Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w13 9/1 uku. 16
  • Majibu ya Maswali ya Biblia

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Majibu ya Maswali ya Biblia
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Habari Zinazolingana
  • Biblia Inasema Nini Kuhusu Ndoa?
    Maswali ya Biblia Yajibiwa
  • Jinsi Familia Yako Inavyoweza Kuwa na Furaha
    Habari Njema Kutoka kwa Mungu!
  • Ilinde Ndoa Yako
    Daftari la Mkutano wa Huduma na Maisha Yetu ya Kikristo—2021
  • Kupata Furaha Katika Zawadi ya Ndoa
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1985
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 9/1 uku. 16
[Picha katika ukurasa wa 16]

Majibu ya Maswali ya Biblia

Ndoa inawezaje kuwa na furaha?

Ushauri wa Biblia kuhusu ndoa ni wenye kutegemeka kwa sababu unatoka kwa Mwanzilishi wa ndoa, Yehova Mungu. Inatufundisha jinsi ya kuwa na sifa zinazoweza kufanya ndoa iwe yenye furaha na inatuonya kuhusu mitazamo inayoweza kuharibu ndoa. Pia, inatufundisha jinsi ya kuwasiliana ili tuzidishe furaha katika ndoa.​—Soma Wakolosai 3:8-10, 12-14.

Mume na mke wanapaswa kuheshimiana. Kila mmoja akitimiza wajibu aliopewa na Mungu, ndoa yao inaweza kuwa na furaha.​—Soma Wakolosai 3:18, 19.

Ni nini kinachofanya ndoa idumu?

Wenzi wa ndoa wanaweza kuishi pamoja ikiwa wanapendana. Mungu anatufundisha jinsi ya kupendana. Yeye na Mwanaye Yesu wameweka mfano bora wa upendo wa kujidhabihu.​—Soma 1 Yohana 4:7, 8, 19.

Mume na mke watafurahia kuishi pamoja ikiwa wataheshimu mpango wa ndoa ulioanzishwa na Mungu. Mungu alianzisha ndoa iwe muungano wa kudumu kati ya mume na mke ili kulinda familia. Ndoa inaweza kudumu kwa sababu Mungu aliumba mume na mke wakamilishane kimwili na kihisia. Pia, aliwaumba kwa mfano wake, wakiwa na uwezo wa kuiga upendo wake.​—Soma Mwanzo 1:27; 2:18, 24.

Kwa habari zaidi ona sura ya 14 ya kitabu hiki, Biblia Inafundisha Nini Hasa?, kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova

Unaweza kukipakua kwenye www.jw.org/sw

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki