Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Mhubiri 1:1-12:14
  • Muhubiri

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Muhubiri
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Muhubiri

MUHUBIRI

1 Maneno ya mukutanishaji,*+ mwana wa Daudi, mufalme katika Yerusalemu.+

 2 “Yote ni bure* kabisa!” ni vile mukutanishaji anasema,

“Yote ni bure kabisa! Kila kitu ni bure!”+

 3 Mutu anapata faida gani kwa kazi zake zote za nguvu

Zenye anafanya kwa jasho chini ya jua?+

 4 Kizazi kinapita, na kizazi kinakuja,

Lakini dunia inadumu* milele.+

 5 Jua linatokea,* na jua linashuka;

Na linarudia haraka mahali kwenye litatokea tena.+

 6 Upepo unaenda kusini na kuzunguka mupaka kaskazini;

Unaendelea kuzunguka tena na tena; upepo unaendelea kufanya mizunguko yake.

 7 Mito yote ya kidogo* inatiririka kuingia katika bahari, lakini bahari haijae.+

Mahali mito ya kidogo inatoka, ni kule inarudia ili kutiririka tena.+

 8 Mambo yote yanachokesha;

Hakuna mwenye anaweza hata kueleza juu ya hilo.

Jicho halishibake kuona;

Na sikio halijae kwa sababu ya kusikia.

 9 Mambo yenye yamekwisha kuwa, ndiyo yatakuwa tena,

Na mambo yenye yamekwisha kufanywa, ndiyo yatafanywa tena;

Hakuna kitu kipya chini ya jua.+

10 Je, kuko kitu chochote chenye mutu anaweza kusema, “Angalia hiki⁠—ni kipya”?

Kimekuwa tangu zamani sana;

Kimekuwa mbele ya wakati wetu.

11 Hakuna mwenye anakumbuka watu wa zamani;

Wala hakuna mwenye atakumbuka wenye watakuja;

Wala wale wenye watakuja kisha hawatawakumbuka.+

12 Mimi, mukutanishaji, nimekuwa mufalme juu ya Israeli katika Yerusalemu.+ 13 Niliazimia katika moyo wangu kujifunza na kuchunguza kwa hekima+ kila jambo lenye limefanywa chini ya mbingu+⁠—​kazi zenye kutaabisha zenye Mungu amepatia wana wa binadamu wafanye.

14 Niliona kazi zote zenye zilifanywa chini ya jua,

Na angalia! mambo yote yalikuwa bure,* na kufuatilia upepo.+

15 Kitu chenye kukunjama hakiwezi kunyooshwa,

Na kitu chenye kukosekana hakiwezi kuhesabiwa.

16 Kisha nikasema katika moyo wangu: “Angalia! Nimepata hekima nyingi, kuliko mutu yeyote mwenye alinitangulia Yerusalemu,+ na moyo wangu umepata hekima nyingi sana na ujuzi.”+ 17 Nilijikaza sana katika moyo wangu ili nijue hekima na kujua wazimu* na kujua ujinga,+ na hayo pia ni kufuatilia upepo.

18 Kwa maana hekima nyingi inaleta hali ya kuvunjika moyo sana,

Kwa hiyo kila mutu mwenye anaongeza ujuzi anaongeza maumivu.+

2 Kisha nikasema katika moyo wangu: “Kuja na nijaribu raha,* na nione nitapata mema gani.” Lakini angalia! hilo pia lilikuwa bure.*

 2 Kuhusu kicheko nilisema, “Ni wazimu!”

Na kuhusu raha,* “Iko na faida gani?”

3 Nilichunguza kwa moyo wangu kwa kujifurahisha kupitia divai,+ na wakati huo niliendelea kulinda hekima yangu; hata nilikumbatia upumbavu ili nione ni jambo gani la muzuri sana lenye wanadamu wanapaswa kufanya kwa siku kidogo za maisha yao chini ya mbingu. 4 Nilifanya mambo makubwa.+ Nilijijengea nyumba nyingi;+ Nilijipandia mashamba ya mizabibu.+ 5 Nilitengeneza mashamba na bustani zangu, na nilipanda ndani kila namna ya miti ya matunda. 6 Nilijifanyia viziwa vya maji, ili kumwangilia maji pori la miti yenye kukomaa muzuri. 7 Nikakuwa na watumishi wanaume na watumishi wanamuke,+ na watumishi wengine walizaliwa katika nyumba yangu.* Pia, nikakuwa na mifugo mingi⁠—ngombe na makundi+⁠—​kuliko watu wote wenye walinitangulia Yerusalemu. 8 Nilijikusanyia feza na zahabu,+ hazina za* wafalme na za majimbo.+ Nilijikusanyia waimbaji wanaume na waimbaji wanamuke, na pia kile chenye kinaletea wana wa binadamu furaha nyingi⁠—​mwanamuke, ndiyo, wanamuke wengi.* 9 Basi nikakuwa mukubwa na nikapita wale wote wenye walinitangulia Yerusalemu.+ Na hekima yangu ilibakia pamoja na mimi.

10 Sikujiima kitu chochote chenye nilitamani.*+ Sikuima moyo wangu raha* yoyote, kwa maana moyo wangu ulifurahi kwa sababu ya kazi yangu yote ya nguvu, na hiyo ndiyo zawabu yenye* nilipata kwa sababu ya kazi yangu yote ya nguvu.+ 11 Lakini wakati nilifikiria kazi zote zenye mikono yangu ilikuwa imefanya na kazi yote ya nguvu yenye nilitoa jasho ili kuitimiza,+ niliona kwamba kila kitu ni bure,* na kufuatilia upepo;+ sikuona kitu chochote chenye kuwa cha maana kabisa* chini ya jua.+

12 Kisha nikaanza kuchunguza hekima, wazimu, na ujinga.+ (Kwa maana mutu mwenye atakuja kisha mufalme atafanya nini? Atafanya tu mambo yenye yamekwisha kufanywa.) 13 Na nikaona kwamba hekima iko na faida kuliko ujinga,+ kama vile mwangaza uko na faida kuliko giza.

14 Macho ya mutu mwenye hekima yako katika kichwa chake;*+ lakini mujinga anatembea katika giza.+ Pia nimefikia kutambua kwamba kuko jambo moja lenye linafikia* watu wote.+ 15 Kisha nikasema katika moyo wangu: “Kile kinapataka mujinga ni kile kitanipata mimi pia.”+ Sasa, nimepata faida gani kwa kuwa na hekima nyingi sana? Basi nikasema katika moyo wangu: “Jambo hili pia ni bure.”* 16 Kwa maana mutu mwenye hekima kama vile mujinga, wote hawataendelea kukumbukwa.+ Katika siku zenye kuja, wote watasahauliwa. Na mutu mwenye hekima atakufa namna gani? Pamoja na mujinga.+

17 Basi nikachukia maisha,+ kwa sababu niliona kila jambo lenye kufanywa chini ya jua kuwa linasikitisha, kwa maana kila jambo lilikuwa bure,*+ na kufuatilia upepo.+ 18 Nilifikia kuchukia kazi yote ya nguvu yenye nilikuwa nimefanya chini ya jua,+ kwa sababu ni lazima niiachie ule mwenye atakuja kisha mimi.+ 19 Na ni nani anajua kama atakuwa mwenye hekima ao mupumbavu?+ Lakini atasimamia vitu vyote vyenye nilitumia nguvu na hekima nyingi ili kuvipata chini ya jua. Jambo hilo pia ni bure.* 20 Basi nikaanza kupoteza tumaini katika moyo wangu kwa sababu ya kazi yote ya nguvu yenye nilikuwa nimefanya kwa jasho chini ya jua. 21 Kwa maana mutu anaweza kufanya kazi ya nguvu, akiongozwa na hekima na ujuzi na ufundi, lakini analazimika kuachia fungu lake mutu mwenye hakulitumikia.*+ Hili pia ni bure* na ni jambo la mubaya sana.*

22 Kwa kweli mutu anapata faida gani kwa kazi yake yote ya nguvu na tamaa yenye inamuchochea* kufanya kazi kwa bidii chini ya jua?+ 23 Kwa maana siku zake zote, kazi yake inamuletea maumivu na hali ya kuvunjika moyo,+ na hata usiku moyo wake haupumuzike.+ Jambo hili pia ni bure.*

24 Hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mutu kuliko kula, kunywa, na kufurahia kazi yake ya nguvu.+ Nilivumbua kwamba jambo hili pia linatoka katika mukono wa Mungu wa kweli,+ 25 kwa maana ni nani anakula na kunywa muzuri kuliko mimi?+

26 Anamupatia mutu mwenye anamupendeza hekima na ujuzi na furaha,+ lakini anamupatia mutenda-zambi kazi ya kukusanya na kurundika tu ili apatie ule mwenye anamupendeza Mungu wa kweli.+ Jambo hilo pia ni bure,* ni kufuatilia upepo.

3 Kila kitu kiko na wakati wake wenye uliwekwa,

Kila kazi chini ya mbingu iko na wakati wake:

 2 Wakati wa kuzaliwa na wakati wa kufa;

Wakati wa kupanda na wakati wa kungoa kitu chenye kilipandwa;

 3 Wakati wa kuua na wakati wa kuponyesha;

Wakati wa kubomoa na wakati wa kujenga;

 4 Wakati wa kulia na wakati wa kucheka;

Wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza;*

 5 Wakati wa kutupa majiwe na wakati wa kukusanya majiwe;

Wakati wa kukumbatia na wakati wa kujizuia kukumbatia;

 6 Wakati wa kutafuta na wakati wa kuacha kutafuta chenye kimepotea;

Wakati wa kulinda na wakati wa kutupa;

 7 Wakati wa kupasua+ na wakati wa kushona,

Wakati wa kunyamaza+ na wakati wa kusema;+

 8 Wakati wa kupenda na wakati wa kuchukia;+

Wakati wa vita na wakati wa amani.

9 Mufanyakazi anapata faida gani kwa bidii yake yote?+ 10 Nimeona kazi yenye Mungu amepatia wana wa binadamu wafanye. 11 Amefanya kila kitu kuwa kizuri* kwa wakati wake.+ Hata ametia umilele katika moyo wao; lakini wanadamu hawatavumbua hata siku moja kazi yenye Mungu wa kweli amefanya tangu mwanzo mupaka mwisho.

12 Nimeona kwamba hakuna jambo la muzuri zaidi kwao kuliko kufurahi na kufanya mema wakati wa maisha yao,+ 13 na kwamba kila mutu anapaswa kula na kunywa na kufurahia kazi yake yote ya nguvu. Ni zawadi ya Mungu.+

14 Nimefikia kujua kwamba kila kitu chenye Mungu wa kweli anafanya kitadumu milele. Hakuna chenye kinaweza kuongezwa wala kupunguzwa juu ya hicho. Mungu wa kweli amefanya mambo yakuwe vile, ili watu wamuogope.+

15 Kila kitu chenye kinatokea kimekwisha kutokea, na kile kitakuja kimekwisha kuwa;+ lakini Mungu wa kweli anatafuta kile kimekuwa kikifuatiliwa.*

16 Tena nimeona hili chini ya jua: Mahali pa haki palikuwa uovu, na mahali pa uadilifu* palikuwa uovu.+ 17 Basi nikasema katika moyo wangu: “Mungu wa kweli atahukumu wenye haki na waovu,+ kwa maana kila kazi na kila jambo liko na wakati wake.”

18 Pia nikasema katika moyo wangu kuhusu wana wa binadamu kwamba Mungu wa kweli atawajaribu na kuwaonyesha kwamba wako kama wanyama, 19 kwa maana kuko jambo moja lenye linapata* wanadamu na jambo moja lenye linapata wanyama; wote wanapatwa na jambo lilelile.+ Namna mumoja anakufa, ni vile mwingine anakufa; na wote wako na roho ileile.+ Kwa hiyo mwanadamu hashindie wanyama, kwa sababu kila kitu ni bure.* 20 Wote wanaenda mahali palepale.+ Wote wanatoka katika mavumbi,+ na wote wanarudia katika mavumbi.+ 21 Ni nani kabisa anajua kama roho ya wanadamu inapanda juu, na kama roho ya wanyama inashuka kwenye udongo?+ 22 Na niliona kwamba hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kuliko kufurahia kazi yake,+ kwa sababu hiyo ndiyo zawabu yake,* kwa maana ni nani anaweza kumuonyesha mambo yenye yatatokea kisha yeye kufa?+

4 Nikachunguza tena matendo yote ya ukandamizaji yenye kufanywa chini ya jua. Nikaona machozi ya wenye kukandamizwa, na hapakukuwa mutu wa kuwafariji.+ Na wakandamizaji wao walikuwa na nguvu, na wale wenye kukandamizwa hawakukuwa na mutu wa kuwafariji. 2 Na nilipongeza wafu wenye walikuwa tayari wamekufa kuliko wazima wenye walikuwa wangali wanaishi.+ 3 Na mwenye kuwa katika hali ya muzuri zaidi kuliko wote wawili ni ule mwenye hajazaliwa,+ mwenye hajaona mambo yenye kuhuzunisha yenye yanafanywa chini ya jua.+

4 Na nimeona namna kushindana+ kunafanya watu wajikaze sana* na kufanya kazi kwa ufundi; jambo hili pia ni bure,* ni kufuatilia upepo.

5 Mujinga anakunja mikono yake na wakati huo mwili wake unaendelea kuwa muzaifu.*+

6 Mukono mumoja wa pumuziko ni muzuri zaidi kuliko mikono mbili ya kazi ya nguvu na kufuatilia upepo.+

7 Nilichunguza jambo lingine lenye kuwa bure* chini ya jua: 8 Kuko mutu mwenye kuwa peke yake; hana rafiki; hana mwana wala ndugu, lakini kazi yake yote ya nguvu haina mwisho. Macho yake hayashibake utajiri.+ Lakini hajiulizake, ‘Ninafanya kazi hii yote ya nguvu na kujiima mambo ya muzuri kwa ajili ya nani’?+ Jambo hili pia ni bure* na ni lenye kuhuzunisha.+

9 Wawili ni muzuri zaidi kuliko mumoja+ kwa sababu wako na zawabu ya muzuri* kwa ajili ya kazi yao ya nguvu. 10 Kwa maana kama mumoja wao anaanguka, ule mwingine anaweza kusimamisha mwenzake. Lakini itakuwa namna gani kwa ule mwenye kuwa peke yake kama anaanguka bila mutu wa kumusimamisha?

11 Tena, kama wawili wanalala pamoja, watapata joto, lakini mwenye kuwa peke yake anaweza namna gani kupata joto? 12 Mutu anaweza kumushinda nguvu mwenye kuwa peke yake, lakini wawili wenye kuwa pamoja wanaweza kushindana naye. Na kamba ya nyuzi tatu (3) haiwezi kukatika haraka.*

13 Mutoto maskini lakini mwenye hekima ni muzuri zaidi kuliko mufalme muzee lakini mujinga,+ mwenye haone tena ulazima wa kutii maonyo.+ 14 Kwa maana yeye* alitoka katika gereza na kuwa mufalme,+ hata kama alizaliwa maskini katika ufalme huo.+ 15 Nilichunguza wale wote wenye kuwa wazima wenye wanatembea chini ya jua, na pia hali ya ule mutawala kijana mwenye anakamata nafasi ya ule mwingine. 16 Hata kama iko* na watu wengi sana wenye kumuunga mukono, wale wenye watakuja kisha hawatamufurahia.+ Jambo hili pia ni bure,* ni kufuatilia upepo.

5 Ukuwe muangalifu wakati unaenda katika nyumba ya Mungu wa kweli;+ ni muzuri zaidi ukaribie ili kusikiliza+ kuliko kutoa zabihu kama vile wajinga wanafanya,+ kwa maana hawajue kwamba jambo lenye wanafanya ni mubaya.

2 Usikuwe haraka kufungua kinywa chako, wala usiache moyo wako useme haraka mbele ya Mungu wa kweli,+ kwa maana Mungu wa kweli iko* mbinguni lakini wewe uko katika dunia. Ndiyo sababu maneno yako yanapaswa kuwa kidogo.+ 3 Kwa maana ndoto inatokana na mawazo mengi sana,*+ na kusema-sema kwa mujinga kunatokana na maneno mengi sana.+ 4 Kila mara wakati unaweka naziri kwa Mungu, usikawie kuitimiza,+ kwa maana hafurahie wajinga.+ Naziri yenye unaweka, uitimize.+ 5 Ni muzuri zaidi usiweke naziri kuliko kuweka naziri na kukosa kuitimiza.+ 6 Usiruhusu kinywa chako kikufanye* utende zambi,+ na usiseme mbele ya malaika* kwamba lilikuwa kosa.+ Sababu gani umukasirishe Mungu wa kweli kwa sababu ya maneno yenye unasema na hivyo kumufanya aharibu kazi ya mikono yako?+ 7 Kwa maana kama vile mawazo mengi yanafanya mutu aote ndoto,+ vilevile, maneno mengi yanaongoza kwenye mambo ya bure.* Lakini umuogope Mungu wa kweli.+

8 Kama unaona maskini wanakandamizwa kwa njia yoyote na haki inavunjwa na uadilifu* havifuatwe katika wilaya yako, jambo hilo lisikushangaze.+ Kwa maana ofisa mukubwa iko* anaangaliwa na ule mwenye kuwa juu zaidi kuliko yeye, na kuko wengine wenye wako tena juu kuliko wao.

9 Pia, wao wote wanagawana faida ya inchi; hata mufalme anapata faida kutoka katika shamba.+

10 Mwenye anapenda feza hatashiba feza, wala mwenye anapenda mali hatashiba mapato.+ Jambo hili pia ni bure.*+

11 Wakati vitu vya muzuri vinaongezeka, wenye kuvikula wanaongezeka.+ Na mwenye vitu hivyo anapata faida gani, isipokuwa kuviangalia tu na macho yake?+

12 Usingizi wa mutumishi ni mutamu, ikuwe amekula mingi ao kidogo, lakini vitu vingi vyenye tajiri iko* navyo havimuruhusu alale.

13 Kuko jambo la mubaya sana lenye* nimeona chini ya jua: utajiri wenye mutu alijirundikia ili kujiumiza mwenyewe. 14 Utajiri huo ulipotea kwa sababu ya kuutumia mubaya,* na wakati anazaa mwana, hana kitu chochote chenye alibakia nacho.+

15 Kama vile mutu alitoka katika tumbo la uzazi la mama yake, ataenda akiwa uchi, kama vile alikuja.+ Na hawezi kubeba kitu chochote kwa ajili ya kazi yake yote ya nguvu.+

16 Hili pia ni jambo la mubaya sana:* Kama vile alikuja, ni vile ataenda; na kuko faida gani kwa mutu mwenye anaendelea kufanya kazi ya nguvu kwa ajili ya upepo?+ 17 Pia, kila siku anakula katika giza, akiwa amevunjika moyo kabisa na akiwa mugonjwa na mwenye kukasirika.+

18 Nimeona kwamba hili ndilo jambo la muzuri na lenye kufaa: kwamba mutu anapaswa kula, kunywa, na kufurahia kazi yake yote ya nguvu+ yenye anafanya kwa jasho chini ya jua siku kidogo za maisha yenye Mungu wa kweli amemupatia, kwa maana hiyo ndiyo zawabu yake.*+ 19 Pia, wakati Mungu wa kweli anapatia mutu utajiri na vitu vya kimwili+ na kumuwezesha kuvifurahia, anapaswa kukamata zawabu yake* na kufurahia kazi yake ya nguvu. Hiyo ni zawadi ya Mungu.+ 20 Kwa maana itakuwa vigumu kwake kutambua* kwamba siku za maisha yake zinapita haraka, kwa sababu Mungu wa kweli anamufanya aendelee kufurahi sana katika moyo wake.+

6 Kuko jambo lingine la mubaya sana lenye* nimeona chini ya jua, na linatokea mara nyingi kati ya wanadamu: 2 Mungu wa kweli anapatia mutu utajiri na vitu vya kimwili na utukufu, na hivyo mutu hakose kitu chochote chenye anatamani;* lakini Mungu wa kweli hamuwezeshe kuvifurahia, hata kama mugeni anaweza kuvifurahia. Jambo hili ni bure* na ni mateso makubwa. 3 Kama mwanaume anazaa watoto mia moja (100) na kuishi miaka mingi na kuzeeka, lakini hafurahie* vitu vyake vya muzuri mbele aingie katika kaburi,* ninapaswa kusema kwamba mutoto mwenye alizaliwa akiwa amekufa anashindia mwanaume huyo.+ 4 Kwa maana mutoto huyo alikuja bure na kuenda katika giza, na jina lake limefunikwa katika giza. 5 Hata kama hakuona jua wala kujua kitu, anashindia* tu mwanaume huyo.+ 6 Kuko faida gani kuishi miaka elfu moja (1 000) mara mbili bila kuwa na furaha? Je, wote hawaende mahali pamoja?+

7 Kazi yote ya nguvu yenye mutu anafanya ni kwa ajili ya kujaza kinywa chake;+ lakini hamu yake ya kula* haitoshelezwe hata kidogo. 8 Kwa maana mwenye hekima anamupita mujinga kwa njia gani,+ ao mutu maskini anapata faida gani kwa sababu ya kujua kupambana na maisha?* 9 Ni muzuri zaidi kufurahia mambo yenye macho yanaona kuliko mutu kuhangaikia tamaa zake.* Jambo hili pia ni bure,* ni kufuatilia upepo.

10 Kila kitu chenye kiko kimekwisha kupewa jina, na inajulikana mwanadamu ni nini; na hawezi kubishana na* ule mwenye kuwa na nguvu kuliko yeye. 11 Wingi wa maneno,* ni wingi wa mambo ya bure;* na maneno mengi yanamuletea mwanadamu faida gani? 12 Ni nani anajua jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kufanya katika siku kidogo za maisha yake ya bure,* yenye anapitisha kama kivuli?+ Kwa maana ni nani anaweza kumuambia mambo yenye yatatokea chini ya jua kisha yeye kufa?

7 Jina la muzuri* linashindia mafuta ya muzuri,+ na siku ya kufa inashindia siku ya kuzaliwa. 2 Ni muzuri zaidi kuenda katika nyumba ya maombolezo kuliko kuenda katika nyumba ya karamu,+ kwa sababu huo ndio mwisho wa kila mwanadamu, na wenye kuwa wazima wanapaswa kuweka jambo hilo katika moyo. 3 Taabu inashindia kicheko,+ kwa maana huzuni ya uso inafanya moyo ukuwe muzuri zaidi.+ 4 Moyo wa mwenye hekima uko katika nyumba ya maombolezo, lakini moyo wa mujinga uko katika nyumba ya shangwe.*+

5 Ni muzuri zaidi kusikiliza karipio la mutu mwenye hekima+ kuliko kusikiliza wimbo wa wapumbavu. 6 Kwa maana kicheko cha mupumbavu ni kama mulio wa miiba yenye kuteketea kwa moto chini ya chungu;+ na jambo hili pia ni bure.* 7 Lakini kukandamizwa kunaweza kumufanya mutu mwenye hekima akuwe wazimu, na rushwa* inapotosha moyo.+

8 Mwisho wa jambo ni muzuri zaidi kuliko mwanzo wake. Ni muzuri zaidi kuwa muvumilivu kuliko kuwa na roho yenye majivuno.+ 9 Usikuwe haraka kukasirika,*+ kwa maana kukasirika kunakaa katika kifua cha wapumbavu.*+

10 Usiseme: “Sababu gani siku za zamani zilikuwa muzuri zaidi kuliko siku hizi?” kwa maana haiko hekima ndiyo inakufanya uulize vile.+

11 Hekima pamoja na uriti ni kitu kizuri na ni faida kwa wale wenye wanaona mwangaza wa siku.* 12 Kwa maana hekima ni ulinzi+ kama vile feza ni ulinzi,+ lakini faida ya ujuzi ni hii: Hekima inalinda uzima wa mwenye kuwa nayo.+

13 Fikiria kazi ya Mungu wa kweli, kwa maana ni nani anaweza kunyoosha kile chenye amekunja?+ 14 Katika siku ya muzuri, fikiria wema wake,+ lakini katika siku ya taabu,* kumbuka kwamba Mungu ameifanya hii sawa na ile ingine,+ ili wanadamu wasijue kwa hakika* kile kitawapata wakati wenye kuja.+

15 Katika maisha yangu ya bure*+ nimeona kila jambo⁠—​kuanzia mwenye haki+ mwenye anaangamia katika haki yake mupaka mutu muovu mwenye anaishi maisha ya murefu ijapokuwa ubaya wake.+

16 Usikuwe mwenye haki kupita kiasi,+ wala kujifanya mwenye hekima kupita kiasi.+ Sababu gani ulete uharibifu juu yako mwenyewe?+ 17 Usikuwe muovu kupita kiasi, wala usikuwe mupumbavu.+ Sababu gani ukufe mbele ya wakati wako?+ 18 Inafaa kutii onyo moja bila kuacha lingine;+ kwa maana mwenye anamuogopa Mungu atatii maonyo yote mbili.

19 Hekima inamufanya mutu mwenye hekima akuwe na nguvu zaidi kuliko watu kumi (10) wenye nguvu katika muji.+ 20 Kwa maana hakuna mwenye haki katika dunia mwenye anafanya mema sikuzote na hafanyake zambi.+

21 Tena, usiweke katika moyo kila neno lenye watu wanasema;+ ukifanya vile, unaweza kumusikia mutumishi wako akikusema mubaya;* 22 kwa maana unajua muzuri katika moyo wako kwamba wewe mwenyewe umesema wengine mubaya mara nyingi.+

23 Nilipima mambo hayo yote kwa hekima, na nilisema: “Nitakuwa na hekima.” Lakini sikuweza. 24 Mambo yenye yamekuja kuwa yako mbali sana na ni mazito sana. Ni nani anaweza kuelewa jambo hilo?+ 25 Nilielekeza moyo wangu ili kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na sababu yenye kufanya mambo yatokee, na kuelewa uovu wa upumbavu na ujinga wa wazimu.+ 26 Kisha nikavumbua hili: Mwanamuke mwenye kuwa kama wavu wa* muwindaji ni muchungu zaidi kuliko kifo, moyo wake ni kama nyavu za* kukokotwa, na mikono yake ni kama minyororo ya gereza. Mutu mwenye anamupendeza Mungu wa kweli anamuponyoka mwanamuke huyo,+ lakini mutenda-zambi ananaswa naye.+

27 “Angalia, hili ndilo jambo lenye nilivumbua,” ni vile mukutanishaji anasema.+ “Nilichunguza jambo moja kisha lingine ili kufikia uamuzi wangu, 28 lakini jambo lenye niliendelea* kutafuta, sikupata. Nilipata mwanaume mumoja* kati ya elfu moja (1 000), lakini sijapata mwanamuke kati yao. 29 Ni hili tu ndilo nimevumbua: Mungu wa kweli aliumba wanadamu wakiwa wanyoofu,+ lakini wao wenyewe wametafuta mipango mingi.”+

8 Ni nani mwenye kuwa kama mutu mwenye hekima? Ni nani anajua kutatua tatizo?* Hekima ya mutu inafanya uso wake ungae na inatuliza uso wake wenye ukali.

2 Ninasema: “Tii maagizo ya mufalme+ kwa sababu ya kiapo kwa Mungu.+ 3 Usiondoke haraka mbele yake.+ Usiunge mukono jambo lolote la mubaya;+ kwa maana anaweza kufanya kile anapenda, 4 kwa sababu neno la mufalme liko na nguvu;+ ni nani anaweza kumuambia: ‘Unafanya nini?’”

5 Mwenye anashika amri hataumia,+ na moyo wenye hekima utajua wakati na utaratibu wenye kufaa.*+ 6 Kwa maana kila jambo liko na wakati na utaratibu wake,*+ kwa sababu matatizo ya wanadamu ni mengi sana. 7 Kwa kuwa hakuna mwenye anajua mambo yenye yatatokea, ni nani anaweza kumuambia namna yatatokea?

8 Kama vile hakuna mutu mwenye kuwa na uwezo juu ya roho* ao mwenye anaweza kuzuia roho, vilevile hakuna mwenye kuwa na uwezo juu ya siku ya kifo.+ Kama vile hakuna mwenye anaruhusiwa kuondoka wakati wa vita, vilevile uovu hautaruhusu wale wenye wanazoea kuutenda waponyoke.*

9 Nimeona mambo haya yote, na nilichunguza katika moyo wangu kila kazi yenye imefanywa chini ya jua, wakati mwanadamu ametawala mwanadamu mwenzake ili kumuumiza.*+ 10 Na niliona waovu wakizikwa, watu wenye walizoea kuingia na kutoka mahali patakatifu, lakini walisahauliwa haraka katika muji kwenye walitenda vile.+ Jambo hili pia ni bure.*

11 Kwa sababu azabu haikutolewa haraka juu ya tendo la mubaya,+ moyo wa wanadamu hauogope kutenda mabaya.+ 12 Hata kama muovu anaweza kutenda mabaya mara mia moja (100) na kuendelea kuishi wakati murefu, lakini ninajua kwamba mambo yatawaendea muzuri wale wenye kumuogopa Mungu wa kweli, kwa sababu wanamuogopa.+ 13 Lakini mambo hayatamuendea muzuri muovu,+ wala hatarefusha siku zake zenye ziko kama kivuli,+ kwa sababu hamuogope Mungu.

14 Kuko jambo la bure* lenye linatendeka katika dunia: Kuko wenye haki wenye wanatendewa kama vile wamefanya mambo maovu,+ na kuko watu waovu wenye wanatendewa kama vile wametenda kwa haki.+ Ninasema kwamba jambo hili pia ni bure.*

15 Basi nikashauri watu wafurahi,+ kwa sababu chini ya jua hakuna jambo la muzuri zaidi kwa mwanadamu kuliko kula, kunywa, na kufurahi; anapaswa kufanya vile wakati anatumika sana sikuzote za maisha yake,+ zenye Mungu wa kweli amemupatia chini ya jua.

16 Nilijikaza sana katika moyo wangu ili kupata hekima na kuona kazi* yote yenye kufanywa katika dunia,+ hata nilikosa usingizi muchana na usiku.* 17 Basi nikafikiria kazi yote ya Mungu wa kweli, na nikavumbua kwamba wanadamu hawawezi kuelewa mambo yenye kufanyika chini ya jua.+ Hata kama watu wanajaribu kwa bidii namna gani, hawawezi kuyaelewa. Hata wakisema kwamba wako na hekima ya kutosha kuweza kujua, hawawezi kuyaelewa kabisa.+

9 Kwa hiyo nilitia mambo yote haya katika moyo wangu na kuona kwamba wenye haki na wenye hekima, na pia kazi zao, wako katika mikono ya Mungu wa kweli.+ Watu hawajue upendo ao chuki yenye ilifanywa mbele wakuwe. 2 Wote wanapatwa na jambo lilelile,*+ wenye haki na pia waovu,+ watu wazuri na safi na wale wenye hawako safi, wale wenye kutoa zabihu na wale wenye hawatoe zabihu. Mutu muzuri ni sawa na mutenda-zambi; mutu mwenye anaapa kiapo ni sawa na ule mwenye kuwa muangalifu kuhusu kuapa kiapo. 3 Hili ni jambo lenye kuhuzunisha lenye linatendeka chini ya jua: Kwa sababu wote wanapatwa na jambo lilelile,*+ moyo wa wanadamu umejaa ubaya; na kuko wazimu katika moyo wao wakati wa maisha yao, na kisha wanakufa!*

4 Kuko tumaini kwa mutu yeyote mwenye kuwa kati ya wazima, kwa sababu imbwa mwenye kuwa muzima anashindia simba mwenye amekufa.+ 5 Kwa maana wazima wanajua* kwamba watakufa,+ lakini wafu hawajue kitu chochote,+ wala hawana zawabu* tena, kwa sababu mambo yote yenye yanaweza kukumbukwa juu yao yamesahauliwa.+ 6 Tena, upendo wao na chuki yao na wivu wao tayari vimepotea, na hawawezi tena kushiriki katika mambo yenye kufanywa chini ya jua.+

7 Uende, ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo muchangamufu,+ kwa sababu tayari Mungu wa kweli amefurahia kazi zako.+ 8 Nguo zako zikuwe nyeupe,* na usikose kutia mafuta kwenye kichwa chako.+ 9 Furahia maisha pamoja na bibi yako mupendwa+ siku zote za maisha yako ya bure, zenye Yeye amekupatia chini ya jua, siku zako zote za maisha yako yenye kuwa bure,* kwa maana hilo ndilo fungu lako* katika maisha na katika kazi yako ya nguvu yenye unafanya kwa jasho chini ya jua.+ 10 Kila jambo lenye mukono wako unapata kufanya, ulifanye kwa nguvu zako zote, kwa sababu hakuna kazi wala mipango wala ujuzi wala hekima katika Kaburi,*+ mahali unaenda.

11 Nimeona jambo lingine chini ya jua, kwamba haiko wenye mbio ndio wanashinda kila mara katika mbio, wala haiko wenye nguvu ndio wanashinda katika vita,+ wala haiko wenye hekima ndio wanapata kila mara chakula, wala haiko wenye akili ndio wanakuwa kila mara na utajiri,+ wala haiko wenye ujuzi ndio wanafanikiwa kila mara,+ kwa sababu wakati na matukio yenye hayatazamiwe* yanafikia wote. 12 Kwa maana mwanadamu hajue wakati wake.+ Kama vile samaki wanakamatwa katika wavu* hatari na kama vile ndege wanakamatwa katika mutego, ni vile pia wana wa binadamu wananaswa wakati wa taabu,* wakati inawafikia bila kutazamia.

13 Niliona pia jambo hili kuhusu hekima chini ya jua⁠—​na lilinivutia: 14 Kulikuwa muji mudogo wenye watu kidogo; na mufalme mwenye nguvu alikuja kupigana nao na aliuzunguka na kutengeneza vitu vikubwa vya kutumia ili kuuzunguka kwa ajili ya vita. 15 Katika muji huo kulikuwa mutu fulani maskini lakini mwenye hekima, naye akaokoa muji huo kupitia hekima yake. Lakini hakuna mwenye alimukumbuka mutu huyo maskini.+ 16 Na nikasema katika moyo wangu: ‘Hekima inashindia nguvu;+ lakini hekima ya maskini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwe.’+

17 Ni muzuri zaidi kusikiliza maneno ya utulivu ya mwenye hekima kuliko makelele ya mutu mwenye kutawala kati ya wapumbavu.

18 Hekima inashindia silaha za vita, lakini mutenda-zambi mumoja tu anaweza kuharibu mambo mengi ya muzuri.+

10 Kama vile mainzi wenye kufa wanafanya mafuta ya mutengenezaji wa marashi yanuke na kutoa pofu, ni vile pia upumbavu kidogo unaharibu hekima na utukufu.+

2 Moyo wa mwenye hekima unamuongoza katika njia yenye inafaa,* lakini moyo wa mujinga unamuongoza katika njia yenye haifae.*+ 3 Katika kila njia yenye mupumbavu anatembea, hana akili ya muzuri,*+ na anafanya kila mutu ajue kwamba yeye ni mupumbavu.+

4 Kama kasirani* ya mutawala inawaka juu yako, usitoke mahali pako,+ kwa maana utulivu unatuliza zambi kubwa.+

5 Kuko jambo lenye kuhuzunisha lenye nimeona chini ya jua, kosa fulani lenye linafanywa na wenye mamlaka:+ 6 Upumbavu umepewa vyeo vingi vya juu, lakini matajiri* wanabakia katika vyeo vya chini.

7 Nimeona watumishi wakiwa kwenye migongo ya farasi lakini wakubwa wakitembea kwa miguu kama vile watumishi.+

8 Mwenye anachimba shimo anaweza kuangukia ndani;+ na mwenye anabomoa ukuta wa majiwe anaweza kuumwa na nyoka.

9 Mwenye anachimbua majiwe yatamuumiza, na mwenye anapasua vipande vikubwa vya muti anaweza kuwa katika hatari kwa sababu ya vipande hivyo.*

10 Kama kifaa cha chuma kinapoteza makali na kama mutu hakinoe, atahitaji kutumia nguvu nyingi zaidi. Lakini hekima inasaidia kupata mafanikio.

11 Kama nyoka anauma mbele ya kuchezeshwa, mutu mwenye kuchezesha nyoka mwenye ufundi* hapate faida yoyote.

12 Maneno yenye kutoka katika kinywa cha mwenye hekima yanafanya akubaliwe,+ lakini midomo ya mujinga ndiyo inamuharibu.+ 13 Maneno ya kwanza yenye kutoka katika kinywa chake ni upumbavu,+ na maneno yake ya mwisho ni wazimu wenye kuleta musiba. 14 Lakini mupumbavu anaendelea kusema.+

Mwanadamu hajue mambo yenye yatatokea; ni nani anaweza kumuambia mambo yenye yatakuja kisha yeye?+

15 Kazi ya nguvu ya mujinga inamuchokesha, kwa sababu hajue hata namna ya kupata njia ya kuenda katika muji.

16 Ole wake inchi wakati mufalme wake ni kijana+ na wakubwa wanaanza kufanya karamu asubui! 17 Heri inchi yenye mufalme wake ni mwana wa watu wenye vyeo na yenye wakubwa wake wanakula kwa wakati wenye unafaa ili kupata nguvu, haiko juu ya kulewa!+

18 Kwa sababu ya uvivu mukubwa sehemu ya juu ya nyumba inabonyea, na kwa sababu ya mikono yenye uvivu, nyumba inavuya.+

19 Mukate unafanywa* ili kuleta kicheko, na divai inafanya maisha yafurahishe;+ lakini feza zinatimiza mahitaji yote.+

20 Hata katika mawazo yako,* usilaani mufalme,*+ wala usilaani tajiri katika chumba chako cha kulala; kwa sababu ndege* anaweza kupeleka sauti,* ao kiumbe chenye mabawa kinaweza kurudilia mambo yenye yalisemwa.

11 Tupa* mukate wako juu ya maji,+ kwa maana kisha siku nyingi utaupata tena.+ 2 Patia fungu watu saba (7) ao hata munane (8),+ kwa maana haujue ni taabu gani itatokea* katika dunia.

3 Kama mawingu yanajaa maji, mvua itanyesha juu ya dunia; na kama muti unaanguka kuelekea kusini ao kaskazini, mahali kwenye muti unaangukia ni pale utabakia.

4 Mwenye anaangalia upepo hatapanda mbegu, na mwenye anaangalia mawingu hatavuna.+

5 Kama vile haujue namna roho inafanya kazi katika mifupa ya mutoto mwenye kuwa ndani ya* mwanamuke mwenye mimba,+ ni vile pia haujue kazi ya Mungu wa kweli, mwenye anafanya mambo yote.+

6 Panda mbegu zako asubui na usiache mukono wako upumuzike mupaka mangaribi;+ kwa maana haujue ni ya wapi itafanikiwa, kama ni hii ao ile, ao kama zote mbili zitakuwa muzuri.

7 Mwangaza ni mutamu, na ni muzuri kwa macho kuona jua. 8 Kwa maana kama mwanadamu anaishi miaka mingi, acha aifurahie yote.+ Lakini anapaswa kukumbuka kwamba siku za giza zinaweza kuwa nyingi; mambo yote yenye yatakuja ni bure.*+

9 Kijana, furahi wakati ungali kijana, na moyo wako ufurahi katika siku za ujana wako. Fuata njia za moyo wako na uende kwenye macho yako yanakuongoza; lakini ujue kwamba Mungu wa kweli atakuleta katika hukumu* kwa sababu ya mambo hayo yote.+ 10 Kwa hiyo ondoa katika moyo wako mambo yenye kuleta mahangaiko, na uepushe mwili wako na mambo yenye kuumiza, kwa maana ujana na kipindi kizuri cha maisha ni bure.*+

12 Basi, kumbuka Muumbaji wako Mukubwa katika siku za ujana wako,+ mbele siku za taabu* hazijakuja+ na mbele haijafika miaka yenye utasema: “Siifurahie”; 2 mbele ya jua na mwangaza na mwezi na nyota kuwa na giza,+ na mbele ya mawingu kurudia kisha* mvua kubwa; 3 siku yenye walinzi wa* nyumba wanatetemeka, na wanaume wenye nguvu wanainama, na wanamuke wanaacha kusaga kwa sababu wamekuwa kidogo, na mabibi wenye kuangalia kupitia madirisha wanaona giza;+ 4 wakati milango yenye inaelekea kwenye barabara imefungwa, wakati sauti ya jiwe la kusagia inapunguka, wakati mutu anaamushwa na sauti ya ndege, na mabinti wa wimbo wanazimia.+ 5 Tena, mutu anaogopa nafasi za juu, na kuko mambo yenye kuogopesha sana katika barabara. Na muti wa lozi unatoa maua,+ na panzi anajikokota, na tunda lenye kuleta hamu ya kula linapasuka,* kwa sababu mwanadamu anaenda kwenye nyumba yake ya kudumu+ na waombolezaji wanatembea huku na huku katika barabara;+ 6 mbele kamba ya feza haijaondolewa, na bakuli la zahabu kuvunjwa, na mutungi wenye kuwa kwenye chemchemi kuvunjwa, na gurudumu* la maji kwa ajili ya tangi kuvunjika. 7 Kisha mavumbi yanarudia kwenye udongo,+ kama vile yalikuwa, na roho* inarudia kwa Mungu wa kweli mwenye aliitoa.+

8 “Yote ni bure* kabisa!” ni vile mukutanishaji anasema,+ “Kila kitu ni bure.”+

9 Zaidi ya kuwa na hekima, mukutanishaji aliendelea kufundisha watu mambo yenye alijua,+ na alifikiri sana* na kuchunguza kwa uangalifu ili akusanye* mezali nyingi.+ 10 Mukutanishaji alijikaza kutafuta maneno yenye kupendeza+ na kuandika maneno ya kweli yenye hayana makosa.*

11 Maneno ya wenye hekima ni kama michokoo ya kuongozea ngombe,+ na semi zao zenye kukusanywa ni kama misumari yenye kupigiliwa kwa nguvu; yametolewa kutoka kwa muchungaji mumoja. 12 Kuhusu jambo lingine zaidi ya mambo haya, mwana wangu, ufanye angalisho: Hakuna mwisho wa kutunga vitabu vingi, na kujitoa sana kwa vitabu hivyo kunachokesha mwili.+

13 Huu ndio mwisho wa jambo, mambo yote yamekwisha kusikiwa: Ogopa Mungu wa kweli+ na ushike amri zake,+ kwa maana hilo ndilo jambo lote lenye mwanadamu anapaswa kufanya.+ 14 Kwa maana Mungu wa kweli atahukumu kila tendo, kutia ndani kila jambo lenye kufichwa, kama ni jambo la muzuri ao la mubaya.+

Ao “mwenye kukusanya watu; mwenye kuita watu kwenye mukusanyiko.”

Ao “ubatili.”

Tnn., “inasimama.”

Ao “linaangaza.”

Ao “Mito midogo ya kipindi cha baridi; Mito midogo yenye kutokea wakati fulani.”

Ao “ubatili.”

Ao “upumbavu mwingi sana.”

Ao “shangwe.”

Ao “ubatili.”

Ao “shangwe.”

Tnn., “wana wa nyumba.”

Ao “mali ya pekee kwa.”

Ao “bibi, ndiyo, mabibi.”

Tnn., “chenye macho yangu yaliomba.”

Ao “shangwe.”

Ao “fungu lenye.”

Ao “ubatili.”

Ao “chenye faida.”

Ao “Macho ya mutu mwenye hekima yako wazi.”

Ao “mwisho mumoja wenye unafikia.”

Ao “ubatili.”

Ao “ubatili.”

Ao “ubatili.”

Ao “kupatia kila kitu mutu mwenye hakukitumikia.”

Ao “ubatili.”

Ao “musiba mubaya sana.”

Tnn., “kujikaza kwa moyo wake.”

Ao “ubatili.”

Ao “ubatili.”

Tnn., “kuruka-ruka.”

Ao “chenye kupangwa muzuri; chenye kufaa.”

Ao pengine, “chenye kimepita.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “mwisho mumoja wenye unapata.”

Ao “ubatili.”

Ao “fungu lake.”

Ao “watumike sana.”

Ao “ubatili.”

Tnn., “na anakula nyama yake mwenyewe.”

Ao “ubatili.”

Ao “ubatili.”

Ao “faida kubwa.”

Ao “kwa vyepesi.”

Pengine ni ule mutoto mwenye hekima.

Ao “eko.”

Ao “ubatili.”

Ao “eko.”

Ao “mambo mengi sana ya kufanya.”

Tnn., “kifanye mwili wako.”

Ao “mujumbe.”

Ao “ubatili.”

Angalia Maana ya Maneno.

Ao “eko.”

Ao “ubatili.”

Ao “eko.”

Ao “musiba mubaya sana wenye.”

Ao “shuguli ya mubaya.”

Ao “musiba mubaya sana.”

Ao “hilo ndilo fungu lake.”

Ao “fungu lake.”

Ao “kukumbuka.”

Ao “musiba mwingine mubaya sana wenye.”

Ao “hakose kitu chochote kwa ajili ya nafsi yake.”

Ao “ubatili.”

Ao “nafsi yake haifurahie.”

Ao “na hata kaburi halijakuwa lake.”

Tnn., “iko na pumuziko zaidi kuliko.”

Ao “nafsi yake.”

Tnn., “kutembea mbele ya wazima.”

Tnn., “kutanga-tanga kwa nafsi.”

Ao “ubatili.”

Ao “kutetea jambo lake mbele ya.”

Ao pengine, “vitu.”

Ao “ubatili.”

Ao “ubatili.”

Ao “Sifa ya muzuri.” Tnn., “Jina.”

Ao “raha.”

Ao “ubatili.”

Ao “kata-midomo.”

Tnn., “Usikuwe haraka kukasirika katika roho yako.”

Ao pengine, “ni tabia ya mupumbavu.”

Ni kusema, wenye wako wazima.

Ao “musiba.”

Ao “wasivumbue.”

Ao “ubatili.”

Tnn., “akikulaani.”

Ao “makila ya.”

Ao “makila ya.”

Ao “nafsi yangu iliendelea.”

Ao “mwanaume munyoofu.”

Ao “kufasiria maana ya jambo.”

Ao “wakati na hukumu yenye kufaa.”

Ao “hukumu yake.”

Ao “pumuzi, upepo.”

Ao pengine, “uovu wao hauwezi kuokoa waovu.”

Ao “kumutendea mubaya; kumutesa.”

Ao “ubatili.”

Ao “lenye kuvunja moyo.”

Ao “ubatili.”

Ao “shuguli.”

Ao pengine, “kwamba watu hawapate usingizi ikuwe muchana ao usiku.”

Ao “mwisho uleule.”

Ao “mwisho uleule.”

Tnn., “na kisha hilo⁠—wanaenda kwa wafu!”

Ao “wanatambua.”

Ao “mushahara.”

Ni kusema, nguo zenye kungaa ambazo zinaonyesha hali ya furaha, hapana nguo za maombolezo.

Ao “siku zako za ubatili.”

Ao “sehemu yako.”

Ao “Sheoli,” ni kusema, kaburi la wanadamu wote. Angalia Maana ya Maneno.

Ao “matukio yenye hayakuwaziwa.”

Ao “makila.”

Ao “musiba.”

Tnn., “uko kwenye mukono wake wa kuume.”

Tnn., “uko kwenye mukono wake wa kushoto.”

Tnn., “moyo wake unakosewa.”

Tnn., “roho, pumuzi.”

Ao “wenye uwezo.”

Ao pengine, “anapaswa kufanya angalisho navyo.”

Tnn., “mwenye anajua sana kutumia ulimi.”

Ao “Chakula kinafanywa.”

Ao pengine, “kwenye kitanda chako.”

Ao “usiseme mufalme mubaya.”

Tnn., “kiumbe mwenye kuruka wa mbinguni.”

Ao “habari.”

Ao “Tuma.”

Ao “musiba gani utatokea.”

Tnn., “mifupa katika tumbo la uzazi la.”

Ao “ubatili.”

Ao “atakuomba utoe hesabu.”

Ao “ubatili.”

Ao “musiba.”

Ao pengine, “pamoja na.”

Ao “wenye kuchunga.”

Ni tunda lenye kuitwa capre.

Ao “mupeto; pneu.”

Ao “nguvu ya uzima.”

Ao “ubatili.”

Ao “alitafakari.”

Ao “apange kwa utaratibu.”

Ao “sahihi ya kweli.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine