Hesabu
21 Wakati mufalme Mukanaani wa Aradi,+ mwenye aliishi Negebu, alisikia kama Israeli alikuwa amekuja kupitia njia ya Atarimu, alishambulia Israeli na kukamata mateka wamoja kati yao. 2 Kwa hiyo Israeli akafanya naziri hii kwa Yehova: “Kama unatia watu hawa katika mukono wangu, hakika nitaharibu miji yao.” 3 Kwa hiyo Yehova akasikiliza sauti ya Israeli na akatia Wakanaani katika mikono yao, na wakawaharibu pamoja na miji yao. Basi wakaita mahali pale Horma.*+
4 Wakati waliendelea na safari yao kutoka Mulima Hori+ kupitia njia ya Bahari Nyekundu ili kuzunguka inchi ya Edomu,+ watu wakachoka* kwa sababu ya safari. 5 Na watu wakaendelea kusema mubaya juu ya Mungu na juu ya Musa,+ na kusema: “Sababu gani mumetupandisha kutoka Misri ili tukufie katika jangwa? Hakuna chakula na maji,+ na sisi tumechukia* mukate huu wenye kuzaraulika.”+ 6 Kwa hiyo Yehova akatuma nyoka wenye sumu* kati ya watu, na nyoka hao wakaendelea kuuma watu, na hivyo Waisraeli wengi wakakufa.+
7 Kwa hiyo watu wakakuja kwa Musa na kumuambia: “Tumefanya zambi kwa kusema mubaya juu ya Yehova na juu yako.+ Umulilie Yehova ili atuondolee nyoka hawa.” Na Musa akamulilia Mungu kwa ajili ya watu.+ 8 Kisha Yehova akamuambia Musa: “Tengeneza nyoka mwenye sumu* wa mufano na umuweke juu ya nguzo. Basi wakati mutu yeyote ameumwa, ataangalia mufano huo ili aendelee kuishi.” 9 Mara moja Musa akatengeneza nyoka wa shaba+ na kumuweka juu ya nguzo,+ na kila mara wakati nyoka alikuwa ameuma mutu na mutu huyo aangalie nyoka huyo wa shaba, aliendelea kuishi.+
10 Kisha Waisraeli wakaondoka na kupiga kambi Oboti.+ 11 Halafu wakaondoka Oboti na kupiga kambi Iye-abarimu,+ katika jangwa lenye linaangaliana na Moabu, kuelekea upande wa mashariki. 12 Kutoka pale wakaondoka na kupiga kambi karibu na Bonde* la Zeredi.+ 13 Kutoka pale wakaondoka na kupiga kambi katika eneo la Arnoni,+ lenye kuwa katika jangwa na lenye linasambaa kuanzia mupaka wa Waamori, kwa maana Arnoni ni mupaka wa Moabu, katikati ya Moabu na Waamori. 14 Ndiyo sababu kitabu cha Vita za Yehova kinazungumuzia “Vahebu katika eneo la Sufa na mabonde ya Arnoni, 15 na muteremuko wa* mabonde, wenye unasambaa kuelekea makao ya Ari na kufika kwenye mupaka wa Moabu.”
16 Kisha wakasafiri mupaka Beeri. Ni kuhusu kisima hicho Yehova alimuambia Musa: “Wakusanye watu, ili niwapatie maji.”
17 Wakati huo, Israeli aliimba wimbo huu:
“Bubujika, Ee kisima!—Mukijibu!*
18 Kisima chenye wakubwa walichimba, chenye watu wenye vyeo kati ya watu walichimba,
Kwa fimbo ya kamanda na kwa fimbo zao wenyewe.”
Kisha wakatoka katika jangwa na kuenda Matana, 19 kutoka Matana mupaka Nahalieli, na kutoka Nahalieli mupaka Bamoti.+ 20 Wakatoka Bamoti na kuenda kwenye bonde lenye kuwa katika eneo* la Moabu,+ kwenye kichwa cha Pisga,+ yenye inaangaliana na Yeshimoni.*+
21 Sasa Israeli akatuma wajumbe kwa Sihoni, mufalme wa Waamori, ili wamuambie:+ 22 “Uturuhusu tupite katika inchi yako. Hatutageuka na kuingia katika shamba ao shamba la mizabibu. Hatutakunywa maji ya kisima chochote. Tutatembea katika Barabara ya Mufalme mupaka wakati tutakuwa tumepita katika eneo lako.”+ 23 Lakini Sihoni hakuruhusu Israeli apitie katika eneo lake. Tofauti na hiyo, Sihoni akakusanya watu wake wote na kuenda kushambulia Israeli katika jangwa na akafika Yahazi na kuanza kupigana na Israeli.+ 24 Lakini Israeli akamushinda kwa upanga+ na akakamata inchi yake+ kuanzia Arnoni+ mupaka Yaboki,+ karibu na Waamoni, kwa sababu muji wa Yazeri+ uko kwenye mupaka wa eneo la Waamoni.+
25 Kwa hiyo Israeli akakamata miji hiyo yote, na wakaanza kuishi katika miji yote ya Waamori,+ katika Heshboni na miji yake yote ya pembeni-pembeni.* 26 Kwa maana Heshboni ulikuwa muji wa Sihoni, mufalme wa Waamori, mwenye alikuwa amepigana na mufalme wa Moabu na kukamata inchi yake yote mupaka Arnoni. 27 Ndiyo maana watu walitunga usemi huu wa kimezali wa uchokozi:
“Mukuje Heshboni.
Muji wa Sihoni ujengwe na kufanywa imara kabisa.
28 Kwa maana moto ulitoka Heshboni, mwali wa moto ulitoka katika muji wa Sihoni.
Umeteketeza muji wa Ari wa Moabu, mabwana wa mahali pa juu pa Arnoni.
29 Ole wako, Moabu! Mutaharibiwa, Enyi watu wa Kemoshi!+
Anafanya watoto wake wanaume kuwa wakimbizi na watoto wake wanamuke kuwa watu wenye walikamatwa mateka wa Sihoni, mufalme wa Waamori.
30 Tuwatupie mishale;
Heshboni utaharibiwa mupaka Diboni;+
Tuuharibu mupaka Nofa;
Moto utasambaa mupaka Medeba.”+
31 Kwa hiyo Israeli akaanza kuishi katika inchi ya Waamori. 32 Kisha Musa akatuma watu fulani wapeleleze Yazeri.+ Wakakamata miji yake ya pembeni-pembeni* na wakafukuza Waamori wenye walikuwa kule. 33 Kisha wakageuka na kupanda kupitia Njia ya Bashani. Na Ogu+ mufalme wa Bashani akatoka pamoja na watu wake wote ili kupigana nao kule Edrei.+ 34 Yehova akamuambia Musa: “Usimuogope,+ kwa maana nitamutia yeye na watu wake wote na inchi yake katika mukono wako,+ na utamutendea kama vile ulimutendea Sihoni mufalme wa Waamori, mwenye aliishi Heshboni.”+ 35 Kwa hiyo wakaendelea kumupiga na kumuua, yeye pamoja na wana wake na watu wake wote, mupaka hapakukuwa hata mumoja wa watu wake mwenye aliokoka,+ na wakakamata inchi yake.+