Muhubiri
1 Maneno ya mukutanishaji,*+ mwana wa Daudi, mufalme katika Yerusalemu.+
3 Mutu anapata faida gani kwa kazi zake zote za nguvu
Zenye anafanya kwa jasho chini ya jua?+
6 Upepo unaenda kusini na kuzunguka mupaka kaskazini;
Unaendelea kuzunguka tena na tena; upepo unaendelea kufanya mizunguko yake.
7 Mito yote ya kidogo* inatiririka kuingia katika bahari, lakini bahari haijae.+
Mahali mito ya kidogo inatoka, ni kule inarudia ili kutiririka tena.+
8 Mambo yote yanachokesha;
Hakuna mwenye anaweza hata kueleza juu ya hilo.
Jicho halishibake kuona;
Na sikio halijae kwa sababu ya kusikia.
9 Mambo yenye yamekwisha kuwa, ndiyo yatakuwa tena,
Na mambo yenye yamekwisha kufanywa, ndiyo yatafanywa tena;
Hakuna kitu kipya chini ya jua.+
10 Je, kuko kitu chochote chenye mutu anaweza kusema, “Angalia hiki—ni kipya”?
Kimekuwa tangu zamani sana;
Kimekuwa mbele ya wakati wetu.
11 Hakuna mwenye anakumbuka watu wa zamani;
Wala hakuna mwenye atakumbuka wenye watakuja;
Wala wale wenye watakuja kisha hawatawakumbuka.+
12 Mimi, mukutanishaji, nimekuwa mufalme juu ya Israeli katika Yerusalemu.+ 13 Niliazimia katika moyo wangu kujifunza na kuchunguza kwa hekima+ kila jambo lenye limefanywa chini ya mbingu+—kazi zenye kutaabisha zenye Mungu amepatia wana wa binadamu wafanye.
14 Niliona kazi zote zenye zilifanywa chini ya jua,
Na angalia! mambo yote yalikuwa bure,* na kufuatilia upepo.+
15 Kitu chenye kukunjama hakiwezi kunyooshwa,
Na kitu chenye kukosekana hakiwezi kuhesabiwa.
16 Kisha nikasema katika moyo wangu: “Angalia! Nimepata hekima nyingi, kuliko mutu yeyote mwenye alinitangulia Yerusalemu,+ na moyo wangu umepata hekima nyingi sana na ujuzi.”+ 17 Nilijikaza sana katika moyo wangu ili nijue hekima na kujua wazimu* na kujua ujinga,+ na hayo pia ni kufuatilia upepo.
18 Kwa maana hekima nyingi inaleta hali ya kuvunjika moyo sana,
Kwa hiyo kila mutu mwenye anaongeza ujuzi anaongeza maumivu.+