Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w13 15/1 uku. 32
  • Kampanye Iliyopangwa Vizuri Inazaa Matunda

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kampanye Iliyopangwa Vizuri Inazaa Matunda
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “ALIWAZIA NI MUTU MUKUBWA”
  • Unaweza Kusali Namna Gani Juu Mungu Akusikie?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Walijitoa kwa Kujipendea Katika Inchi ya Norvège
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Kampanye ya Kugawia Watu Mialiko ya Ukumbusho Itaanza Tarehe 2 Mwezi wa 4
    Huduma Yetu ya Ufalme—2011
  • Kampanye ya Kuwaalika Watu Kwenye Ukumbusho Itaanza Tarehe 17 Mwezi wa 3
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
w13 15/1 uku. 32

Kampanye Iliyopangwa Vizuri Inazaa Matunda

[Picha kwenye ukurasa wa 32]

María Isabel ni binti muhubiri mwenye bidii katika muji wa San Bernardo katika inchi ya Chilie huko Amerika ya Kusini. Yeye na familia yao ni wa kabila la Mapuche. Familia yao nzima iliunga mukono kwa furaha mupango wa kuunda kutaniko mupya katika luga ya Wamapuche, inayoitwa pia Mapudungun.

Tangazo lilipofanywa kwamba Ukumbusho wa Kifo cha Kristo utafanywa katika luga ya Mapudungun na kwamba kuna mialiko 2 000 ya kugawia watu katika luga hiyo, jambo hilo lilimufanya María Isabel afikiri sana. Basi atafanya nini ili kusaidia? Alikumbuka habari kuhusu matokeo mazuri ambayo vijana wengine Mashahidi walipata walipohubiria wanafunzi wenzao na walimu wao. Alizungumuza jambo hilo na wazazi wake, na wote pamoja waliamua kwamba María Isabel afikirie njia atakayotumia ili kugawa mialiko kwenye masomo. Alitumia njia gani?

Kwanza, aliomba wakubwa wa masomo ruhusa ya kubandika karatasi moja kwenye mulango mukubwa wa kuingilia. Walimukubalia na pia walimusifu kwa wazo hilo. Siku moja asubuhi, wakati wa kuita majina ya wanafunzi, mukubwa wa masomo alitumia kikuza sauti na kufanya tangazo kuhusu mualiko huo!

Kisha, María Isabel aliomba ruhusa ya kuingia katika kila somo. Kisha kupewa ruhusa na walimu, alikuwa anaingia katika kila somo na kuuliza ikiwa kuna wanafunzi wanaozungumuza luga ya Wamapuche. María Isabel anasema hivi: “Nilifikiri kama labda nitapata tu wanafunzi 10 ao 15 katika masomo yote, lakini walikuwa wengi na niligawa mialiko 150!”

“ALIWAZIA NI MUTU MUKUBWA”

Mwanamuke mumoja aliyeona mualiko huo kwenye mulango wa masomo, alitafuta mutu wa kumupatia maelezo zaidi kuhusu tukio hilo la ukumbusho. Wazia namna alivyoshangaa walipomuongoza kwenye binti wa miaka 10! María Isabel anasema hivi akiwa mwenye kicheko: “Aliwazia ni mutu mukubwa.” María Isabel alimutolea mualiko na maelezo mafupi, kisha akamuomba adresi yake ili yeye na wazazi wake waweze kumutembelea na kumuelezea mengi kuhusu Ufalme wa Mungu. Wahubiri 20 wanaotumikia katika eneo la luga ya Mapudungun walifurahi kabisa kumuona mwanamuke huyo akija kwenye Ukumbusho, na Wamapuche wengine 26 wenye kupendezwa. Sasa kuna kutaniko lenye kuendelea vizuri!

Hata iwe una miaka ngapi, je, unaweza kufikiria kualika wanafunzi wenzako ao wafanyakazi wenzako kwenye Ukumbusho, kwenye hotuba ya watu wote, ao kwenye mukusanyiko wa wilaya? Ili ujue namna ya kufanya, tafuta katika vichapo vyetu habari za ndugu na dada waliofanya hivyo na kupata matokeo mazuri. Pia, umuombe Yehova roho takatifu yake ili ikusaidie kusema bila woga. (Lu. 11:13) Ukifanya hivyo, wewe pia unaweza kushangazwa na matokeo utakayopata na hilo litakutia moyo sana kwa kuwa ulijikaza kupanga mambo vizuri.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine