Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 4 uku. 8
  • Sababu Gani Biblia Imeokoka?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu Gani Biblia Imeokoka?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Ni Neno ya Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Historia ya Maana
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Musaada Zaidi Kwa Ajili Ya Familia
    Amuka!—2018
  • Uko na Mawazo Gani Juu ya Biblia?
    Uko na mawazo gani juu ya Biblia?
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 4 uku. 8

HABARI KUBWA | BIBLIA ILIOKOKA NAMNA GANI?

Sababu Gani Biblia Imeokoka?

Biblia imeokoka. Ndiyo sababu unaweza kuipata na kuisoma leo. Na wakati unachagua tafsiri ya muzuri ya Maandiko, unaweza kuwa hakika kwamba unasoma Biblia yenye kupatana na maandishi ya kwanza.a Lakini, sababu gani kuna habari nyingi zenye kushangaza juu ya namna Biblia iliokoka hata kama kulikuwa hatari ya kuharibika, upinzani, na hatari ya kutaka kubadilisha kimakusudi ujumbe wake? Biblia iko na jambo gani la pekee?

“Sasa, niko hakika kwamba Biblia yenye niko nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu”

Wanafunzi wengi wa Biblia wamefikia kuwa na mawazo yenye mutume Paulo alikuwa nayo. Aliandika hivi : “Andiko lote limeongozwa na roho ya Mungu.” (2 Timotheo 3:16) Wanaamini kwamba Biblia imeokoka kwa sababu Biblia tu ndiyo Neno la Mungu na kwa sababu Mungu amelinda Neno lake mupaka leo. Faizal, mwenye tulitaja katika habari ya kwanza ya gazeti hili alifikia kuamua kuchunguza yeye mwenyewe mawazo yenye watu walisema juu ya Neno la Mungu kwa kujifunza Biblia. Mambo yenye alivumbua yalimushangaza. Kisha, alitambua kwamba Biblia haiunge mukono mafundisho mengi yenye dini nyingi zenye kujiita kuwa za Kikristo zinafundisha. Zaidi ya hilo, moyo wake uliguswa wakati alijifunza kusudi la Mungu juu ya dunia kama vile inaonyeshwa katika Neno Lake.

Anasema hivi: “Sasa, niko hakika kwamba Biblia yenye niko nayo ni zawadi kutoka kwa Mungu. Tena, Mungu mwenye aliumba ulimwengu wote, ana uwezo wa kutupatia kitabu na kukilinda kwa ajili yetu. Kusema jambo lenye kuwa tofauti na hilo ni kuonyesha kama uwezo wa Mungu Mweza-Yote, uko na mipaka! Na mimi ni nani ili niseme kama uwezo wa Mungu uko na mipaka?”—Isaya 40:8.

a Ona habari “Jinsi ya Kuchagua Tafsiri Nzuri ya Biblia” katika Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 5, 2008.

Habari zenye tumetoka kuona zimeonyesha namna Biblia ililindwa. Lakini sasa, namna gani unaweza kuwa hakika kwamba Biblia ni “neno la Mungu” kabisa na kwamba haiko kitabu cha hadisi za kuwazia tu? (1 Wathesalonike 2:13) Angalia video fupi yenye kichwa Tunawezaje Kuwa na Hakika Kwamba Yale Yaliyoandikwa Katika Biblia Ni ya Kweli? kwenye adresi ya Internete www.jw.org. (Fungua kichwa MACHAPISHO > VIDEO)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine