Mapendekezo kwa Ajili ya Utumishi
Mnara wa Mlizi Julai 1
“Kwa kuwa hatujui yale yatakayotukia wakati ujao, unafikiri maneno ya Yesu kuhusu kuhangaika yanaweza kutusaidia? [Soma Mathayo 6:25, na umruhusu ajibu.] Gazeti hili la Mnara wa Mlinzi linazungumzia jinsi kutumia kanuni za Biblia kunavyoweza kutusaidia kupunguza mahangaiko kuhusu pesa, matatizo ya familia, na hatari zinazoweza kutupata.”
Amkeni Julai
“Watu wengi leo wanahangaishwa sana na hali zao za maisha. Je, unakubaliana na jambo hilo? [Mruhusu ajibu.] Biblia inaonyesha kwamba mtazamo unaofaa ni muhimu sana tunapokabili matatizo. [Soma Methali 24:10.] Gazeti hili lina madokezo mazuri ya jinsi ya kushughulikia hali ngumu na pia lina mifano ya watu wanaofanya hivyo leo.”