BIBLIA INASEMA NINI?
Ni nini kinatufikia wakati tunakufa?
WATU FULANI WANAAMINI kama wakati mutu anakufa, sehemu fulani ya mwili wake inaenda kuishi mahali pengine, lakini wengine wanaamini kama kifo ni mwisho wa mambo yote. Wewe unaamini nini?
MAMBO BIBLIA INASEMA
‘Wafu, hawajue lolote kamwe.’ (Mhubiri 9:5) Wakati tunakufa, hatuko tena.
MAMBO MENGINE YENYE TUNAJIFUNZA KATIKA BIBLIA
Adamu, mwanaume wa kwanza, alirudia katika mavumbi wakati alikufa. (Mwanzo 2:7; 3:19) Kama yeye, wale wote wenye wanakufa wanarudia katika mavumbi.—Mhubiri 3:19, 20.
Wakati mutu anakufa, anaondolewa hatia ya zambi zake, ao anasamehewa. (Waroma 6:7) Hakuna malipizi mengine juu ya zambi kisha mutu kufa.
Watu waliokufa wanaweza kuishi tena?
UNAWEZA KUJIBU NINI?
Ndiyo
Hapana
Pengine
MAMBO BIBLIA INASEMA
‘Kutakuwa ufufuo.’ —Matendo 24:15.
BIBLIA INATUFUNDISHA TENA NINI?
Mara nyingi, Biblia inalinganisha kifo na usingizi. (Yohana 11:11-14) Mungu anaweza kuamusha mutu mwenye amekufa, kama vile tunaweza kuamusha mutu mwenye kulala usingizi.—Ayubu 14:13-15.
Biblia inazungumuzia watu mbalimbali wenye walifufuliwa, na hilo linatupatia sababu ya muzuri ya kuamini kama watu waliokufa watafufuliwa.—1 Wafalme 17:17-24; Luka 7:11-17; Yohana 11: 39-44.