Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w14 6/15 kur. 3-6
  • “Lainisha Mapito ya Mguu Wako” Ili Ufanye Maendeleo

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • “Lainisha Mapito ya Mguu Wako” Ili Ufanye Maendeleo
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Vichwa vidogo
  • Habari Zinazolingana
  • TAYARISHA NJIA KWA KUFANYA MAAMUZI MAZURI
  • KUONDOA VIZUIZI NJIANI
  • ENDELEA KUFANYA MAENDELEO YA KIROHO
  • Vijana, Je, Mnatanguliza Malengo ya Kiroho Maishani?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2018
  • Kwa Nini Uichunguze Biblia?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Tunawafurahia Vijana Wanaotembea Katika Njia ya Yehova
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1976
  • Watoto Wenye Furaha Katika Ulimwengu Wenye Upotoe
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1982
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 6/15 kur. 3-6
Njia iliyo na vizuizi vingi

“Lainisha Mapito ya Mguu Wako” Ili Ufanye Maendeleo

WATU wa Mungu walipoondoka Babiloni mwaka wa 537 K.W.K., Yehova alipendezwa na njia waliyotumia kurudi Yerusalemu. Aliwaambia hivi: “Fungueni njia ya watu. Fanyeni matuta, fanyeni matuta kwa ajili ya njia kuu. Ondoeni mawe juu yake.” (Isa. 62:10) Wazia jinsi Wayahudi walivyotii agizo hilo. Huenda wale waliotangulia waliitengeneza barabara hiyo, labda kwa kufunika mashimo na kuondoa mawe. Kufanya hivyo kungewasaidia ndugu zao waliokuwa nyuma yao.

Sisi pia tunapaswa kulainisha njia yetu ili kufikia miradi ya kiroho. Yehova anataka watumishi wake wote watembee kwenye njia hiyo bila vizuizi vyovyote visivyo vya lazima. Neno lake linatuhimiza hivi: “Lainisha mapito ya mguu wako, nazo njia zako zote na zifanywe imara.” (Met. 4:26) Iwe wewe ni kijana au una umri wa makamo, unaweza kuona hekima ya kutumia shauri hilo linalotoka kwa Mungu.

TAYARISHA NJIA KWA KUFANYA MAAMUZI MAZURI

Huenda umesikia watu wakisema hivi kuhusu kijana fulani: ‘Ana fursa nzuri sana ya kufanikiwa,’ au, ‘Atafika mbali.’ Kwa ujumla, vijana wana afya nzuri, wanajifunza mambo haraka, na wanatamani sana kufanikiwa maishani. Ndiyo sababu Biblia inasema hivi: “Uzuri wa vijana ni nguvu zao.” (Met. 20:29) Kijana anayetumia vipaji na nguvu zake kumtumikia Yehova anaweza kufikia miradi ya kiroho na kupata furaha ya kweli.

Hata hivyo, kama ujuavyo, ulimwengu unataka sana kutumia uwezo wa vijana wetu. Kijana Shahidi anapofanya vizuri shuleni, huenda mshauri, mwalimu, au mwanafunzi mwenzake akamshinikiza kufuatilia elimu ya juu ili afanikiwe katika mfumo huu wa mambo. Ndugu au dada kijana mwenye uwezo wa kuwa mwanariadha anaweza kushawishiwa kufuatilia michezo maishani. Je, umekabili hali kama hiyo, au unajua mtu fulani anayekabili mkazo kama huo? Ni nini kitakachomsaidia Mkristo kufanya uamuzi wa hekima?

Mafundisho ya Biblia yanaweza kumsaidia mtu ajitayarishe kutembea kwenye njia bora zaidi maishani. Andiko la Mhubiri 12:1 linasema hivi: “Mkumbuke, sasa, Muumba wako Mkuu katika siku za ujana wako.” Wewe au rafiki yako kijana mnawezaje ‘kumkumbuka Muumba wenu Mkuu’ kwa njia bora zaidi?

Mfikirie Erica kutoka Afrika Magharibi. Alipenda kucheza mpira wa miguu. Alianza kuchezea timu ya taifa akiwa na umri wa miaka 15. Punde si punde, angepata mazoezi ya pekee ya kucheza mpira barani Ulaya, na huenda baadaye angekuwa mchezaji wa kulipwa. Lakini shauri la ‘kumkumbuka Muumba wake Mkuu’ lingemsaidiaje? Wewe na rafiki zako vijana mnaweza kujifunza nini?

Eric alianza kujifunza Biblia na Mashahidi wa Yehova alipokuwa shuleni. Alijifunza kwamba Muumba wake ataondoa kabisa matatizo ya wanadamu. Eric alijifunza kwamba ni muhimu kutumia wakati na nguvu zake kufanya mapenzi ya Mungu. Kwa msingi wa hekima hiyo, Eric alichagua kutokuwa mwanamichezo wa kulipwa. Badala yake, alibatizwa na kujitahidi kufanya maendeleo ya kiroho. Baadaye, akawa mtumishi wa huduma na kisha akaalikwa kuhudhuria Shule ya Biblia ya Ndugu Waseja.

Huenda Eric angetajirika na kuwa mashuhuri ikiwa angefuatilia michezo. Lakini alitambua ukweli wa kanuni hii ya Biblia: “Vitu vyenye thamani vya tajiri ni mji wake wenye nguvu, navyo ni kama ukuta wa ulinzi katika mawazo yake.” (Met. 18:11) Kwa kweli, mtu anajidanganya anapofikiri kwamba utajiri unaweza kumlinda. Isitoshe, wale wanaofuatilia utajiri kwa bidii mara nyingi ‘hujichoma wenyewe kila mahali kwa maumivu mengi.’—1 Tim. 6:9, 10.

Inapendeza kwamba vijana wengi wamepata shangwe na usalama wa kudumu kwa kufanya utumishi wa wakati wote. Eric anasema hivi: “Nimejiunga na ‘timu’ kubwa ya watumishi wa Yehova wa wakati wote. Hiyo ndiyo timu bora zaidi, na ninamshukuru Yehova kwa kunionyesha njia pekee ya kupata furaha ya kweli na mafanikio maishani.”

Namna gani wewe? Badala ya kufuatilia miradi ya kilimwengu, kwa nini usiimarishe “njia zako” mbele za Yehova kwa kutumika ukiwa painia?​—Tazama sanduku lenye kichwa “Kupata Manufaa Yasiyopatikana Chuo Kikuu.”

KUONDOA VIZUIZI NJIANI

Wenzi fulani wa ndoa walipotembelea ofisi ya tawi ya Marekani waliona kwamba Wanabetheli walimtumikia Yehova kwa furaha. Dada aliandika hivi baadaye: “Tuliridhika sana na maisha yetu.” Wenzi hao waliamua kutumia wakati na nguvu zao kufanya mengi zaidi katika utumishi.

Mwanzoni, walihisi kwamba hawawezi kufanya mabadiliko yaliyohitajika. Lakini siku moja, walitafakari andiko la siku lililozungumzia maneno ya Yesu katika Yohana 8:31, linalosema hivi: “Mkikaa katika neno langu, ninyi kwa kweli ni wanafunzi wangu.” Hivyo, wakaamua hivi: “Manufaa tunayopata tunaporahisisha maisha yetu yanastahili dhabihu hiyo.” Waliuza nyumba yao kubwa na vitu wasivyohitaji na kuhamia kutaniko lililohitaji msaada. Sasa, wanafanya upainia, na pia wanasaidia katika ujenzi wa Majumba ya Ufalme na kujitolea katika makusanyiko ya wilaya. Wanahisije? “Kuishi maisha rahisi zaidi kumetuletea shangwe nyingi sana kwa sababu tunafanya kile ambacho tengenezo la Yehova linatuhimiza kufanya.”

ENDELEA KUFANYA MAENDELEO YA KIROHO

Sulemani aliandika hivi: “Macho yako yatazame mbele moja kwa moja, naam, macho yako yenye kung’aa yanapaswa kutazama mbele yako moja kwa moja.” (Met. 4:25) Kama dereva anayekazia fikira barabara, tunapaswa kuepuka mambo yanayoweza kutukengeusha na kutuzuia kuweka na kufikia miradi ya kiroho.

1. Mashahidi wa Yehova wakitumia ujana wao kufikia miradi ya kiroho; 2. Njia iliyoondolewa Vizuizi

Unaweza kuweka na kufikia miradi gani ya kiroho? Bila shaka, kuwa mtumishi wa wakati wote ni mradi mzuri. Unaweza pia kuhamia kutaniko la karibu linalohitaji wahubiri wenye uzoefu ili kuhubiri eneo lake kubwa. Au huenda kutaniko lina wahubiri wengi wenye uzoefu lakini halina wazee na watumishi wa huduma wa kutosha. Je, unaweza kusaidia katika mojawapo ya njia hizo? Kwa nini usizungumze na mwangalizi wa mzunguko ili akueleze jinsi unavyoweza kusaidia? Ikiwa unataka kuhamia eneo la mbali zaidi, unaweza kuomba habari kuhusu makutaniko ya mbali yanayohitaji msaada.b

Acheni tufikirie tena Isaya 62:10. Huenda baadhi ya Wayahudi walifanya kazi ngumu ya kulima na kutengeneza njia ili watu wa Mungu wafike Yerusalemu. Ikiwa unajitahidi kabisa kufikia miradi fulani katika utumishi mtakatifu, usife moyo. Kwa msaada wa Mungu, wewe pia unaweza kufikia miradi hiyo. Endelea kumwomba Yehova akupe hekima unapojitahidi kuondoa vizuizi kwenye njia yako. Kwa wakati unaofaa, inaelekea kwamba utaona Yehova akikusaidia ‘kulainisha mapito ya mguu wako.’—Met. 4:26.

a Jina limebadilishwa.

b Tazama kitabu Tengenezo Linalofanya Mapenzi ya Yehova, ukurasa wa 111 hadi 112.

Kupata Manufaa Yasiyopatikana Chuo Kikuu

Flavia

FLAVIA alipokuwa msichana mdogo, nyanya yake aliyekuwa Shahidi wa Yehova aliongea naye kuhusu Biblia. Hata hivyo, baba yake aliyekuwa mwalimu alimhimiza ajifunze kuhusu vitu vya asili na kufuatilia elimu ya juu. Watu wengine walimwambia hivi: “Kizazi chenu kinaweza kuokoa sayari yetu isiangamie.” Akiungwa mkono na baba yake, alijiunga na chuo kikuu maarufu na kuanza kufanya utafiti kuhusu njia za kuzalisha nishati isiyochafua mazingira.

Punde si punde, Flavia aligundua kwamba wanafunzi wengi hawakuwa na lengo la “kuokoa sayari.” Pia, baadhi ya miradi ya chuo ilidhaminiwa na kampuni fulani za kibiashara, kwa hiyo huenda watafiti walihisi kwamba wana wajibu wa kulinda kampuni hizo. Jambo hilo lilimsumbua sana Flavia. Mashahidi wa Yehova walipomtembelea nyumbani, alianza tena kupendezwa na inayosema Biblia kumhusu Mungu na wakati ujao.

Flavia alikubali kweli ya Biblia na kubatizwa. Hata hivyo, hakupata wakati wa kutosha wa kuhubiri habari njema kwa sababu alikuwa akisomea shahada ya juu ya digrii. Siku moja alimsikiliza mwangalizi wa mzunguko akizungumzia andiko la Yakobo 4:17: “Ikiwa mtu anajua jinsi ya kufanya yaliyo sawa na bado hayafanyi, hiyo ni dhambi kwake.” Hilo lilimchochea Flavia kufikiria hali yake. Anasema hivi: “Ingawa nilitaka baraka za Yehova, nilitaka pia kupata uradhi kutokana na kazi yangu nikiwa mwanasayansi. Nilihitaji kuamua.”

Flavia aliamua kukatiza masomo yake ya chuo kikuu. Je, anajuta? Anasema hivi:

“Katika utumishi wa Yehova, nimepata manufaa yasiyopatikana chuo kikuu. Yehova amekuwa mwema kwangu. Amenifundisha kuwa mwenye fadhili, kuwapenda na kuwasaidia wengine kiroho. Ninafurahia sana ndoa yangu na nina tumaini zuri ajabu la wakati ujao ambalo haliwezi kulinganishwa na ahadi za sayansi. Ni Yehova peke yake anayeweza kuiokoa sayari hii. Sitamwacha kamwe.” Flavia na mume wake wanatumika katika makao makuu ya Mashahidi wa Yehova huko New York.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki