Hesabu
27 Kisha mabinti wa Selofehadi,+ mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase, wa familia za Manase mwana wa Yosefu, wakakaribia. Majina ya mabinti hao yalikuwa Mala, Noa, Hogla, Milka, na Tirsa. 2 Wakasimama mbele ya Musa, mbele ya Eleazari kuhani, mbele ya wakubwa,+ na mbele ya mukusanyiko wote kwenye muingilio wa hema ya mukutano na wakasema: 3 “Baba yetu alikufa katika jangwa, lakini hakukuwa katika kikundi chenye kilijiunga pamoja ili kumupinga Yehova, watu wenye walimuunga Kora mukono,+ lakini alikufa kwa sababu ya zambi yake mwenyewe na hakukuwa na mutoto yeyote mwanaume. 4 Sababu gani jina la baba yetu lipotee katika familia yake kwa sababu hakukuwa na mutoto mwanaume? Utupatie uriti kati ya ndugu za baba yetu.” 5 Kwa hiyo Musa akapeleka jambo lao mbele ya Yehova.+
6 Kisha Yehova akamuambia Musa hivi: 7 “Mabinti wa Selofehadi wanasema kweli. Unapaswa kabisa kuwapatia uriti kati ya ndugu za baba yao na kupitisha uriti wa baba yao kwao.+ 8 Na uambie Waisraeli, ‘Kama mutu anakufa bila kuwa na mutoto mwanaume, basi mutapitisha uriti wake kwa mutoto wake mwanamuke. 9 Na kama hana mutoto mwanamuke, mutapatia ndugu zake uriti wake. 10 Na kama hana ndugu, mutapatia ndugu za baba yake uriti wake. 11 Na kama baba yake hana ndugu, mutapatia uriti wake mutu wa karibu mwenye iko* na uhusiano wa damu pamoja naye katika familia yake, naye ataukamata kuwa mali yake. Hii itakuwa sheria ya uamuzi wa hukumu kwa ajili ya Waisraeli, kama vile Yehova amemuamuru Musa.’”
12 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Panda katika mulima huu wa Abarimu,+ na uone inchi yenye nitapatia Waisraeli.+ 13 Kisha kuiona, utakusanywa pia kwa watu wako,*+ kama vile Haruni ndugu yako alikusanywa,+ 14 kwa sababu wakati mukusanyiko ulikuwa unagombana na mimi katika jangwa la Zini, muliasi agizo langu la kunitakasa mbele yao kupitia maji.+ Hayo ndiyo maji ya Meriba+ kule Kadeshi+ katika jangwa la Zini.”+
15 Kisha Musa akamuambia Yehova: 16 “Yehova, Mungu wa roho ya watu wote,* aweke juu ya mukusanyiko mwanaume 17 mwenye atatoka inje na kuingia ndani mbele yao na kuwatosha inje na kuwaingiza ndani, ili mukusanyiko wa Yehova usikuwe kama kondoo wenye hawana muchungaji.” 18 Kwa hiyo Yehova akamuambia Musa: “Chukua Yoshua mwana wa Nuni, mwanaume mwenye roho iko ndani yake, na utie mukono wako juu yake.+ 19 Kisha umusimamishe mbele ya kuhani Eleazari na mbele ya mukusanyiko wote, na umuweke katika madaraka mbele ya macho yao.+ 20 Utamupatia sehemu fulani ya mamlaka* yako,+ ili mukusanyiko wote wa Waisraeli umusikilize.+ 21 Atasimama mbele ya Eleazari kuhani, mwenye atauliza kwa ajili yake kulingana na hukumu ya Urimu+ mbele ya Yehova. Kwa agizo lake watu watatoka inje na kwa agizo lake wataingia ndani, yeye na Waisraeli wote wenye kuwa pamoja naye na mukusanyiko wote.”
22 Kwa hiyo Musa akafanya kama vile Yehova alikuwa amemuamuru. Akamuchukua Yoshua na kumusimamisha mbele ya Eleazari kuhani na mbele ya mukusanyiko wote, 23 na akaweka mikono yake juu yake na kumuweka katika madaraka,+ kama vile Yehova alikuwa amesema kupitia Musa.+