachochewa kujifunza mengi kuhusu jinsi unavyoweza kumkaribia zaidi Mungu mtakatifu, Yehova?

[Picha katika ukurasa wa 9]

Tuna uwezo wa kusitawisha utakatifu

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki