Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • nwt Maombolezo 1:1-5:22
  • Maombolezo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maombolezo
  • Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Biblia—Tafsiri ya Ulimwengu Mupya
Maombolezo

MAOMBOLEZO

א [Aleph]*

1 Namna sasa amekaa akiwa peke yake, muji wenye ulikuwa umejaa watu!+

Namna amekuwa kama mujane, yeye mwenye alikuwa na watu wengi kati ya mataifa!+

Namna ule mwenye alikuwa binti ya kifalme kati ya majimbo* amewekwa kwenye kazi za kulazimishwa!+

ב [Beth]

 2 Analia sana usiku,+ na machozi yake yanafunika mashavu yake.

Hakuna mutu yeyote wa kumufariji kati ya wapenzi wake wote.+

Wenzake wote wamemusaliti;+ wamekuwa maadui wake.

ג [Gimel]

 3 Yuda ameenda katika uhamisho+ kwa mateso na utumwa mukali.+

Anapaswa kukaa kati ya mataifa;+ hapate mahali pa kupumuzikia.

Wote wenye kumutesa wamemufikia katika taabu yake.

ד [Daleth]

 4 Barabara za kuenda Sayuni zinaomboleza, kwa sababu hakuna mutu yeyote mwenye anakuja kwenye sikukuu.+

Milango yake yote mikubwa imekuwa ukiwa;+ makuhani wake wanalia kwa maumivu.

Mabikira wake* wako na huzuni, na yeye iko* katika uchungu mukali.

ה [He]

 5 Wapinzani wake wamekuwa sasa bwana wake;* maadui wake hawana mahangaiko.+

Kwa maana Yehova amemuletea huzuni kwa sababu ya makosa yake mengi.+

Watoto wake wameenda katika utekwa mbele ya adui.+

ו [Waw]

 6 Utukufu wote umetoka kwa binti ya Sayuni.+

Wakubwa wake wamekuwa kama paa wenye hawakupata malisho,

Na wanatembea wakiwa wenye kuchoka mbele ya mwenye kuwafuatilia.

ז [Zayin]

 7 Katika siku za mateso yake na za kukosa kuwa na makao, Yerusalemu anakumbuka

Vitu vyote vyenye samani vyenye vilikuwa vyake katika siku za zamani sana.+

Wakati watu wake walianguka katika mukono wa adui na hakukuwa na musaidizi,+

Maadui walimuona na wakacheka* juu ya kuanguka kwake.+

ח [Heth]

 8 Yerusalemu amefanya zambi sana.+

Ndiyo sababu amekuwa kitu chenye kuchukiza.

Wote wenye walikuwa wanamuheshimia wanamutendea sasa kama kitu cha kuzarauliwa, kwa maana wameona uchi wake.+

Yeye mwenyewe analia kwa maumivu+ na anageuka kwa haya.

ט [Teth]

 9 Uchafu wake uko katika nguo zake.

Hakufikiria wakati wake wenye kuja.+

Alianguka kwa njia ya kushangaza; hana mutu wa kumufariji.

Ee Yehova, ona mateso yangu, kwa maana adui amejitukuza mwenyewe.+

י [Yod]

10 Adui ametia mikono yake juu ya hazina zake zote.+

Kwa maana ameona mataifa yakiingia patakatifu pake,+

Watu wenye uliamuru wasiingie katika kutaniko lako.

כ [Kaph]

11 Watu wake wote wanalia kwa maumivu; wanatafuta mukate.+

Wametoa vitu vyao vyenye samani ili wapate chakula, ili tu waendelee kuishi.*

Angalia, Ee Yehova, na uone namna nimekuwa kama mwanamuke mwenye hana mafaa yoyote.*

ל [Lamed]

12 Je, haimaanishe kitu chochote kwenu ninyi wote wenye kupita katika barabara?

Muangalie na muone!

Je, kuko maumivu yoyote kama maumivu yenye nimetendewa,

Yenye Yehova amefanya nipate katika siku ya kasirani yake yenye kuwaka?+

מ [Mem]

13 Kutoka juu ametuma moto katika mifupa yangu,+ na anatiisha kila mumoja.

Ametandika wavu* kwa ajili ya miguu yangu; amenilazimisha nigeuke na nirudie nyuma.

Amenifanya kuwa mwanamuke mwenye ameachwa ukiwa.

Niko mugonjwa muchana wote.

נ [Nun]

14 Makosa yangu yamefungwa kama nira, yamefungwa pamoja kwa mukono wake.

Yamewekwa kwenye shingo yangu, na nguvu zangu zimeisha.

Yehova amenitia katika mukono wa watu wenye siwezi kupingana nao.+

ס [Samekh]

15 Yehova ametupa pembeni watu wote wenye nguvu kutoka katikati yangu.+

Ameita mukusanyiko juu yangu ili kuponda vijana wangu wanaume.+

Yehova amemukanyanga binti bikira wa Yuda katika kikamulio cha divai.+

ע [Ayin]

16 Ninalia kwa sababu ya mambo hayo;+ macho yangu yanatiririka machozi.

Kwa maana mutu yeyote mwenye angenifariji ao kunitia moyo* iko* mbali sana na mimi.

Watoto wangu wameachwa ukiwa, kwa sababu adui ameshinda.

פ [Pe]

17 Sayuni amenyoosha mikono yake,+ hana mutu wa kumufariji.

Yehova ametoa amri juu ya Yakobo kwa maadui wake wote wenye kumuzunguka.+

Yerusalemu imekuwa kwao kitu chenye kuchukiza.+

צ [Tsade]

18 Yehova ni mwenye haki,+ kwa maana nimeasi amri zake.*+

Musikilize, ninyi vikundi vyote vya watu, na muone maumivu yangu.

Mabikira wangu* na vijana wangu wanaume wameenda katika utekwa.+

ק [Qoph]

19 Nimeita wapenzi wangu kwa sauti kubwa, lakini wamenisaliti.+

Katika muji makuhani wangu na wazee wangu wameangamia,

Wakati walitafuta chakula ili waendelee kuishi.*+

ר [Resh]

20 Ona, Ee Yehova, kwa maana niko katika taabu kali.

Sehemu zangu za ndani zinavurugika.*

Moyo wangu umepinduka ndani yangu, kwa maana nimeasi kabisa.+

Inje upanga unaua watu;+ ndani ya nyumba ni kama kifo.

ש [Shin]

21 Watu wamesikia kilio changu cha maumivu; hakuna mutu wa kunifariji.

Maadui wangu wote wamesikia juu ya musiba wangu.

Wanafurahi, kwa sababu uliuleta.+

Lakini utaleta siku yenye ulitangaza,+ wakati watakuwa kama mimi.+

ת [Taw]

22 Uovu wao wote ukuje mbele yako, na uwatendee kwa ukali,+

Kama vile umenitendea kwa ukali kwa sababu ya makosa yangu yote.

Kwa maana vilio vyangu vya maumivu ni vingi, na moyo wangu ni mugonjwa.

א [Aleph]

2 Namna Yehova amefunika binti ya Sayuni katika wingu la kasirani yake!

Ametupa chini uzuri wa Israeli kutoka mbinguni mupaka duniani.+

Hakukumbuka kiti cha miguu yake+ katika siku ya kasirani yake.

ב [Beth]

 2 Yehova amemeza bila huruma makao yote ya Yakobo.

Katika kasirani yake amebomoa ngome za binti ya Yuda.+

Ameangusha chini na kuchafua ufalme+ na wakubwa wake.+

ג [Gimel]

 3 Katika joto kali la kasirani amekata nguvu zote* za Israeli.

Alirudisha mukono wake wa kuume wakati adui alikaribia,+

Na katika Yakobo aliendelea kuwaka kama moto wenye unateketeza kila kitu kuuzunguka.+

ד [Daleth]

 4 Amekunja* upinde wake kama adui; na kama mupinzani, ametayarisha mukono wake wa kuume ili kushambulia;+

Aliendelea kuua wote wenye kupendeza macho.+

Na amemwanga kasirani yake kali kama moto+ katika hema ya binti ya Sayuni.+

ה [He]

 5 Yehova amekuwa kama adui;+

Amemeza Israeli.

Amemeza minara yake yote;

Ameharibu mahali pake pote penye ngome.

Na katika binti ya Yuda anafanya kilio na maombolezo viongezeke.

ו [Waw]

 6 Anatendea kibanda chake kwa jeuri,+ kama kibanda chenye kuwa katika bustani.

Amemaliza* sikukuu yake.+

Yehova amefanya sikukuu na sabato zisahauliwe katika Sayuni,

Na katika kasirani yake kali haheshimie mufalme na kuhani.+

ז [Zayin]

 7 Yehova amekataa mazabahu yake;

Amekataa patakatifu pake.+

Ametoa kuta za minara yake yenye ngome katika mukono wa adui.+

Wamepandisha sauti yao katika nyumba ya Yehova,+ kama katika siku ya sikukuu.

ח [Heth]

 8 Yehova ameazimia kuharibu ukuta wa binti ya Sayuni.+

Amenyoosha kamba ya kupimia.+

Hakurudisha mukono wake nyuma ili asilete uharibifu.*

Na anafanya boma na ukuta viomboleze.

Vyote pamoja vimeregezwa.

ט [Teth]

 9 Milango yake mikubwa imezama katika udongo.+

Ameharibu na kuvunja mapingo* yake.

Mufalme wake na wakubwa wake wako kati ya mataifa.+

Hakuna sheria;* hata manabii wake hawapate maono kutoka kwa Yehova.+

י [Yod]

10 Wazee wa binti ya Sayuni wamekaa chini kimya.+

Wanatupa mavumbi kwenye vichwa vyao na kuvaa nguo za magunia.+

Mabikira wa Yerusalemu wameinamisha vichwa vyao mupaka chini.

כ [Kaph]

11 Macho yangu yamechoka kwa sababu ya kutoa machozi.+

Sehemu zangu za ndani zinavurugika.*

Ini langu limemwangwa chini kwa sababu ya kuangamizwa kwa binti* ya watu wangu,+

Kwa sababu watoto na watoto wadogo wanazimia katika viwanja vya watu wote vya muji.+

ל [Lamed]

12 Wanaendelea kuuliza mama zao: “Nafaka na divai viko wapi?”+

Wakati wanazimia kama mutu mwenye aliumizwa katika viwanja vya watu wote vya muji,

Wakati uzima wao unapotea* katika mikono ya mama zao.

מ [Mem]

13 Ninaweza kutumia nini kama shahidi,

Ao ninaweza kukufananisha na nini, Ee binti ya Yerusalemu?

Ninaweza kukulinganisha na nini, ili kukufariji, Ee binti bikira wa Sayuni?

Kwa maana muvunjiko wako ni mukubwa kama bahari.+ Ni nani anaweza kukuponyesha?+

נ [Nun]

14 Maono yenye manabii wako waliona kwa ajili yako yalikuwa ya uongo na yenye hayana maana,+

Na hawakufunua kosa lako ili usipelekwe katika utekwa,+

Lakini waliendelea kuona kwa ajili yako maono ya matangazo ya uongo na yenye kupotosha.+

ס [Samekh]

15 Wale wote wenye kupita katika barabara wanapiga mikono ili kukuchekelea.+

Wanapiga muluzi kwa mushangao+ na kutikisa vichwa vyao juu ya binti ya Yerusalemu, na kusema:

“Je, huu ndio muji wenye walikuwa wanasema juu yake, ‘Unakamilika katika uzuri, furaha ya dunia yote’?”+

פ [Pe]

16 Maadui wako wote wamefungua kinywa chao juu yako.

Wanapiga muluzi na kusaga meno yao na kusema: “Tumemumeza.+

Hii ndiyo siku yenye tulikuwa tunangojea!+ Imefika, na tumeiona!”+

ע [Ayin]

17 Yehova amefanya jambo lenye alikusudia;+ ametimiza neno lake,+

Lenye aliamuru tangu zamani.+

Amebomoa bila huruma.+

Amefanya adui afurahi juu yako; ameinua nguvu* za wapinzani wako.

צ [Tsade]

18 Moyo wao unamulilia Yehova, Ee ukuta wa binti ya Sayuni.

Acha machozi yatiririke kama muto mudogo muchana na usiku.

Usijipatie pumuziko, usipatie jicho lako* pumuziko.

ק [Qoph]

19 Simama! Lia wakati wa usiku, kwenye mwanzo wa makesha.

Mwanga moyo wako kama maji mbele ya uso wa Yehova.

Inua mikono yako kwake kwa ajili ya uzima* wa watoto wako,

Wenye wanazimia kwenye kila pembe* ya barabara kwa sababu ya njaa.+

ר [Resh]

20 Ona, Ee Yehova, na uangalie ule mwenye ulitendea kwa ukali hivi.

Je, wanamuke waendelee kula uzao wao* wenyewe, watoto wao wenyewe wenye afya ya muzuri kabisa,+

Ao, je, makuhani na manabii wauawe katika patakatifu pa Yehova?+

ש [Shin]

21 Kijana mudogo na mwanaume muzee wamelala chini wakiwa wamekufa katika barabara.+

Mabikira wangu* na vijana wangu wanaume wameanguka kwa upanga.+

Umeua katika siku ya kasirani yako; umechinja bila huruma.+

ת [Taw]

22 Kama vile kwa ajili ya siku ya sikukuu,+ unaita woga kutoka kila mahali.

Katika siku ya kasirani kali ya Yehova, hakuna mutu yeyote mwenye alitoroka wala kuokoka;+

Wale wenye nilizaa* na kulea, adui yangu aliwaharibu.+

א [Aleph]

3 Mimi ndiye mutu mwenye ameona mateso kwa sababu ya fimbo ya kasirani yake kali.

 2 Amenifukuza inje na ananitembeza katika giza, hapana katika mwangaza.+

 3 Kwa kweli, analeta mukono wake tena na tena juu yangu siku nzima.+

ב [Beth]

 4 Ameharibisha nyama na ngozi yangu;

Amevunja mifupa yangu.

 5 Amenizunguka kwa ajili ya vita; amenizungusha sumu yenye uchungu,+ na magumu.

 6 Amenilazimisha nikae mahali kwenye giza, kama watu wenye walikufa zamani.

ג [Gimel]

 7 Amenizungushia ukuta, ili nisiweze kutoroka;

Amenifunga kwa pingu nzito za shaba.+

 8 Na wakati ninalia kwa sauti kubwa ili kuomba musaada bila tumaini, anakataa* sala yangu.+

 9 Amefunga njia zangu kwa majiwe yenye kuchongwa;

Amefanya njia zangu zikuwe zenye kujikunja.+

ד [Daleth]

10 Anavizia ili kunishambulia kama dubu, kama simba katika mahali pa kujificha.+

11 Amenitosha kinguvu katika njia na kunikata vipande-vipande;*

Amenifanya nibakie ukiwa.+

12 Amekunja* upinde wake, na ananifanya nikuwe shabaha ya mushale wake.

ה [He]

13 Ametoboa figo zangu kwa mishale* ya mufuko wake wa mishale.

14 Nimekuwa kitu cha kuchekwa kwa vikundi vyote vya watu, nimekuwa kichwa cha wimbo wao siku nzima.

15 Amenishibisha vitu vichungu na kunijaza pakanga.+

ו [Waw]

16 Anavunja meno yangu kwa majiwe ya kidogo-kidogo;

Ananifanya nijikunje katika majivu.+

17 Unaniima* amani; nimesahau mambo ya muzuri.

18 Kwa hiyo ninasema: “Utukufu wangu umeangamia, na pia tazamio langu katika Yehova.”

ז [Zayin]

19 Kumbuka mateso yangu na hali yangu ya kukosa makao,+ pakanga na sumu yenye uchungu.+

20 Hakika wewe utanikumbuka* na kuinama juu yangu.+

21 Ninakumbuka hili katika moyo wangu; ndiyo sababu nitaonyesha mutazamo wa kungojea.+

ח [Heth]

22 Ni kwa sababu ya upendo mushikamanifu wa Yehova ndiyo maana hatukuisha,+

Kwa maana hakuna siku rehema zake zitafikia mwisho.+

23 Ni za mupya kila asubui;+ uaminifu wako ni mwingi.+

24 “Yehova ni fungu langu,”+ ni vile nimesema,* “ndiyo sababu nitaonyesha mutazamo wa kumungojea.”+

ט [Teth]

25 Yehova ni mwema kwa ule mwenye anamutumainia,+ kwa mutu mwenye anaendelea* kumutafuta.+

26 Ni muzuri kungojea kimya-kimya*+ wokovu wa Yehova.+

27 Ni muzuri kwa mwanaume kubeba nira wakati wa ujana wake.+

י [Yod]

28 Akae peke yake na abakie kimya wakati Yeye anaiweka juu yake.+

29 Atie kinywa chake katika mavumbi;+ pengine kungali tumaini.+

30 Apatie shavu lake mutu mwenye kumupiga; na apate kipimo chake kamili cha matusi.

כ [Kaph]

31 Kwa maana Yehova hatatutupa milele.+

32 Hata kama ameleta huzuni, ataonyesha pia rehema kulingana na wingi wa upendo wake mushikamanifu.+

33 Kwa maana haiko kutoka katika moyo wake kwamba atese ao ahuzunishe wana wa binadamu.+

ל [Lamed]

34 Kuponda chini ya miguu ya mutu wafungwa wote wa dunia,+

35 Kuima mutu haki mbele ya Mwenye Kuwa Juu Zaidi,+

36 Kutendea mutu kwa udanganyifu katika kesi yake ya hukumu

—Yehova havumilie mambo hayo.

מ [Mem]

37 Basi, ni nani mwenye anaweza kusema, na jambo hilo litendeke isipokuwa Yehova analiamuru?

38 Kutoka katika kinywa cha Mwenye Kuwa Juu Zaidi,

Mambo ya mubaya na mambo ya muzuri hayatoke pamoja.

39 Sababu gani mutu mwenye uzima atoe malalamiko kuhusu matokeo ya zambi yake?+

נ [Nun]

40 Tuchunguze njia zetu na kuzichunguza kwa uangalifu,+ na tumurudilie Yehova.+

41 Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mwenye kuwa mbinguni:+

42 “Tumekosea na kuasi,+ na haukusamehe.+

ס [Samekh]

43 Kwa kasirani umetuzuia tusikukaribie;+

Umetufuatilia na kutuua bila huruma.+

44 Umeweka kizuizi cha wingu ili usiweze kufikiwa, ili sala yetu isipite ndani.+

45 Unatufanya kuwa takataka na uchafu kati ya vikundi vya watu.”

פ [Pe]

46 Maadui wetu wote wanafungua vinywa vyao juu yetu.+

47 Woga na mashimo vimekuwa fungu letu,+ ukiwa na kuvunjika.+

48 Mito midogo ya maji inatiririka kutoka kwenye macho yangu juu ya kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+

ע [Ayin]

49 Macho yangu yanalia bila kuacha, bila kupumuzika,+

50 Mupaka Yehova aangalie chini na aone kutoka mbinguni.+

51 Macho yangu yameniletea* huzuni kwa sababu ya mabinti wote wa muji wangu.+

צ [Tsade]

52 Maadui wangu wameniwinda bila sababu kama ndege.

53 Wamenyamazisha uzima wangu katika shimo; waliendelea kunitupia majiwe.

54 Maji yalitiririka juu ya kichwa changu, na nikasema: “Nimeisha!”

ק [Qoph]

55 Niliita jina lako, Ee Yehova, kutoka sehemu za chini kabisa za shimo.+

56 Sikiliza sauti yangu; usifunge sikio lako kwa kilio changu cha kuomba musaada, cha kuomba kitulizo.

57 Ulikaribia katika siku yenye nilikuita. Ulisema: “Usiogope.”

ר [Resh]

58 Umetetea kesi zangu za hukumu,* Ee Yehova, umekomboa uzima wangu.+

59 Umeona, Ee Yehova, kosa lenye nilitendewa; tafazali unipatie haki.+

60 Umeona kisasi chao chote, mipango yote ya mubaya yenye walifanya juu yangu.

ש [Sin] ao [Shin]

61 Umesikia zihaka zao, Ee Yehova, mipango yote ya mubaya yenye walifanya juu yangu,+

62 Midomo ya wapinzani wangu na namna wananisema kwa sauti ya chini-chini siku nzima.

63 Uwaangalie; kama wanakaa ao wanasimama, wananichekelea katika nyimbo zao!

ת [Taw]

64 Utawalipa, Ee Yehova, kulingana na matendo yao.

65 Utafanya mioyo yao kuwa migumu, na hiyo ikuwe laana yako kwao.

66 Utawafuatilia katika kasirani yako na kuwaharibu kutoka chini ya mbingu za Yehova.

א [Aleph]

4 Namna zahabu yenye kungaa imepoteza uangavu, zahabu safi!+

Namna majiwe matakatifu+ yamesambaa kwenye kila pembe ya barabara!*+

ב [Beth]

 2 Na wana wa Sayuni wenye samani, wenye walipimwa uzito kwa kulinganishwa na* zahabu yenye kusafishwa,

Namna wameonwa kama mitungi ya udongo,

Kazi ya mikono ya mufinyanzi!*

ג [Gimel]

 3 Hata mbweha wanatoa maziwa ili kunyonyesha watoto wao,

Lakini binti ya watu wangu amekuwa bila huruma,+ kama mbuni katika jangwa.+

ד [Daleth]

 4 Ulimi wa mutoto mudogo mwenye kunyonya umebana kwenye kaakaa* lake kwa sababu ya kiu.

Watoto wanaomba mukate,+ lakini hakuna mwenye anawapatia hata mukate mumoja.+

ה [He]

 5 Wale wenye walikuwa wanakula vyakula vitamu wamelala katika barabara wakiwa na njaa.*+

Wale wenye walilelewa wakiwa wanavaa nguo za rangi nyekundu yenye kungaa+ wamekumbatia marundo ya majivu.

ו [Waw]

 6 Azabu ya* binti ya watu wangu ni kubwa kuliko azabu ya zambi ya Sodoma,+

Muji wenye uliharibiwa kwa wakati kidogo, bila mukono wowote wa kuusaidia.+

ז [Zayin]

 7 Wanaziri+ wake walikuwa safi kuliko teluji,* weupe kuliko maziwa.

Walikuwa wekundu kuliko marijani; walikuwa kama yakuti zenye zilingarishwa.

ח [Heth]

 8 Wameonekana kuwa weusi kuliko masisi;*

Hawatambuliwe katika barabara.

Ngozi yao imekauka juu ya mifupa yao;+ imekuwa kama kuni yenye kukauka.

ט [Teth]

 9 Wale wenye waliuawa kwa upanga ni afazali kuliko wale wenye waliuawa kwa njaa,+

Wale wenye wanaishiwa nguvu, wenye wametobolewa kwa kukosa chakula katika shamba.

י [Yod]

10 Mikono ya wanamuke wenye huruma imetokotesha watoto wao wenyewe.+

Wamekuwa chakula chao cha maombolezo wakati wa kuvunjika kwa binti ya watu wangu.+

כ [Kaph]

11 Yehova ameonyesha kasirani yake kali;

Amemwanga hasira yake yenye kuwaka.+

Na anawasha katika Sayuni moto wenye unateketeza misingi yake.+

ל [Lamed]

12 Wafalme wa dunia na wakaaji wote wa inchi yenye kuzaa hawakuamini

Kwamba mupinzani na adui wangeingia kwenye milango mikubwa ya Yerusalemu.+

מ [Mem]

13 Ilikuwa kwa sababu ya zambi za manabii wake, makosa ya makuhani wake,+

Wenye walimwanga damu ya wenye haki katikati yake.+

נ [Nun]

14 Wametanga-tanga kama vipofu+ katika barabara.

Wamechafuliwa na damu,+

Na hivyo hakuna mutu mwenye anaweza kugusa nguo zao.

ס [Samekh]

15 “Mutoke! Ninyi wachafu!” ni vile wanasema nao kwa sauti kubwa. “Mutoke! Mutoke! Musituguse!”

Kwa maana wamekuwa bila makao na wanatanga-tanga.

Watu wamesema kati ya mataifa: “Hawawezi kukaa hapa pamoja na sisi.*+

פ [Pe]

16 Uso wa Yehova umewatawanya;+

Hatawakubali tena.

Watu hawataheshimia makuhani,+ hawataonyesha wazee wema.”+

ע [Ayin]

17 Hata sasa macho yetu yamechoka kutafuta musaada lakini haupatikane.+

Tuliangalia na kutafuta musaada kutoka kwa taifa lenye halingeweza kutuokoa.+

צ [Tsade]

18 Wametuwinda katika kila hatua+ na hivyo hatungeweza kutembea katika viwanja vyetu vya watu wote.

Mwisho wetu umekaribia; siku zetu zimeisha, kwa maana mwisho wetu umekuja.

ק [Qoph]

19 Wenye kutufuatilia walikuwa wanaenda haraka kuliko tai wa anga.+

Walitufuatilia katika milima; walituvizia katika jangwa.

ר [Resh]

20 Pumuzi ya matundu ya pua zetu, mutiwa-mafuta wa Yehova,+ amenaswa katika shimo lao kubwa,+

Ule mwenye tulisema hivi juu yake: “Tutaishi chini ya kivuli chake kati ya mataifa.”

ש [Sin]

21 Furahi na kushangilia, Ee binti ya Edomu,+ mwenye kukaa katika inchi ya Usi.

Lakini kwako pia kikombe kitapita,+ na utalewa na kufunua uchi wako.+

ת [Taw]

22 Azabu ya kosa lako, Ee binti ya Sayuni, imefikia mwisho wake.

Hatakupeleka tena katika uhamisho.+

Lakini atageuza uangalifu wake kwenye kosa lako, Ee binti ya Edomu.

Atafunua zambi zako.+

5 Kumbuka, Ee Yehova, mambo yenye yalitupata.

Angalia na uone haya yetu.+

 2 Uriti wetu umeenda kwa wageni, nyumba zetu kwa watu wa inchi ingine.+

 3 Tumekuwa mayatima wenye hawana baba; mama zetu ni kama wajane.+

 4 Tunapaswa kununua maji yetu wenyewe ya kunywa,+ na kuni zetu wenyewe zinakuja kwa bei.

 5 Wale wenye kutufuatilia wako kwenye shingo yetu;

Tumechoka, lakini hatupewe pumuziko lolote.+

 6 Tunanyooshea mukono wetu Misri+ na Ashuru,+ ili tupate mukate wa kutosha wa kula.

 7 Mababu zetu wenye walifanya zambi hawako tena, lakini tunapaswa kubeba makosa yao.

 8 Sasa watumishi wanatawala juu yetu; hakuna wa kututosha katika mukono wao.

 9 Tunaleta mukate wetu kwa kutia uzima wetu* katika hatari,+ kwa sababu ya upanga wa jangwa.

10 Ngozi yetu imekuwa moto kama tanuru, kwa sababu ya maumivu ya njaa.+

11 Bibi katika Sayuni wamepatishwa haya,* mabikira katika miji ya Yuda.+

12 Wakubwa walitundikwa kwa mukono wao,+ na wazee hawakuonyeshwa heshima yoyote.+

13 Vijana wanaume wanabeba jiwe la kusagia la mukono, na watoto wanaume wanajikwaa chini ya mizigo ya kuni.

14 Wazee wametoka kwenye mulango mukubwa wa muji;+ vijana wanaume hawapige muziki wao.+

15 Furaha imepotea katika moyo wetu; dansi zetu zimegeuka kuwa maombolezo.+

16 Taji limeanguka kutoka kwenye kichwa chetu. Ole wetu, kwa sababu tumefanya zambi!

17 Kwa sababu hiyo moyo wetu umegonjwa,+

Na kwa sababu ya mambo haya macho yetu yamefifia,+

18 Kwa sababu ya Mulima Sayuni, wenye umekuwa ukiwa;+ sasa mbweha wanatembea-tembea juu yake.

19 Sasa wewe, Ee Yehova, unakaa kwenye kiti cha ufalme milele.

Kiti chako cha ufalme ni cha kizazi kwa kizazi.+

20 Sababu gani unatusahau milele na kutuacha kwa wakati murefu hivi?+

21 Uturudishe kwako, Ee Yehova, na sisi tutarudia kwako kwa kupenda.+

Fanya siku zetu zikuwe mupya kama katika siku za zamani sana.+

22 Hata hivyo, umetukataa kabisa.

Ungali unatukasirikia sana.+

Sura ya 1-4 ni nyimbo za maombolezo zenye ziliandikwa kwa kufuata alfabeti ya Kiebrania ao mupangilio wa kishairi.

Ao “wilaya za utawala.”

Ao “Vijana wake wanamuke.”

Ao “eko.”

Tnn., “kichwa chake.”

Ao “wakashangilia.”

Ao “ili tu kurudisha nafsi.”

Maneno haya yanahusu muji wa Yerusalemu wenye unazungumuziwa kama mutu.

Ao “makila.”

Ao “kutia moyo nafsi yangu.”

Ao “eko.”

Tnn., “kinywa chake.”

Ao “Vijana wangu wanamuke.”

Ao “ili kurudisha nafsi.”

Tnn., “Matumbotumbo yangu yanavurugika.”

Tnn., “kila pembe.”

Tnn., “Amekanyanga.”

Ao “Ameharibu.”

Tnn., “asimeze.”

Pingo ni kipande cha muti ao cha chuma cha kufungia mulango kwa ndani.

Ao “agizo.”

Tnn., “Matumbotumbo yangu yanavurugika.”

Maneno ya kishairi yenye kuzungumuzia vitu kama watu, pengine yanaonyesha huruma ao sikitiko.

Ao “nafsi yao inapotea.”

Tnn., “pembe.”

Tnn., “binti ya jicho lako.”

Ao “nafsi.”

Tnn., “kwenye kichwa cha kila barabara.”

Ao “matunda yao.”

Ao “Vijana wangu wanamuke.”

Ao “wenye nilizaa wakiwa na afya ya muzuri.”

Ao “anazuia; anafungia.”

Ao pengine, “kuniachilia nikuwe bure.”

Tnn., “Amekanyanga.”

Tnn., “wana.”

Ao “Unaima nafsi yangu.”

Ao “nafsi yako itanikumbuka.”

Ao “nafsi yangu imesema.”

Ao “kwa nafsi yenye inaendelea.”

Ao “kungojea kwa uvumilivu.”

Ao “yameletea nafsi yangu.”

Ao “kesi za hukumu za nafsi yangu.”

Tnn., “kwenye kichwa cha kila barabara.”

Ao “walikuwa wenye samani kama.”

Angalia Maana ya Maneno.

Kaakaa ni sehemu ya juu ndani ya kinywa.

Tnn., “wakiwa ukiwa.”

Tnn., “Kosa la.”

Ao “neige.”

Tnn., “weusi.”

Ao “Hawawezi kukaa hapa wakiwa wageni.”

Ao “nafsi yetu.”

Ao “wamelalwa kinguvu.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine