Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/1 uku. 3
  • Kifo Ndio Mwisho wa Mambo Yote?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kifo Ndio Mwisho wa Mambo Yote?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wakati Mutoto Wako Anauliza Juu ya Kifo
    Amuka!—2015
  • Sababu Gani Watu Wanakufa?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • Wafu Wako mu Hali Gani?
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • “Ninafanya Vitu Vyote Kuwa Vipya”
    ‘Tumuimbie Yehova kwa Furaha’
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/1 uku. 3
Habari ya mutu aliyegongwa na motokari alipokuwa akitembea kwa miguu

KICHWA | JE KIFO NDIO MWISHO WA MAMBO YOTE?

Uchungu wa Kifo

Kifo ni habari yenye kuhuzunisha. Watu wengi hawapendi kuzungumuza juu ya kifo. Lakini siku moja, tutalazimika kupambana nacho. Na uchungu wa kifo ni mukali na wenye kuumiza sana.

Hakuna kitu kinachoweza kututayarisha vizuri ili kupambana na kifo cha muzazi, bibi, bwana, ao mutoto. Musiba unaweza kutokea kwa gafula ao baada ya muda murefu. Iwe musiba ulitokea namna gani, maumivu ya kifo hayawezi kuepukwa, na yanaweza kuleta matokeo mabaya sana.

Antonio, ambaye baba yake alikufa kwa kugongwa na motokari, anasema hivi: “Ni kama vile mutu fulani anafunga nyumba yako na anaenda na funguo. Hauwezi kurudia nyumbani, hata kwa muda mufupi. Unaendelea tu kukumbuka kwamba ulikuwa na nyumba. Hilo ni jambo jipya lakini ni la hakika. Ijapokuwa unajaribu kukataa jambo hilo, kwa sababu linaonekana kuwa lisilo la haki, hakuna jambo lolote unaweza kufanya.”

Alipofiwa na bwana yake, Dorothy, aliyekuwa na miaka 47, aliamua kutafuta majibu ya maulizo fulani juu ya kifo. Akiwa mwalimu wa masomo ya watoto ya Siku ya Yenga, hakuwa anafikiri kwamba kifo ndio mwisho wa mambo yote. Lakini Dorothy hakujua ni jambo gani linalotokea mutu anapokufa. Alimuuliza muhubiri wa kanisa lao la Anglikani hivi: “Ni nini kinatufikia tunapokufa?” Muhubiri huyo akamujibu: “Kwa kweli, hakuna mutu anajua. Tunapaswa tu kungojea na kuona.”

Je, tunapaswa tu “kungojea na kuona”? Je, kuna namna ya kujua ikiwa kifo ndio mwisho wa mambo yote?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine