Pitio la Shule ya Huduma ya Kitheokrasi
Maswali yafuatayo yatazungumziwa katika Shule ya Huduma ya Kitheokrasi juma linaloanza Agosti 25, 2014.
Andiko la Mambo ya Walawi 18:3 linatusaidiaje tuweze kuepuka viwango vilivyopotoka vya kuamua mema na mabaya? (Efe. 4:17-19) [Julai 7, w02 2/1 uku. 29 fu. 4]
Sheria iliyoko katika Mambo ya Walawi 19:2 inatufundisha nini, na kwa nini tunapaswa kujitahidi kutii? [Julai 7, w09 7/1 uku. 9 fu. 5]
Kanuni iliyotegemeza sheria ya zamani ya kuokota masalio inatufundisha nini leo? (Law. 19:9, 10) [Julai 7, w06 6/15 uku. 22-23 fu. 13]
Kwa nini tunaweza kusema kwamba, sheria ya “jicho kwa jicho” haikupendekeza kulipiza kisasi? (Law. 24:19, 20) [Julai 14, w09 9/1 uku. 22 fu. 2-3]
Ni katika hali zipi ilikuwa kosa kwa Waisraeli kutoza riba kwenye mikopo, lakini kutoza riba kuliruhusiwa wakati gani? (Law. 25:35-37) [Julai 21, w04 5/15 uku. 24 fu. 3]
Kwa nini mara nyingi Maandiko hutaja makabila 12 ya Israeli ingawa kihalisi yalikuwa makabila 13? (Hes. 1:49, 50) [Julai 28, w08 7/1 uku. 21]
Tunajifunza somo gani kuhusu kuwaonyesha ufikirio wazee wazee kwenye simulizi linalohusu utumishi wa lazima wa Walawi katika andiko la Hesabu 8:25, 26? [Ago. 11, w04 8/1 uku. 25 fu. 1]
Kwa nini Waisraeli walisitawisha roho ya kunung’unika baada ya kutolewa Misri kimuujiza na tunaweza kujifunza somo gani muhimu kutokana na simulizi hilo? (Hes. 11:4-6) [Ago. 18, w95 3/1 uku. 15-16 fu. 10]
Tunajifunza nini tunaposoma kuhusu jinsi Musa alivyoitikia alipopata habari kwamba Eldadi na Medadi wanatenda kama manabii? (Hes. 11:27-29) [Ago. 18, w04 8/1 uku. 26 fu. 4]
Ni kanuni gani ya maana tunayoweza kujifunza kutokana na sheria waliyopewa Waisraeli ya ‘kujifanyia upindo wenye nyuzinyuzi kwenye miisho ya nguo zao’? (Hes. 15:37-39) [Ago. 25, w04 8/1 uku. 26 fu. 7]