Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • Zaburi 53:utangulizi-6
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • Kwa kiongozi; katika mutindo wa Mahalati.* Maskili.* Ya Daudi.

      53 Mupumbavu* anasema katika moyo wake:

      “Hakuna Yehova.”+

      Matendo yao yenye hayako ya haki yamepotoka na yanachukiza;

      Hakuna mwenye kutenda mema.+

       2 Lakini Mungu anaangalia wana wa binadamu akiwa mbinguni+

      Ili aone kama kuko mutu yeyote mwenye kuwa na ufahamu, kama kuko mutu yeyote mwenye kumutafuta Yehova.+

       3 Wote wamekengeuka;

      Wote pamoja wamepotoka.

      Hakuna mwenye kutenda mema,

      Hakuna hata mumoja.+

       4 Je, hakuna hata mumoja kati ya wakosaji mwenye anaelewa?

      Wanameza watu wangu kama vile wanakula mukate.

      Hawamuitie Yehova.+

       5 Lakini watajaa woga mukubwa,

      Woga wenye hawajapata kuwa nao hata siku moja,*

      Kwa maana Mungu atasambaza mifupa ya wale wenye kuwashambulia ninyi.*

      Mutawapatisha haya, kwa maana Yehova amewakataa wao.

       6 Aa! kama tu wokovu wa Israeli ungetoka Sayuni!+

      Wakati Yehova atakusanya tena watu wake wenye walikamatwa mateka,

      Yakobo ashangilie, Israeli afurahi.

  • Waroma 3:10-12
    Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
    • 10 kama vile imeandikwa: “Hakuna mwenye haki, hakuna hata mumoja;+ 11 hakuna hata mumoja mwenye kuwa na ufahamu; hakuna hata mumoja mwenye anamutafuta Mungu. 12 Watu wote wameenda pembeni, wote wamekuwa wenye hawana mafaa yoyote; hakuna hata mumoja mwenye anaonyesha fazili, hakuna hata mumoja.”+

Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine