Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w11 10/1 uku. 6
  • 3 Mungu Analipiza Kisasi—Je, Ni Kweli?

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • 3 Mungu Analipiza Kisasi—Je, Ni Kweli?
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari Zinazolingana
  • Je, Mungu Atahukumu Watu kwa Moto wa Mateso?
    Je, Mungu Atahukumu Watu kwa Moto wa Mateso?
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Misiba ya Asili?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Je, Misiba ya Asili Ni Adhabu Kutoka Kwa Mungu?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2008
  • Je, Mungu Anatumia Misiba ya Asili Kuwaadhibu Wanadamu Leo?
    Amkeni!—2012
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 10/1 uku. 6

3 Mungu Analipiza Kisasi​—Je, Ni Kweli?

Mambo ambayo huenda umesikia: “Mungu anaweka rekodi ya dhambi zote ambazo wanadamu wanafanya, naye hulipiza kisasi kwa kuwaadhibu milele katika moto wa mateso.”

“Mungu anatumia misiba ya asili kuwaadhibu watenda dhambi.”

Biblia inafundisha nini?: Andiko la 2 Petro 3:9 linasema kwamba Yehova “hataki yeyote aangamizwe bali hutaka wote wafikie toba.” Badala ya kukazia fikira makosa yetu, yeye anakazia fikira sifa zetu nzuri. “Macho [ya Mungu] yanaenda huku na huku duniani kote ili aonyeshe nguvu zake kwa ajili ya wale ambao moyo wao ni mkamilifu kumwelekea yeye.”—2 Mambo ya Nyakati 16:9.

Moto wa mateso si fundisho la Biblia. Hata wazo la kuwatesa waovu milele katika moto linamchukiza Mungu. Adhabu yake kuu kwa waovu ni kifo. (Yeremia 7:31; Waroma 6:7) Mungu hasababishi misiba ya asili ambayo huharibu bila kuchagua. Misiba hiyo ni matukio yasiyotazamiwa yanayoweza kumpata mtu yeyote.—Mhubiri 9:11.

Jinsi kujua ukweli kunavyokusaidia: Tunaweza kumkaribia Mungu zaidi tunapotambua kwamba yuko “tayari kusamehe” na si mwepesi wa kuhukumu. (Zaburi 86:5) Hatupaswi kumtumikia Mungu kwa sababu tunajihisi tuna hatia au tunaogopa sana kuadhibiwa. Badala yake, tunaweza kusitawisha imani yetu tukiwa na nia inayofaa kabisa—kumpenda Yehova. Upendo huo unakuwa kama nguvu inayotuchochea kufanya yote tuwezayo ili kumfurahisha.—Mathayo 22:36-38; 1 Yohana 5:3.

Ingawa Mungu anataka kila mtu abadilike na kufanya mema, anajua kwamba wengi hawatafanya hivyo. Kama hangechukua hatua dhidi ya wale ambao wameamua kufanya mambo mabaya, basi hangekuwa tofauti na mtawala anayetoa sheria bila kuhakikisha kwamba zinafuatwa, na hivyo kuruhusu ukosefu wa haki na kuteseka kuongezeke bila kufanya lolote. (Mhubiri 8:11) Kujua kwamba Mungu hataendelea kuvumilia uovu milele kunafanya tuwe na tumaini lenye nguvu kuhusu wakati ujao. Mungu ameahidi kuondoa wale wanaoendelea kufanya mambo maovu, ili “wapole” wafurahie uzima wa milele duniani kama alivyokusudia mwanzoni.—Zaburi 37:10, 11, 29.a

[Maelezo ya Chini]

a Ili kujifunza mengi zaidi kuhusu jinsi Mungu atakavyofanya dunia kuwa paradiso, ona sura ya 3 na ya 8 ya kitabu Biblia Inafundisha Nini Hasa?

[Blabu katika ukurasa wa 6]

Je, Mungu angetaka tumwabudu kwa sababu tunaogopa kuadhibiwa?

[Hisani ya Picha katika ukurasa wa 6]

Engravings by Doré

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki