Watchtower MAKTABA KWENYE MTANDAO
Watchtower
MAKTABA KWENYE MTANDAO
Kiswahili
  • BIBLIA
  • MACHAPISHO
  • MIKUTANO
  • w19 Desemba uku. 15
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Hakuna video yoyote kwa sasa.

Samahani, haikuwezekana kupakia video.

  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
  • Habari Zinazolingana
  • Maisha Yalikuwaje Katika Paradiso?
    Msikilize Mungu Uishi Milele
  • Uhai Baada ya Kifo—Watu Huamini Nini?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—1999
  • Uasi Katika Makao ya Roho
    Roho za Wafu—Je! Zaweza Kukusaidia au Kukuumiza? Je Ziko Kweli?
  • Je, Una Nafsi Isiyoweza Kufa?
    Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2007
Pata Habari Zaidi
Mnara wa Mlinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Funzo)—2019
w19 Desemba uku. 15

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Shetani alipomwambia Hawa kwamba hatakufa ikiwa atakula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya, je, alikuwa akianzisha wazo la kutokufa kwa nafsi lililoenea leo?

Hawa anashawishiwa na Shetani anayeongea kupitia nyoka

Inaonekana si hivyo. Ibilisi hakumwambia Hawa kwamba akila tunda alilokatazwa na Mungu angeonekana kwamba amekufa lakini sehemu fulani isiyoonekana iliyo ndani yake (sehemu ambayo watu fulani leo huiita nafsi isiyoweza kufa) ingeendelea kuishi mahali pengine. Akizungumza kupitia nyoka, Shetani alidai kwamba ikiwa Hawa angekula matunda ya mti huo, ‘hakika asingekufa’ kabisa. Alikuwa akimaanisha kwamba Hawa angeendelea kuishi, akifurahia maisha bora duniani bila ya kumtegemea Mungu.—Mwa. 2:17; 3:3-5.

Ikiwa fundisho la uwongo la kutokufa kwa nafsi linalofundishwa leo halikuanza katika Edeni, lilianzia wapi? Hatuna uhakika. Tunajua kwamba ibada zote za uwongo zilifutiliwa mbali katika Gharika ya siku za Noa. Hakuna mafundisho yoyote ya uwongo ya kidini yaliyoendelea kufuatwa baada ya Gharika kwa sababu ni Noa na familia yake tu ndio waliokoka, nao walikuwa waabudu wa kweli.

Hivyo basi, fundisho la sasa la kutokufa kwa nafsi ya mwanadamu lazima lilianzishwa mara tu baada ya Gharika. Mungu alipovuruga lugha Babeli na watu wakatawanyika “duniani pote kutoka huko,” ni wazi kwamba waliendeleza wazo la kwamba wanadamu wana nafsi isiyoweza kufa. (Mwa. 11:8, 9) Haidhuru fundisho hilo la uwongo lilianza lini, tunaweza kuwa na hakika kwamba “baba ya uwongo,” Shetani Ibilisi, alihusika na alifurahi sana kuona jinsi lilivyoenea kotekote.—Yoh. 8:44.

    Maktaba Kwenye Mtandao (1980-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili
    • Shiriki
    • Mapendezi
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Masharti ya Utumiaji
    • Sera ya Faragha
    • Mpangilio wa Faragha
    • JW.ORG
    • Ingia
    Shiriki