Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 5/1 uku. 22
  • Epuka Marafiki Wabaya!

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Epuka Marafiki Wabaya!
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Uharibifu wa Sodoma na Gomora
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Yesu Ashinda Vishawishi
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2009
  • Yesu Anawaponya Watu Kimuujiza
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Yesu Awashangaza Wasikilizaji Wake
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 5/1 uku. 22

Kwa Ajili ya Vijana

Epuka Marafiki Wabaya!

Maagizo: Fanya zoezi hili katika mazingira matulivu. Unaposoma maandiko, jiwazie ukiwa katika matukio yanayozungumziwa. Wazia kikao. Sikia sauti. Hisi kama wahusika wakuu wanavyohisi. Wazia kwamba masimulizi haya ni halisi kabisa.

Wahusika wakuu: Dina, Shekemu, Yakobo, Simeoni, na Lawi

Muhtasari: Dina ananajisiwa na Shekemu, na ndugu zake wenye hasira wanalipiza kisasi.

1 CHUNGUZA TUKIO HILI.—SOMA MWANZO 34:1-31.

Unafikiri Dina alijihusisha na mambo gani akiwa na rafiki zake huko Kanaani?

․․․․․

Unafikiri ni maneno gani yenye ‘kushawishi’ ambayo Shekemu aliendelea kumwambia Dina?

․․․․․

Unatambua hisia gani wakati Yakobo anapowakemea Simeoni na Lawi katika mstari wa 30?

․․․․․

2 CHIMBA ZAIDI.

Unafikiri ni kwa nini Dina aliwatembelea mabinti wa Kanaani kwa ukawaida? (Kwa mfano, walishirikiana katika mambo gani? Alipata vitu gani miongoni mwa Wakanaani ambavyo hangeweza kupata kwao nyumbani?)

․․․․․

Ni sifa gani zenye kuvutia za Shekemu ambazo huenda Dina aliona? (Soma tena mstari wa 3, 12, na 19.)

․․․․․

Biblia inaonyeshaje kwamba Dina hakutaka kufanya ngono na Shekemu? (Soma tena mstari wa 2.)

․․․․․

Unafikiri ilikuwa sawa kwa Simeoni na Lawi kulipiza kisasi kwa kuwauwa wanaume wa jiji la Shekemu? Kwa nini?

․․․․․

3 TUMIA MAMBO ULIYOJIFUNZA. ANDIKA MAMBO ULIYOJIFUNZA KUHUSU . . .

Umuhimu wa kuchagua rafiki zako kwa busara.

․․․․․

Umuhimu wa kujizuia, hata kama una sababu nzuri ya kukasirika.

․․․․․

NJIA NYINGINE UNAYOWEZA KUTUMIA HABARI HIYO.

Unaweza kufanya nini ili kuepuka kutumiwa vibaya kingono na watu ambao hawathamini viwango vya Mungu vya maadili?

․․․․․

4 NI MAMBO GANI KATIKA SIMULIZI HILI AMBAYO YAMEKUGUSA MOYO SANA, NA KWA NINI?

․․․․․

Ikiwa huna Biblia, waombe Mashahidi wa Yehova wakupe moja, au soma habari zaidi katika Intaneti www.watchtower.org

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki