Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w11 1/10 uku. 3
  • Je, Wewe Umedanganywa?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je, Wewe Umedanganywa?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Matokeo ya Mubaya Sana ya Uongo wa Kwanza
    Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha ya Mukristo—2020
  • Petro na Anania Walisema Uongo—Tunaweza Kujifunza Somo Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Utoaji Mbalimbali
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Wakati Mutoto Wako Anasema Uongo
    Amuka!—2014
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
w11 1/10 uku. 3

Je, Wewe Umedanganywa?

NI MAMBO machache yanayoumiza zaidi kuliko kujua kwamba mtu fulani unayemwamini amekudanganya. Unaweza kukasirika, kuhisi umedharauliwa au hata kusalitiwa. Udanganyifu unavunja urafiki na ndoa; na unafanya watu wapoteze mamilioni ya pesa.

Basi, wazia jinsi ambavyo ungehisi kama ungejua kwamba umedanganywa kumhusu Mungu. Ikiwa unamwogopa Mungu, matokeo yanaweza kuwa mabaya kama ilivyokuwa kwa watu wafuatao ambao walikuwa wafuasi wa dini:

● “Nilihisi kwamba nimesalitiwa na kanisa.”—DEANNE.

● “Nilikasirika. Nilihisi kuwa nimedanganywa, yaani, nilihisi kuwa matumaini na malengo yangu hayana maana yoyote.”—LUIS.

Huenda hata usiwazie kwamba inawezekana kuwa umedanganywa kumhusu Mungu. Yaelekea mambo unayojua kumhusu uliyasikia kutoka kwa mtu unayemwamini na ambaye hawezi kamwe kukuumiza kimakusudi, kama vile mzazi wako, kasisi, pasta, au rafiki wa karibu. Huenda umeamini fundisho fulani katika maisha yako yote. Lakini je, hukubali kwamba fundisho fulani linaweza kuwa la uwongo ingawa watu wengi wanaliamini? Aliyekuwa rais wa Marekani, Franklin D. Roosevelt alitambua jambo hilo, kwa kuwa alisema: “Kurudia-rudia uwongo hakuufanyi kuwa ukweli.”

Unaweza kujua jinsi gani kwamba umedanganywa? Wakati mmoja Yesu alisali hivi kwa Mungu: “Neno lako ni kweli.” (Yohana 17:17) Ndiyo, Neno la Mungu, Biblia, linatusaidia kutofautisha ukweli na uwongo.

Acha tuone mafundisho matano ya uwongo kumhusu Mungu ambayo Biblia inafunua. Utaona jinsi ukweli unavyoweza kubadili maisha yako yawe bora.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine